Category Archive Mafundisho

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

Wimbo Ulio Bora 2:10-13

[10]Mpendwa wangu alinena, akaniambia,  Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,

[11]Maana tazama, kaskazi imepita,  Masika imekwisha, imekwenda zake;

[12]Maua yatokea katika nchi,  Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.

[13]Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.

Mahusiano yoyote yale hukumbwa na vipindi tofauti tofauti.ni sawa na dunia na misimu yake, kuna vipindi Vya kiangazi, vipindi vya masika, vipindi vya joto, na vipindi vya baridi…

Vivyo hivyo pia mahusiano yoyote hukumbwa na nyakati kama Hizi..

Watu wa agano la kale walikuwa katika nyakati ngumu za upendo na Mungu, nyakati zao zilijawa na misuko-suko, ukame na kutaabika, nyakati za jasho na damu…Kwasababu shetani alikuwa na nafasi kubwa katika maisha ya wanadamu, lakini walikuwa hawajamjua bado Mungu vizuri.

Lakini mwokozi alipokuja, alituliza dhoruba zote, mawimbi yote, jua lote, mizigo yote, na taabu zote ..alilitimiza hilo kwa kujitoa kwake pale msalabani. Ndio maana akasema yeye ni Bwana wa sabato, ( pumziko). Kwasababu Alikuja kuleta pumziko haswaa la pendo lake, ili mtu asikae katika masumbufu ya aina yoyote rohoni.

Hivyo leo hii anasema nasi kama mtu amwambiaye mpenzi wake habari za faraja..

10]Mpendwa wangu alinena, akaniambia,  Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,

[11]Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake; [12]Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika,

Huu ni wakati wa kuitikia wito wake mkuu wa upendo usio na usumbufu.. mpokee sasa ukuburudishe maishani. Akupe uzima wa milele, akupe faraja na tumaini uone maana ya maisha. Nyakati hizi ni za hatari, ulimwengu hauwezi kukupeleka popote, kinyume chake utaishia jehanamu tu ukiufuata, lakini ukimgeukia mwokozi na kumfuata utapata uzima wa milele.

SHALOM.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

Print this post

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

Wimbo Ulio Bora 8:6-7

[6]Nitie kama muhuri moyoni mwako,  Kama muhuri juu ya mkono wako;  Kwa maana upendo una nguvu kama mauti,  Na wivu ni mkali kama ahera.  Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.

[7]Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.

Habari hiyo inamzungumzia Bwana arusi ambaye anataka kuingia katika mahusiano ya ndani na bibi arusi wake, hivyo anaanza kwa kumwomba amkubali Kama “Muhuri” .

muhuri huwa unawakilisha umiliki halali wa kitu hicho..

Hivyo huyu Bwana arusi anamtaka bibi arusi akubali muhuri wake, katika  moyo wake na katika mkono wake…pande mbili…moyoni ikiwakilisha ndani yake ni mkononi nje, yaani upendo wa ndani na ule upendo wa nje…kumilikiwa kwa ndani lakini pia kumilikuwa kwa nje..

Na matokeo Ya kufanya hivyo ndio hapo anaendelea kueleza sifa za huo upendo akisema upendo una nguvu kama mauti…yaani Kama vile mauti isivyo pingika juu ya mtu, kwamba kufa atakufa tu, vivyo hivyo upendo wa kweli ukimnasa mtu haupingiki..atamlinda tu.

lakini pia anasema wivu wake ni mkali kama Ahera,  ni mfano huo huo, maana yake hauvumilii maovu, pale unaponajisiwa…ni lazima utatoa tu matokeo..unakula Kama moto moyoni…ndio Uliomla Bwana Yesu alipoona nyumba ya Baba yake imegeuzwa kuwa pango la wanyang’anyi akatengeneza kikoto na kuanza kuharibu kwa makusudi kazi zote za kipepo zilizokuwa zinaendelea pale hekaluni…wivu wa upendo huharibu lakini vile vilivyo viovu.

Bado anasema ‘maji mengi na mito Haviwezi kuuzima, Kama mtu angetoa badala ya upendo  Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa’

yaani hata mtu akijaribu kuuzimisha kwa hongo za kifedha anafanya kazi bure…

Ni kufunua nini rohoni?

Nguvu ya upendo wa Kristo kwetu pale tunapoupokea vizuri..tunakuwa salama milele ndani Yake..

Lakini Hatua ya kwanza Kristo anataka kututia muhuri wake moyoni na mkononi…na muhuri huo ni Roho Mtakatifu(Waefeso 4:30), anataka udhihirisho wa Roho uonekane mioyoni mwetu, lakini pia mwilini (kwa matendo yetu).

Utakatifu wa ndani na nje.

Kuna Watu wanampokea Yesu moyoni tu, lakini lakini badiliko la nje hawana habari nalo, wanamkiri kwa vinywa vyao lakini kwa matendo yao wanamkana..

Tito 1:16

[16]Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.

