Jibu: Turejee..
Kumbukumbu la Torati 11:15 “Nami nitakupa nyasi katika MAVUE yako kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
“Mavue” ni kiswahili kingine cha “mashamba”….shamba likiwa moja linaitwa “VUE” yakiwa mengi “MAVUE”.
Kwahiyo hapo anaposema “Nitakupa nyasi katika mavue yako”.…maana yake nitakupa nyasi katika mashamba yako.
Hii ni ahadi ya Mungu kwa wana wa Israeli, na ni ahadi ya MUNGU kwetu pia, ikiwa tutayashinda
Tuanzie ule mstari wa 13..
Kumbukumbu 11:13-15 “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote, 14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako. 15 Nami nitakupa nyasi katika MAVUE YAKO kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
Kumbukumbu 11:13-15 “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote,
14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.
15 Nami nitakupa nyasi katika MAVUE YAKO kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
Neno hili pia tunalisoma katika
Maandiko yafuatayo…
1Samweli 25:15 na 1Samweli 30:11.
Je umempokea Bwana YESU KRISTO?..
Kama bado unasubiri nini mpendwa?..Fahamu ya kuwa kwa jinsi unavyozidi kuendelea kuishi maisha ya dhambi
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Print this post
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