(Masomo maalumu ya utakaso)
Jina la Bwana na Mwokozi YESU KRISTO libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia yetu.
Je unazijua sehemu Nne (04) za Mwili wa Bwana YESU zilizotobolewa na kumwaga damu pale msalabani?.. Basi kama huzifahamu sehemu hizo ni 1)Kichwa, 2)Mikono, 3)Ubavu na 4)Miguu.
Tutazame moja baada ya nyingine, na pia tujifunze kwanini ni viungo hivyo ndio vilimwaga damu na kwanini vinahitaji utakaso sana.
1.KICHWA
Maandiko yanatuonyesha kuwa Bwana YESU alivikwa taji ya Miiba ..
Mathayo 27:28 “Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu. 29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
Mathayo 27:28 “Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
Kwanini sehemu hii ya kichwa ilimwagika damu?.. Ni kwasababu kichwani ndiko kwenye ufahamu wa mtu, na milango yote ya ufahamu kama macho, masikio, pua na ulimi vipo huko.. na kwa kupitia vitu hivyo watu wanafanya dhambi, kwamfano kupitia ulimi mtu atasema uongo, atatukana, atakejeli n.k,
Kupitia macho mtu atatazama kwa kiburi sawasawa na (Mithali 6:17), kupitia macho mtu ataangalia uchafu, na pia kupitia masikio mtu atasikiliza mabaya, usengenyaji, njama mbaya n.k
Kwahiyo ni lazima Damu ingekota usoni kutakasa uso wa Bwana kwani dhambi zetu zote alizibeba yeye
2. UBAVU.
Biblia pia inatuonyesha kuwa Ubavuni mwa YESU palitokea damu..
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu; 34 Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;
34 Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Sasa kwanini ubavuni?.. Ni kwasababu ubavuni ndipo Moyo wa mtu ulipo, na hata wale Askari wa kirumi walikusudia kuhakiki kifo cha Bwana YESU kwa kumpiga mkuki katika moyo..
Na moyo ndio ubebao mawazo yote ya mtu ikiwemo mawazo mabaya..
Mathayo 15:19 “Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano”
Kwahiyo kulikuwa na sababu kwanini damu itokea moyoni ni kuonyesha utakaso wa Moyo..
3. MIKONO
Pia Biblia inatuonyesha kuwa mikono ya Bwana YESU ilitoka damu..
Yohana 20:25 “Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo”.
Kwanini mikono?.. Kwasababu mikono ndio inayoshika, inayofanya kazi za kila namna, (zilizo njema na mbovu)…watu wanafanya mauaji kwa kutumia mikono yao, kwa ufupi mikono ni nyenzo kubwa ya mabaya ndani ya mtu ndio maana katika ile ile Mithali maandiko yanasema, moyo uwazayo mabaya ni machukizo kwa Bwana..
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17 macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
4. MIGUU
Biblia inatuonyesha sehemu nyingine ya mwisho ya mwili wa Bwana YESU iliyomwagika damu ni miguu..
Luka 24:38 “Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? 39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Luka 24:38 “Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Miguu ni kiungo kingine chenye kuutia mwili mzima unajisi..watu wanatumia miguu kukimbilia mabaya, kukimbilia uzinzi, mauaji, ulevi n.k
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
Sasa viungo hivi ni lazima vitakaswe kwa damu ya YESU, na vinatakaswaje?
Vinatakaswa kwanza kwa kumwamini Bwana YESU KRISTO, na kuomba na kuacha dhambi.. zingatia hili neno “kuacha dhambi” kupitia viungo hivyo.
Angalia miguu yako inachokimbilia, je ni chema au ni kibaya.. jiuepushe miguu yako na njia za wakosaji, angali macho yako yanachokitazama ni chema au kibaya, jiepushe na kutazama mambo yasiyofaa, vivyo hivyo na mikono yako na moyo wako, angalia sana unavyovifuatilia na kuvifanya.
Mwisho, kumbuka tunaishi katika siku za mwisho, na Kristo amekaribia sana kurudi, wakati wowote parapanda ya mwisho italia na hukumu ya mataifa itaanza, je umejiandaaje?
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
UZURI WA MAJIVU.
IPO NJIA YA MKATO YA KUFIKA KIWANGO VYA MBALI VYA KIROHO.