Hapo bado upendo wa kweli haijafunuliwa…lakini pale tunapodhamiria kumpokea Kristo Kwelikweli, basi nguvu ya upendo wake inatunasa na matokeo yake yanakuwa hata tufani ya namna gani ije, yeye mwenyewe anatushika, hata dunia nzima itutenge bado hatuwezi tikiswa, hata tuahidiwe utajiri na mali zote duniani, bado upendo wetu hauwezi kupungua kwa Kristo, kwasababu ni wewe mwenyewe aliyetunasa kwa agano la muhuri rohoni na mwilini.

Yesu alisema…

Warumi 8:35-39

[35]Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu. 

Bwana akubariki.

Je upo tayari leo kuokoka? Kama ni ndio basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii kwa msaada huo bure.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO

Maombi Maalumu ya Kuombea Ndoa.

Print this post

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO


Wimbo Ulio Bora 5:2-6

[2]Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha! 

Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, 

Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku. 

[3]Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje? 

[4]Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake. 

[5]Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane,  Penye vipini vya komeo. 

[6]Nalimfungulia mpendwa wangu,  Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; 

(Nimezimia nafsi yangu aliponena), 

Nikamtafuta, nisimpate,  Nikamwita, asiniitikie. 

Habari hii inaeleza kisa cha mtu na mpenzi wake, ambayo inafunua mahusiano ya mtu na Kristo, na jinsi mwitikio Wake unavyopaswa uwe.

 

Hapa anaonyesha mwanamke mmoja akiwa ndani usiku amelala peke yake na mara akasikia mpenzi wake anabisha Mlango amfungulie, 

Lakini  alijawa na uzito, akaanza kukawia-kawia, pengine huwenda kwasababu ya starehe ya kitanda, au kuna mambo yake mengine ya siri alikuwa anayafanya

Lakini bado mpenzi wake aliendelea kugonga, bila mfanikio ya kufunguliwa…na safari hii akatoa mpaka maneno ya upendo yamkini yatamshawishi ili aje kufungua kwa haraka. Lakini bado hakufua dafu.

Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, 

Mpaka dakika ya mwisho, alipogonga, na mbisho ule kuingia moyoni mwa yule mwanamke, ukamchoma ndipo akatoka haraka na kwenda kumfungulia..

Lakini kwa bahati mbaya hakumkuta, kumbe tayari alishaondoka…akaanza kutoka kumtafuta bila mafanikio..na matokeo yake huko nje kukutana na madhara mengine.

Ni nini Kristo analifundisha kanisa lake?

Hili ni jambo ambalo watu wengi humfanyia Kristo rohoni sasa…Anasema..anasema..

Ufunuo wa Yohana 3:20

[20]Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. 

Lakini watu hukawia-kawia kwasababu ya udanganyifu wa mambo Ya duniani, mwingine atasema ngoja kwanza nimalize ujana, ndio nitaokoka, mwingine ngoja nipate kazi mwingine ngoja niolewe, mwingine ngoja ifike mwakani, mwingine ngoja nikimaliza masomo ndio nitampokea Yesu..n.k

Ndugu Saa ya wokovu ni sasa Kristo anakuita, wakati ndio huu, usipoufungua moyo wako sasa, utafika Wakati utamtafuta Kristo na hutampata…

Luka 13:24

[24]Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze. 

Luka 12:36-40

[36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. 

[37]Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. 

[38]Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. 

[39]Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. 

[40]Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu. 

Okoka leo ndugu, neema ya wokovu ipo sasa lakini haitadumu milele..hiyo sauti inayoita moyoni mwako itii, haraka, starehe za duniani zinapita, maisha yanapita,  ikiwa upo tayari kumkabidhi Bwana maisha yako, basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure kwa msaada huo..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mshulami ni msichana gani?

Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).

Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).

 

Print this post

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

Wimbo Ulio Bora 3:1-4

[1]Usiku kitandani nalimtafuta mpendwa wa nafsi yangu, Nalimtafuta, nisimpate.

[2]Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini,  Katika njia zake na viwanjani,

Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu. Nikamtafuta, nisimpate.

[3]Walinzi wazungukao mjini waliniona; Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?

[4]Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena,  Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu,  Chumbani mwake aliyenizaa.

Kitabu cha wimbo ulio-bora, ni kitabu ambacho huchukiliwa kimwili na watu wengi kana kwamba kiliandikwa mahususi kwa wana-ndoa.. Jambo ambalo sio kweli, Ikumbukwe kuwa dhumuni kuu la biblia ni kutueleza WAZO la Mungu, juu yetu ambalo hilo alilikamilisha kifasaha kupitia Yesu Kristo. Hivyo popote pale unapopasoma kwa namna moja au nyingine inaeleza kusudi la Mungu kwetu, katika kuyatimiza mapenzi yake..

Na ni kawaida yake tangu zamani  kutumia mifano halisi ya namna mbalimbali ili kudhihirisha kusudi lake kamilifu kwetu.

Kwamfano ameweka familia, tujue sifa za wazazi ili tunapomwita Mungu Baba, tujue tabia za ubaba hasaa zipoje…Ameweka mabwana na watumwa ili tunapomwita yeye Bwana tujue sisi tunapaswa tuweje kwake kama watumwa..

