1 Wakorintho 13:9-10
[9]Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; [10]lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
[9]Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
[10]lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
Biblia inatupa dira kamili wa maisha yetu, na namna ambavyo tunapaswa kumwelewa Mungu na utendaji kazi wake kwetu sisi. Ni vizuri wewe kama mtoto wa Mungu, kujua ni kipi umewezeshwa kujua na kipi hujawezeshwa..
Watu wengi tunapopitia hili andiko, tunashindwa kulitafakari kwa ndani zaidi, na matokeo yake yanakuwa ni kuishi maisha ya kuhangaika na kutaabika tukidhani kuwa Mungu hasemi au Mungu hajibu.
Roho Mtakatifu anatufundisha kuwa katika eneo la kujua mambo yote, sisi hatujakusudiwa kwa sasa. Hujakusudiwa kuishi duniani ujue kila kitu.
Bali kwa sehemu ndogo tu.. kwa mfano wa sasa tunasema unapewa vidokezo(trailer) vya filamu. Lakini picha nzima ya filamu yote hutaijua sasa, mpaka utakapovuka ng’ambo.
Ndivyo ilivyo katika mambo yote, kwamfano ikiwa mtu unamwomba Mungu akupe kujua jambo Fulani, au akufunulie kila kitu kinachoendelea au kitakachoendelea, au akufunulie kila kitu kinachohusu maisha yako ya sasa au ya baadaye…usitarajie utaonyeshwa taswira yote, kwamba leo itakuwa hivi, kesho vile, mwaka vile, wiki ijayo vile n.k. ndugu haiwi hivyo Mungu atakugusia kwa sehemu tu..ndogo ndogo ambazo hizo zitakupa picha fulani…lakini si taswira yote, kwasababu tumepewa kujua kwa sehemu.
Ikiwa wewe ni nabii, Mungu amekuonyesha jambo, toa unabii kama ulivyoonyeshwa usianze kuweka matukio yako ambayo hujaonyeshwa ..mwisho wa siku utajichanganya mwenyewe au jamii unayoitabiria..kwasababu hata iweje huwezi jua kila kitu, huwezi funuliwa kila jambo hata ulieje.
Ndio yaliyomkuta Yohana Mbatizaji.. aliweka matarajio yake, fikra zake, na kuziamini sana mwisho wa siku akamwona hata Kristo siye…ilihali alimshuhudia mwenyewe ndiye.
Kwamfano leo utaenda kwa nabii, kisha akaonyeshwa kwenye maono umebeba mtoto wa kiume, sasa kwasababu atataka kujifanya yeye ni nabii mwenye viwango vya juu ataanza kutoa simulizi zake za uongo…Bwana ananionyesha utabeba mtoto wa kiume hivi karibuni, hivyo andaa nguo zake, pia mwombee, mwandalie na sadaka ya shukrani.
Lakini kumbe Mungu hakumaanisha atampa mtoto, alimaanisha atamfanikisha na kumfanya mlezi wa mayatima.. kwa taswira ile ya mwanamke aliyembeba mtoto.
Matokeo yake yule mwanamke anaweka matarajio yake hapo, miaka inapita hapati mtoto, baadaye yule nabii anaonekana mwongo. Kumbe sio..ni kwasababu alijaribu kuvuka kipimo cha unabii alichopimiwa.
Angesema Bwana amenionyesha hivi na hivi.. zaidi ya hapo sijui, Mungu atakufunulia mwenyewe, ingetosha kumpa yule mama wigo wa kutafakari maono yake, na yatakapotimia atajua kuwa kumbe tafsiri yake ndio ile.
Vivyo hivyo hata wewe mwenyewe..utamwomba Mungu akuthibitishie jambo Fulani, utagundua mara nyingi hupewi taarifa za kujitosheleza juu ya hilo jambo, utapewa ishara tu, wakati mwingine alama Fulani, .
Ukiona hivyo usihangaike sana kupata picha yote ya kila kitu, bali chukua hatua na Bwana atakuwa na wewe..
Kuishi kwa Imani.
Jambo kuu tuliloumbiwa na Mungu, ni kuishi kwa imani sio kwa kuona.
Jambo lolote lifanye kwa imani, kwasababu hujapewa kujua kila kitu kwa ufasaha wote sasa..
Ikiwa na kushuhudia huwezi kungoja kwanza Mungu akuonyeshe jina la mtaa, aina ya mtu utakayekutana naye, nguo aliyovaa na jina lake ndipo uende…hapo ndugu utangoja sana..
Lakini unaenda kwa imani,.ukiamini lile Neno kwamba “nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari,” na matokeo yake unakutana na yule mtu ambaye Mungu amemkusudia kati ya wengi.
Hivyo ndugu fahamu kuwa tunajua kwa sehemu, tunatoa unabii kwa sehemu..
Ndio maana anamalizia kwa kusema;
1 Wakorintho 13:12
[12]Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.
Tembea kwa Imani. Unabii, maelekezo, taarifa, vinapokuja machache, ni wakati sasa wa kuchukua hatua ya kutenda kuliko kusubiri hapo muda mrefu.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.
KUSUDI LA KWANZA LA KUCHAGULIWA NA MUNGU NI LIPI?
PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.
Print this post
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