Na kipenu ni nini (Isaya 1:8)
Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Print this post
Ikiwa unahitaji Maombezi, wasiliana nasi kwa namba hizi bure. Lakini ikiwa una swali na unahitaji msaada wa kimaandiko andika ujumbe wako katika fomu uionayo chini.
📞 +255 789 001 312
📞 +255 693 036 618
Jina lako
Barua Pepe
Nchi (Lazima)
Namba Ya Simu (Muhimu)
Kichwa cha Ujumbe
Ujumbe Wote
Δ
Mungu ana makusudi makubwa na wewe, kwanza kukuokoa, na pili kukudhihirishia wema wake wote maishani mwako. Maamuzi haya ya kumpokea Bwana Yesu ni ya busara sana ambayo utayafurahia milele yote.
Ili kuupokea wokovu basi hapo ulipo unaweza kuchukua hatua ya imani, kwa kupiga magoti, kisha utafuatisha sala hii kwa imani. Na hakika wakati huu huu utaupokea wokovu bure.
Sema maneno haya kwa sauti:
“Bwana Yesu ninaamini kuwa wewe ni mwana wa Mungu, ninaamini kuwa ulikufa kwa ajili ya dhambi zangu, ukafufuka tena, na sasa unaishi milele. Ninakiri kuwa mimi ni mwenye dhambi, nimestahili hukumu na kifo. Lakini leo ninaungama makosa yangu na dhambi zangu zote, na kuyasalimisha maisha yangu kwako. Ninaomba msamaha wako Bwana Yesu, liandike sasa jina langu katika kitabu cha uzima. Nakukaribisha moyoni mwangu, uwe na Bwana na mwokozi wangu tangu sasa. Nimeamua kukutii na kukufuata wewe sikuzote za maisha yangu. Asante Bwana Yesu kwa kunisamehe na kuniokoa. Amen”
Kwa sala hiyo fupi, tayari Bwana Yesu ameshakusamehe dhambi zako, kumbuka kusamehewa sio kumlilia Mungu sana kwa wingi wa dhambi zako ulizomtenda..Kana kwamba unamshawishi Mungu akusamehe. Hapana.
Mungu tayari alishawasamehe wanadamu kwa kifo cha Yesu Kristo pale msalabani. Hivyo ni jukumu tu la wanadamu kuukubali msamaha wa dhambi mioyoni mwao kwa kuamini Kile ambacho Mungu alikifanya Kupitia Yesu Kristo.
Ndicho ambacho Mungu alikisema hapa
Warumi 10:9-10
[9]Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. [10]Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Kuamini kunakozungumziwa hapo ndio huko kukubali kwenyewe kazi ya Yesu aliyoifanya ya kuondoa dhambi za watu, kwa kufa kwake pale msalabani.
Ni sawa na mtu anakuja kukwambia nakupa hii almasi, ukiipokea basi umaskini wako wote umeondoka.
Sasa wewe kwa upande wako sio tena kukililia, hapana bali unawajibu tu wa kuamini kile kitu anachokupa, kwamba kinauwezo wa kuondoa umaskini..Ambapo sasa hudhihirishwa kwa kukipokea.
Ukishapokea sasa ndio matunda yake unayaona, kinyume chake ni kwamba bila kuamini kamwe huwezi kupokea, na umaskini utaendelea kubaki kwako daima.
Ndicho Yesu alichokileta Kwetu. Ambacho ni msamaha wa dhambi. Akasema ukiamini Kuwa nimekufa kwa ajili ya dhambi zako, ili zifutwe kabisa kabisa basi utaokoka. Hivyo pale unapoamini kwa kukubali kumfanya Yesu kuwa ndio Bwana na mwokozi wako tangu huo wakati na kuendelea, na kwamba alikufa kwa ajili yako..Basi dhambi zako zinakuwa zimeondolewa kuanzia huo wakati, haijalishi zilikuwa ni nyingi Kiasi gani.
Hilo tu, ndio maana sala hiyo fupi, ikiwa umeisema kwa dhati yatosha, kukufanya wewe kuwa mwana wa Mungu. Kwasababu tayari Umemkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wako. Hilo ni hakikisho lake.
Nini kinafuata? bofya hapa. >>>
Kataa fikra za shetani
Neema ni nini?
Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo?
Bofya hapa kurudi kwenye mwongozo mkuu wa mafundisho ya mwongofu mpya. >>
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10