Vivyo hivyo ameweka ndoa, na akajifunua kwetu kama mume, na sisi kanisa ni mke wake…Hivyo anataka tujue kama vile upendo wa mke na mume ulivyo ndivyo alivyo yeye kwetu sisi.

Sasa Katika habari hii, tunaona sifa ya upendo ambao Mungu anataka sisi tuuonyeshe kwake, Upendo usio ule wa upande mmoja, bali na upande wa pili, yaani sio  tu yeye kututafuta sisi wakati wote hapana bali Na sisi tumtafute yeye..

Anaeleza kwa mfano wa igizo picha ya  mwanamke ambaye yupo sikuzote na mpenzi Wake kitandani, lakini ikatokea siku moja alipoamka usiku hakumwona kitandani Mwake…

Hivyo hakuweza kuendelea kulala angali mumewe hayupo, ikambidi atoke aanze Kumtafuta usiku ule ule, sio kwa siri Bali hadharani tena sehemu zenye hatari ambazo walinzi tu usiku hupita kufanya doria..Na alipokutana Nao akawauliza juu ya mpenzi wake kama wamemwona, lakini Baadaye kidogo alimwona..akamkumbatia na kurudi naye mpaka mahali pao maalumu.

Ufunuo wake ni upi.

Yapo majira wewe kama mwana wa Mungu utapitia pengine hali fulani ya kushuka viwango kiroho, (ukame wa kiroho)

Lakini ukiwa na upendo wa kweli kwa Mungu wako, ni wazi kuwa hutakaa tu na kusema Mungu nisaidie…Hapana Utachukua tu hatua kama za huyu mwanamke ya kuamka na kuanza kutafuta namna ya kumtafuta mpenzi wako (Kristo) yaani kurejesha viwango vyako vya mwanzoni, hata kwa kugharimika raha, au vitu n.k..

Ndio hapo mtu hutenga muda mwingi wa maombi, mikesha, mifungo n.k.

Na kama vile yule Mwanamke alipowafuata walinzi usiku, kuwauliza habari za mumewe…Ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye kiu na pendo na Mungu hataridhika kutembea yeye kama yeye tu, ataulizia msaada mpaka kwa viongozi wake wa kiroho apate mwongozo..(ambayo hufunua wale walinzi). Na hatimaye kufikia kilele cha mahusiano na Mungu wake tena.

Ndugu, kumbuka kuwa furaha, na amani, uzuri wa Kristo sio tu wa kuletewa sikuzote, bali pia wa kutafuta…Ni kweli siku za kwanza za wokovu uliona Kristo akijifunua Kwako kwa namna za ajabu, hata kama hukufanya lolote lakini sasahivi ni kama huoni moto ule ule uliokuwa nao…jua tu si kwamba umetenda dhambi au umemkosea Mungu…hapana ni kwamba Mungu anataka amke sasa mtafuta mpenzi wako..kudhihirisha upendo wa kweli..

Ndicho Yesu alichowaambia wale waandishi na mafarisayo juu ya wanafunzi wake..

Marko 2:18 Nao wanafunzi wake Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
19 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.
20 Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku ile

Ongeza mikesha, mifungo, kusoma Neno sana…Na hatimaye utavipata na furaha yako itazidi ile ya kwanza…

Kwasababu upendo wa kweli hutafuta…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Naomba kujua maana ya haya maneno katika biblia..“Siti Msharifu”, “Mitalawanda” na “kulalama”

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Print this post

HEKIMA ILIYO SAHIHI, KATIKA HIMIZO LA UTOAJI SADAKA.

Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Yoashiliingiwa na wazo la kutaka kuikarabati nyumba ya Mungu (Hekalu), na kuamsha tena shughuli za kiibada zilizokuwa zimeharibiwa Na watawala wabovu waliotangulia..

Hivyo kwa kuwa alijua ukarabati unahitaji fedha, alichukua hatua ya kuwatoza watu kodi ya nyumba ya Mungu..Ambayo iliagizwa katika torati na Musa..(2Nyakati 24:9)

Hivyo akawateuwa  Walawi, walisimamie jambo hilo tangu mwanzo hadi mwisho, lakini likawa kama linacheleweshwa…

Mpaka baadaye akawauliza tena, kwanini kazi inacheleweshwa, kwa kuona hakuna chochote kilichofanyika..

Lakini mfalme akaja na mkakati mwingine, ili shughuli hiyo ifanyike kwa haraka na wakati, akaona kuliko Kuwalazimisha watu kulipa kodi ngoja aweke sanduku kubwa katika lango la hekalu na kupiga panda kwa watu wote wa Yuda waje kumtolea Mungu wao kwa hiari, bila shuruti..

Na wazo lile likapendwa na watu wengi, na hatma yake makusanyo yakawa mengi, kila siku mpaka wakapata fedha za kuwaajiri wajenzi ili kulikarabati hekalu, na kutengeneza vyombo vya nyumba ya Mungu.

2 Mambo ya Nyakati 24:6-14

[6]Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa BWANA, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda?

[7]Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya BWANA wamewapatia mabaali.

[8]Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya BWANA.

[9]Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea BWANA kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.

[10]Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha.

[11]Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele.

[12]Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya BWANA; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya BWANA, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya BWANA.

[13]Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara.

[14]Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya BWANA, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya BWANA, daima, siku zote za Yehoyada.

Ni nini tunafundishwa Na Roho Mtakatifu..

Utoaji wenye baraka na anaouhitaji Mungu ni ule wa hiyari na sio wa kulazimishwa…kama kanisa la Kristo Lazima tufikie hatua hii, kwamba viongozi hawawashurutishi watu kutoa mchango,mfano Zaka, Kama vile himizo la kodi, kwamba usipotoa unachukuliwa sheria ya kinidhamu …lakini pia watu nao wanawajibika wenyewe kumtolea Mungu kwa uaminifu na moyo..kanisa lifikiapo hatua hii ya kiroho, Mungu huliongezea baraka sana.

Usikubali kukumbushwa-kumbushwa, au kuhimizwa-himizwa kumtolea Mungu, Bali mtolee Mungu zaka zako, sadaka zako, kwa moyo wa furaha, Bwana atakubariki.

2 Wakorintho 9:6-8

[6]Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

[7]Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Bwana awabariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 21:3 Kutenda haki na hukumu  Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

SWALI: Nini maana ya Mithali 21:3

[3]Kutenda haki na hukumu  Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

JIBU:

Mstari huo unatufundisha mambo ambayo Mungu huvutiwa nayo zaidi…

Mungu hupendezwa zaidi na sisi tunapoishi maisha ya haki, tunatenda mema, tunawajali wengine, tunaishi sawasawa ni viwango vyake vya kiroho hapa duniani..kwake hiyo ni bora zaidi ya sadaka zetu tumtoleazo.

Sadaka huwakilisha mambo yote Ya kidini tunayoweza kumfanyia Mungu, mfano ibada, fedha, mifungo, maombi, kuhubiri, kuimba n.k

Bwana huvutiwa zaidi na mioyo na tabia zetu, na sio zile Ibada za nje tu..

Haimaanishi kuwa hapendezwi na hivyo vitu hapana…bali hivyo vifanywe baada ya kutii kwanza..

Tunaona jambo kama hilo amelisisitiza sehemu nyingi kwenye maandiko; Tukianzia kwa Sauli alimwambia, hivyo;

1 Samweli 15:22

[22]Naye Samweli akasema,  je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu  Sawasawa na kuitii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu,  Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.

Mika 6:6-8 inasema;

[6]Nimkaribie BWANA na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja?

[7]Je! BWANA atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?

[8]Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Soma pia..

Isaya 1:11-17 – Inasema…Bwana huchukizwa na sadaka za watu wanaishi katika dhambi

Hivyo ni lazima tujiulize Je! tunatenda haki kwa wengine?

Je! Tunatembea kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wetu?

Je! tunamtii Mungu, kuliko vitu vingine vyovyote?

Je tunawahurumia wengine…?

Mambo kama haya ndio yenye uzito zaidi kwa Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

MCHE MWORORO.

Print this post

Kijana ni nani kibiblia?

Biblia haitoi umri fulani maalumu kwamba mtu akiufikia huo basi ndio huitwa kijana.. Japokuwa ni mtu ambaye yupo umri wa hapo katikati yaani utoto na utu uzima, lakini hutambulika kwa kuangalia vitu kama hatua za ukuaji wake, uwajibikaji wake na uzoefu wake wa kimaisha.

Kwamfano katika biblia watu hawa walitajwa kama vijana.

  • Ishmaeli (mwanzo 21:14-20)
  • Isaka (Mwanzo 22:5)
  • Yusufu mwanzo 42:22. (Akiwa na miaka 17)
  • Mfalme Sauli (1Samweli 9:2)
  • Timotheo (1Timotheo 4:12)

Na wengine kadha wa kadha..

Yafuatayo ni Mambo ambayo kijana yeyote anatarajiwa awe nayo kibiblia.

1) Awe anamtafuta Mungu Na kulitii Neno la Mungu.

Mhubiri 12:1

[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

Zaburi 119:9

[9]Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako. 

2) Awe na hekima na tabia ya uongozi, (yaani wakati wote ajifunze kuwa kielelezo.)

1 Timotheo 4:12

[12]Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.

3) Awe na nguvu za rohoni, za kumshinda shetani.

Mithali 20:29

[29]Fahari ya vijana ni nguvu zao,..

1 Yohana 2:14

[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Lakini pia kijana anakabiliwa na tamaa za ujanani kama vile uzinzi, anasa,starehe..hivyo Anatarajiwa azikimbie wakati wote.

2 Timotheo 2:22

[22]Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.

Kutokana na vigezo hivyo tunaweza Kuona ujana pengine huanzia umri wa kubalehe, mpaka wakati mtu anapungua Nguvu zake mwilini.. labda Miaka 12-45…japo yaweza kupungua au kuzidi..

Zingatia:

Ikiwa wewe ni kijana, hakikisha maonyo hayo unayatendea kazi mapema…

Lakini ikiwa wewe ni mzazi na una mtoto, fahamu kuwa siku moja atakuwa kijana,hivyo kabla adui hajamtumia, anza kumjengea misingi mizuri ya kutembea katika Imani ya wokovu, naye hataicha njia hiyo mpaka atakapokuwa mtu mzima

Mithali 22:6

[6]Mlee mtoto katika njia impasayo,

Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIJANA NA MAHUSIANO.

Je Bwana YESU alikuwa na amri ya kumwingiza mtu katika ufalme wa MUNGU au hakuwa nayo?

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

Print this post

SAFARI YA KUUONA USO WA MUNGU.

Musa (Mgongo)

Kristo (kioo)

Mbinguni (Dhahiri)


Ilikuwa ni shauku ya Musa kutaka Kuuona uso wa Mungu baada ya muda mrefu kukaa bila kumwona Mungu..

Lakini tukirudi kwenye maandiko yanasema, Mungu alizungumza na Musa uso kwa uso kama mtu anavyozungumza na rafiki yake.

Kutoka 33:11 Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.

Lakini iweje tena, aombe kuuona uso wa Mungu, na Mungu kumwambia huwezi kuuona uso wangu ukaishi?

Kutoka 33:20 Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.

21 Bwana akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba;

22 kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa

mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita;

23 nami nitaondoa mkono wangu, nawe utaniona nyuma yangu, bali uso wangu hautaonekana

Ukweli ni kwamba kuuona uso wa Mungu, sio kuona mwonekano Fulani, au umbo Fulani la Mungu. Hapana, bali ni kumjua yeye ndani ni nani.. Tangu zamani Mungu alikuwa akijifunua kwa wanadamu kupitia maumbile mbalimbali, ambayo yanaweza kuchukua taswira ya vitu, wanadamu au malaika(huitwa Theofania),. Hivyo kwa namna yoyote ile Mungu anapomtokea mtu kwa namna mojawapo ya hizo na kuisikia sauti yake kama vile mwanadamu mwenzako anavyozungumza na wewe, ni  sawa na kusema Mungu amesema nawe uso kwa uso. Lakini haimaanishi kuwa umeouna uso wake. Kuuona uso wake ni kumjua yeye ni nani.

Sasa Mungu akamwambia, Musa, huwezi kuniona ukaishi, Kwanini amwambie vile, Je! Mungu ni kifo? Hapana, Mungu ni uzima, lakini Musa alikuwa bado hajakamilika kwasababu ya dhambi, hivyo utukufu wa Mungu asingeweza kuustahimili, kwasababu wakati wa kuustahimili ulikuwa bado, kwani ulihitaji kwanza ondoleo la dhambi kabisa.

Hivyo Mungu akamwonyesha sehemu yake ya nyuma (Mgongo). Lakini Uso hakuuona.. Ndipo akamjua Mungu kwa sehemu yeye ni nani..

Alipomwona alishangaa sana, kwa zile tabia na sifa, Mungu alizokuwa nazo, jinsi zilivyo tofauti na mawazo ya wanadamu.. Pengine alijua ataona mafunuo makubwa ya nguvu na uweza, na mamlaka, ya ukuu, na utukufu usioelezeka kibinadamu, lakini alipomwona Mungu alimwona ni mwenye huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema, mwenye hukumu za haki.

Kutoka 34:5-7

5 Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana.

6 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si

mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;

7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba

zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.

Hata sasa, mtu anayemtambua Mungu kwa namna hii,  basi ameuona mgongo wa Mungu.. Na pale mtu anapoiga tabia hizo basi, amemkaribia Mungu sana.

Lakini safari ya kuuona Uso wa Mungu, ilikuwa bado haijakamilika..

Uso (Katika kioo)

Hivyo wakati ulipofika, Mungu akamtuma mwanawe duniani, (Yesu Kristo), kutuonyesha sasa uso wa Mungu ulivyo..Maandiko yanasema hivyo;

Yohana 1:18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.

Umeona kumbe, hakukuwahi kutokea mtu duniani aliyeuona uso wa Mungu, na moja ya kazi kubwa aliyokuja kuifanya Yesu duniani ni kumfunua Mungu(uso wake) ni nani?

Na kwasababu hakuna mtu mwenye dhambi anayeweza kumwona Mungu akaishi, ilimbidi yeye mwenyewe awe fidia ya dhambi zetu, kwa kufa kwake pale msalabani, ili sisi tuhesabiwe kuwa hatuna dhambi (kwa neema), na ndipo sasa tustahimili kuuona utukufu wa Uso wa Mungu.

Na alipotukamilisha kwa namna hiyo, basi, akatuwezesha pia kumkaribia Mungu tumwone.

Yesu akatufunulia uso wa Mungu, kuwa yeye ni UPENDO. Na upendo wake si ule wa kibinadamu, , kwamba nakupenda kwasababu umenipenda, au umenitendea jambo zuri.. Hapana, bali ni ule usio na sharti wa kuonyesha fadhili hata kwa wanautuchukia..

Musa, aliishia kujua huruma tu za Mungu  juu juu (kibinadamu), lakini hakujua kuwa hata jino kwa jino, ilikuwa ni makosa, kumwonea mwenzako hasira, au hata kumfolea ilikuwa ni makosa, yanayostahili hukumu,  talaka Mungu hapendezwi nazo.. Musa hakujua kuwa Mungu anataka tumwone yeye kama BABA, ambaye ni ‘ABA’ yaani Baba mwenye mahusiano ya karibu na mwanawe, kama ilivyokuwa kwa Yesu na Mungu,yeye alidhani Mungu ni wa kutoa tu amri, sheria na hukumu, Musa hakujua kuwa mwenye dhambi (mfano wa mzinzi, mwanamke mchawi) hapaswi kutupiwa mawe, bali kuhubiriwa injili ili atubu.. Yote hayo Yesu alikuja kutufunulia, kiufasaha kabisa wala hakutuficha chochote..

Kwa jinsi nyingine ni kuwa sisi tumemwona Mungu kupitia Kristo, na kwa kupitia uhalisia wa maisha yake. Tukiyaishi maneno ya Kristo, basi tumemjua Mungu uso wake, kiufasaha kabisa..

Lakini Safari bado inaendelea… Uso wa Mungu katika kilele chake, bado hatujaufikia…

Utauliza kwa namna gani?

Uso dhahiri (mbinguni)

Ni kwamba kwasasa tunaouona kwa njia ya KIOO, bado hatujauona kiuhalisia kabisa kwa macho, japo tunaweza kusema kuona kwenye kioo hakuna tofauti na kuona kabisa kwa macho, lakini ladha huwa zinatofautiana, kumwona Raisi kwenye Tv, ni Yule Yule utakayemwona kwa macho, lakini ladha ni tofauti..

Hivyo Kristo alikuwa kama chapa (kioo) ya Mungu yenyewe, duniani..Yaani sisi tayari tumemwona Mungu kupitia Kristo Yesu..

Waebrania 1:3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;

Ndio maana maandiko bado yanasema, kwasasa tunaona kwa kioo, lakini wakati ule tumjua sana yeye alivyo..

1Wakorintho 13:12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.

Wakati wa kuona dhahiri, wema wote wa Mungu, itakuwa ni mbinguni.

Tutamjua katika eneo gani?

Katika eneo lilelile la upendo, (sawasawa na ile 1Wakorintho 13 ilivyokuwa inaeleza habari hiyo tangu juu)

Hapo ndipo tutaufurahia upendo wa Mungu katika namna ambayo hatujawahi kuijua, kwa vile vitu tulivyoandaliwa na yeye mbinguni, milele…

Hivyo, hatuna budi sasa kutembea katika upendo wa Mungu kwasababu yeye ndio huo..

1Yohana 4:16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

Hitimisho:

Hatua za kuuona  Uso wa Mungu, zilianza, na Musa, (kwa mgongo), zikaja kwa Kristo (kwa kioo), na mwisho mbinguni, (dhahiri).

Je! Umempokea Kristo? Ikiwa bado, fahamu kuwa  huwezi kamwe kumwona Mungu, hata iweje, mpokee leo, akuoshe dhambi zako, kwasababu kumbuka pia alimwambia Musa, hatamwesabia mtu mwovu kuwa hana hatia, yaani kila mmoja atapewa anachostahili. Ukifa katika dhambi zako, hakuna upendo huko kuzimu,hutatolewa huko na kuletwa mbinguni.. kwasababu umechagua mwenyewe giza. Yesu alisema Jehanamu ya moto ipo, na mtu asipomwamini yeye, atakufa katika dhambi zake. Hivyo ndugu, Ingia ndani ya Yesu leo upokee neema, hujui ni lini utaondoka duniani, usiishi tu kama mnyama, tubu dhambi mkimbilie Yesu, akuponye.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

UFAHAMU UFUNGUO WA KUMPENDA BWANA ZAIDI

Print this post

Je tunajazwaje maarifa ya mapenzi yake? (Wakolosai 1:9)

Wakolosai 1:9

[9]Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;

JIBU:

Vifungu hivyo vinaonyesha kiu ya mtume Paulo juu ya watakatifu wa kanisa la Kolosai, Kwamba wajawe kuyajua mapenzi ya Mungu katika hekima yote na ufahamu wa rohoni.

Alijua ili kanisa liweze kumpendeza Mungu na kusimama ni lazima lijue mapenzi ya Mungu makamilifu.. Hivyo Ikawa shauku yake tangu zamani lijazwe kujua mapenzi hayo.

Mapenzi ya Mungu ni yapi?

Kuna makundi mawili (2), ya mapenzi ya Mungu.

1)Mapenzi Ya daima

2) Mapenzi Ya wakati

Mapenzi ya daima: Ni yale ambayo yapo wakati wote, na kwa wote kwamba kila mwamini lazima ayatimize..mfano wa haya ni..ni kama utakatifu (1Wathesalonike 4:3), kuhubiri Injili, kuishi kwa upendo, kukusanyika pamoja, kudumu katika maombi, kumwabudu Mungu.

Lakini mapenzi ya wakati: Ni yale ambayo Mungu anakusudia uyafanye katika kipindi fulani tu, ni mapenzi yasiyo na mfanano, au mwendelezo fulani.. Kwamfano Mungu anakutaka leo usihubiri, bali uende kumtembelea yatima mmoja kijijini. Mfano wa kama alivyoambiwa Filipo awaache makutano aende jangwani kwa ajili ya yule mtu mmoja mkushi.(matendo Matendo 8:26)

Au wakati mwingine unapitishwa katika jaribu fulani, halafu pasipo kujua kuwa hilo ni darasa la Mungu ili kutumiza kusudi fulani, unajikuta unakemea na kushindana nayo…Ndio maana Bwana Yesu alipoomba juu ya kuondolewa kikombe cha mateso, alimalizia kwa kusema Baba mapenzi yako yatimizwe.

Sasa yote haya yanahitaji hekima na maarifa kuyatambua na kuyatimiliza. Si rahisi kuyatambua kwa akili za kibinadamu au kuyatimiliza.

Lakini Swali linakuja mtu anawezaje kupata maarifa hayo ya mapenzi ya Mungu?

1) Kwa maombi.

Jambo la kwanza Paulo analitaja ni kuomba, aliwaombea watakatifu Wa Kolosai kwasababu alijua uwezekano wa kupokea Maarifa hayo upo katika maombi.

Yakobo 1:5

[5]Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.

Maombi hufungua mlango wa Mungu kuyaingilia maisha yetu na kututia katika kusudi Lake kamilifu. Mungu anafanya kazi ndani yetu kupitia maombi…Bila uombaji haiwezekani kutembea ndani ya mapenzi yote ya Mungu.

2) Neno la Mungu.

Kwa kusoma Neno ndipo unapojua Tabia za Mungu, nini anataka na nini hataki. Sauti ya Mungu, maagizo ya Mungu ya moja kwa moja yasiyohitaji usaidizi ni biblia takatifu.

Zaburi 119:105

[105]Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Mtu ajijengeaye tabia ya kusoma biblia, si rahisi kuanguka au kutoka nje ya mpango wa Mungu. Kwasababu lile neno linakaa ndani yake kama mafuta kumfundisha.

3) Mashauri Ya kikristo.

Bwana anafunua mapenzi yake tuwapo katika mabaraza yetu kutafakari maneno yake.. alisema wawili watatu kwa jina lake yupo hapo hapo katikati yao…Wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau, tunaona walikuwa zaidi ya mmoja, ndipo wakiwa katika kutafakari habari za Kristo, Aliungana nao bila hata wao kujua akaanza kuwafundisha, na mwisho wote kujua mapenzi makamilifu ya Mungu ni nini..(Luka 24)

Na ndio maana hatupaswi kulikwepa kanisa kwasababu huko tunaungana na viungo vingi katika Mwili wa Kristo, na hivyo kujengana na kuonyana. Hatimaye mapenzi ya Mungu yanafunuliwa kwetu.

Hata wakati ule kulipotokea sintofahamu ndani ya kanisa kuhusu vyakula na sheria..baraza lilikalishwa kule Yerusalemu kisha mahojiana mengi yakaendelea …lakini mwishoni Mungu alitoa maarifa kwa kusema wajiepushe.na damu na uasherati lakini sio mataifa watwikwe tena kongwa la torati lililowashinda wao.(Matendo 15 )

Hivyo ni vema kumshirikisha pia mpendwa mwenzako/ kanisa mpango wako, yapo mashauri ya ki-Mungu ndani yao yaliyojaa hekima yatakusaidia.

4) Upambanuzi wa kiroho

Huu ni uwezo wa Mungu ambao mtu humwingia kutokana na kiwango chake cha juu cha ukuaji wa kiroho (Waebrania 5:14).. Bila kutegemea kuomba au kumuuliza Mungu mtu hutambua lililo la kweli na lililo la uongo.. lililosahihi na lisilosahihi, la rohoni au la mwilini, lenye Mwongozo wa ki- Mungu au kibinadamu. Tunaweza kujua mapenzi ya Mungu kwa ujuzi huu, unaozalika kutokana na ukomavu wetu wa kiroho.

Hitimisho:

Hivyo wewe kama mwana wa Mungu, kumbuka ni sharti kutembea ndani ya mapenzi yake…madhara ya kutembea nje ya hayo ndio kama yale aliyoyasema Bwana kwenye Mathayo Mathayo 7:21..

[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baraka ni nini na kuna aina ngapi za baraka?.

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

Print this post

FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.

Ahadi mojawapo ya Roho Mtakatifu Kwa wote waliompokea ni kupewa uwezo wa kuzungumza “ufahamu wa Mungu”, kwa vinywa vyao.

Ufahamu huu unaweza kujifunua katika maumbile mbalimbali aidha kwa kueleza habari zilizopita, au habari zijazo, au zinazoendelea sasa hivi, au kutoa maelekezo, au faraja, au neno la hekima, au maarifa, au uponyaji au baraka..Namna zote hizi kwa lugha rahisi kuitwa utabiri/ unabii.

Ukiwa kama mwamini ni vema kufahamu sehemu kubwa sana ambayo Roho Mtakatifu anaitumia kuhudumu ni katika vinywa vyetu. Ndio maana siku ile ya kwanza ya pentekoste aliposhuka, alikaa juu ya wale watu kama “ndimi za moto”. Maana yake ni kuwa huduma yake hasaa hujidhihirisha katika ndimi…ndio maana akaweka moto wake juu ya ndimi zao, lugha zao zikabadilishwa wakaanza kunena kwa lugha mpya.

Kwahiyo kinywa cha mtu aliyeokoka, ni kinywa cha Mungu duniani. Usipojifunza kukifungua kinywa chako kiufasaha, ujue hiyo ni namna mojawapo ya kumzimisha Roho Mtakatifu ndani yako.

Watu wengi hawajui kuwa kila mmoja amepewa uwezo wa kutabiri/ kuhutubu na sio suala la huduma fulani ya kinabii tu, hapana utauliza hilo lipo wapi kwenye maandiko? Soma..

Matendo 2:17 wana wenu na binti zenu watatabiri..

Lakini pia 1 Wakorintho 14:31. Inasema..

[31]Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.

Kuhutubu kama ilivyotumika hapo, ni kutabiri/ kusema ufahamu wa Mungu. Jambo ambalo ni la wote sio baadhi.

Sasa unafunguaje kinywa cha Roho Mtakatifu na unafanya hivyo katika mazingira gani?

Usisubiri mpaka karama fulani ije juu yako, yaani kuonyeshwa/kufunuliwa.. hapana…kwasababu tayari una Roho Mtakatifu ndani yako anza kusema maneno yanayolanda na ahadi za Neno la Mungu, bila kufikiri- fikiri

Kwamfano…

Umepelekwa kwenye mashtaka fulani kwa ajili ya Neno. Au unatakiwa uwasilishe hoja, au ufundishe Neno, au uhubiri, au umekwenda mtaaani kushuhudia.. usianze kusema mimi nitawezaje kuhubiri, au kujieleza, sijui sheria, sijui vizuri biblia, sijui kupangilia maneno…hupaswi kufikiri hivyo. bali ukumbuke ulishapewa kinywa cha moto, tangu siku ulipoamini, wewe nenda kisha anza kuzungumza huko huko katikati ya maneno yako Roho Mtakatifu ataunganika na wewe.

Mathayo 10:18-20

[18]nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

[19]Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

[20]Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.

Mwingine atakuambia mimi siwezi kuomba masafa marefu ninaishiwa na maneno…ndugu hupaswi kukatisha maneno na kuacha Kuomba, ukaenda kulala.. endelea kutafakari huku ukizunguza na Mungu wako Habari mbalimbali za kwenye maandiko, na ghafla tu baada ya muda kidogo utaona unaingia kwenye mkondo fulani wa kimaombi, linatoka neno hili kwenye ufahamu linakuja neno hili la kuombea…ulikuwa umepanga uombe Saa 1, unajikuta unaomba matatu.hapo ni Roho Mtakatifu amekupa Kinywa cha kuomba..na ndani ya maombi hayo ni utabiri tosha, kwasababu sio ufahamu wako, bali ni wa Mungu ndani yako.

Vilevile jifunze kutoa sauti katika uombaji wako wa mara kwa mara..ndio tunafahamu Maombi sio sauti, hata kimoyo- moyo Mungu anasikia, lakini usimzimishe Roho..

Watu wengi wanatamani kunena kwa lugha lakini, wanazuia vinywa vyao kutoa sauti.. wanategemea vipi wanene kwa lugha mpya..unapojiachia Kwenye maombi huku unatoa sauti ni rahisi sana kujazwa Roho Na kuomba kwa lugha.

Eneo lingine labda mtu ni mgonjwa..anahitaji maombi…Fungua kinywa chako kwa ujasiri mtamkie uponyaji…unaweza kudhani ni maneno yako, hujui kumbe Ni Roho Mtakatifu Ameyaingilia na kulifanya tayari kuwa Neno la kinabii la uponyaji, na hatimaye anapokea uponyaji wake saa hiyo hiyo.

Uwapo na Watoto wako, Acha kuzungumza nao, habari za kidunia dunia tu..wawekee mikono wabariki kwa Imani kama vile Isaka alivyowabariki Yakobo na Esau na maneno yale yakawa kweli. Vivyo hivyo na wewe tabiri juu ya watoto wako unataka wawe nani wawapo watu wazima.

Uwapo kazini na marafiki zako, penda kuzungumza maneno ya ki-Mungu wakati mwingi kwasababu huko huko unabii unaweza kupita bila wewe kujijua… mwangalie kayafa

Yohana 11:49-52

[49]Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

[50]wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima.

[51]Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo.

[52]Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili wawe wamoja.

Hivyo kinywa cha ni kinywa cha Roho Mtakatifu usikifunge Bali kijaze Maneno ya Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Print this post