Category Archive Mafundisho

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

SWALI: Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, ni vita ya namna gani tunashindana nayo katika ulimwengu wa Roho?


JIBU: Katika biblia tunaposoma Neno “pepo”, ni vema tufahamu ufunuo wake upo katika namna mbili;

  1. Pepo: Kama malaika muasi
  2. Pepo: Kama pando la malaika muasi

Yote mawili unapaswa kufahamu, Ili ujue ni nani unashughulika naye katika vita hivyo vya kiroho.

Kwamfano, ukisoma ile waefeso 6:12 inayosema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka na wakuu wa giza hili pamoja na majeshi ya mapepo wabaya.. Sasa hao wanaotajwa hasaa ni malaika waasi.

Lakini hawa malaika waasi, huwa na mapando yao, ambayo huyapanda ndani ya watu, mfano wa hayo ni magonjwa, ukichaa, ububu, udhaifu (Marko 9:25)uuaji, uchungu, majivuno, kiburi, masengenyo n.k.. na haya mapando wakati mwingine huitwa mapepo, kwasababu asili yao ni kutoka kwa hao malaika waasi.

Luka 13:11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

Pepo linalozungumziwa hapo, hasaa sio yale mashetani, bali ni pando la udhaifu waliloliweka ndani ya huo mwanamke.

Hizi zote ni kazi za shetani na malaika zake duniani. Sasa mapando haya ndio tunaweza kuyaua (kwa kuyang’oa), lakini sio wale malaika waasi. Ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa

Wale malaika waasi (yaani wakuu wa giza, wafalme, majeshi ya mapepo yote)hatuwezi kuwaua, kwa maombi au kwa namna yoyote, isipokuwa tayari wameshawekewa hukumu yao, siku ile ya mwisho ambapo watatupwa wote kwenye lile ziwa la moto.

Na mapando haya, Bwana Yesu alitoa maelezo yake vema, wakati ambapo adui hupandwa ndani ya mtu..

alisema.

Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Kumbe wakati ambapo watu wamelala, ndipo hupanda mbegu zake. Yaani wakati ambapo watu wamekuwa walegevu kiroho ndipo shetani hupata nguvu ya kuja kupachika, mbegu zake za uharibifu, zitakazokuja kusumbua baadaye. Ndio maana ni lazima ujue kanuni mbalimbali za kumpinga shetani.

Na haya mapando, yanaweza kuwekwa kwa mtu yeyote, hata mtu aliyeokoka, anaweza kuwa nayo. Ndio maana utaona wapo watu wengine wameokoka, lakini wanasumbuliwa na mapepo, kiuhalisia, hawana malaika wale waasi ndani yao, wanayo mapando yao.

Ni sawa, na mtu ambaye anamilika chombo kama komputa, akiwa anaitumia kwa matumizi yake tu ya sikuzote, tu ambayo ni lazima, si rahisi computa hiyo kuvamiwa na virusi, lakini akianza kutembea mitandaoni, kisha kubofya, au kupakua kila kitu anachokiona ni wazi kuwa chombo hicho kipo hatarini kuvamiwa na virusi, na matokeo yake ni kuwa mfumo wote wa kumpyuta unaliwa, au kuharibifu chombo kabisa, ndio maana wanaweka ulinzi (anti-virus) sikuzote,

Vivyo hivyo na maisha ya mwanadamu yakiwa ovyo ovyo, hawezi kukwepa mapando ya mashetani ambayo yamezaa kila mahali. Mtu yeyote ambaye hajaokoka tayari kuna pepo fulani ndani yake.

Kwamfano, mwingine, labda mkristo  ameokoka, halafu akiwa kanisani, anaanza kuruhusu masengenyo kinyume na mchungaji wake, au mama-mchungaji, sasa mtu kama huyo akiwa anaendelea na tabia hiyo..matokeo yake ni kwamba pepo la uchungu litamvaa, ataanza kuwachukia viongozi wake hata bila sababu, na kuzusha vita, na uharibifu hata  wengine. Yeye atadhani ni tabia yake kumbe sio, bali pepo limeshamvaa la uchungu.

Nikupe huu ushuhuda, Kulikuwa na mama mmoja kanisa, kipindi chote ulikuwa ukikutana naye, anamzungumzia vibaya mama mchungaji wa kanisa alilokuwa mwanzo, hapo mwanzo alikuwa vizuri tu kiroho, lakini kwa jinsi siku zilivyozidi kwenda, akiendeleza chuki zake, , hali yake ilikuja kubadilika ghafla, akaomba tumwombee, tulipomwombea alilipuka mapepo, lile pepo likawa linasema “mama mchungaji” yaani asili yangu ni chuki kwa mama mchungaji, tulipolikemea likamwacha akarudia hali yake ya kawaida, akawa mtu mzuri tu.

Samsoni, alipokwenda kuwashindana na wafilisti, hakushughulika  kwanza na wafilisti, bali mashamba yao ya ngano. (mapando yao). Kwa kuyachoma moto. Vivyo hivyo na sisi ili tuyamalize nguvu haya mashetani, tuangushe ngome zao. Ni lazima fikra zetu hasaa zielekee mapando yao.

NAMNA YA KUSHINDANA VITA VYA KIROHO:

Injili:

Kwamfano kuwaangusha wakuu wa giza sio kuwatumia makombora ya moto hapo angani. Hapana, bali ni kwenda kuhubiri injili ili watu wamsikie Kristo waokoke,

Ndio maana Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri waliporudi Yesu aliwaambia ‘nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme’.

Kumbe anguko lake lilikuwa katika kuhubiri na si kumtumia makombora.

Maombi:

Hii ni silaha kubwa, ya kumpinga shetani. Maombi huruhusu, utendaji kazi wa Mungu ndani ya maisha ya mwamini, usipokuwa mwombaji tarajia shetani kuyapangalia maisha yao. Yesu alituagiza tukeshe kuomba tusije ingia majaribuni.

Upendo:

Upendo hupinga, wivu, chuki, uchungu, mashindano, uzinzi, n.k. ambayo haya yote huzaliwa mahali ambapo hapana upendo. Ni lazima kila siku wewe kama mwamini kila siku ujifunze kutendea kazi upendo….ili uondoe mazingira ya mashetani kuangua mayao yao hapo.

Neno:

Ukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yako, adui hawezi kukushinda. Utakumbuka kule jangwani, shetani alipojaribu kumpandia Kristo maneno ya uongo kwa kupitia biblia, yeye mwenyewe alilitumia Neno la Kweli, kumpinga. Watu wengi wanavamiwa na maroho ya upotevu, kwasababu hawana Neno la Mungu mioyoni mwao. Jifunze kusoma biblia. Ni silaha inayoitwa Upanga.

Imani:

Imani huzaa ujasiri, na ujasiri hutoa mamlaka ndani yako. Biblia huiita imani “Ngao” Shetani anapenda kutumia silaha ya woga, ili kuzimisha utendaji kazi wa Mungu mioyoni mwetu. Hatuna budi kusimama kwa utimilifu wa imani kumtumikia Mungu.

Kukemea:

Fahamu adui ni mpingamizi sikuzote, hapembelezwi, bali analazimishwa kutoka, Yesu alimkemea shetani alipotaka kumjaribu kwa kinywa cha Petro, aliyakemewa mapepo yote sugu, yaliyokuwa ndani ya watu yawatoke. Hivyo na wewe pia ukutanapo na kazi hizi za mwovu, jifunze kutumia kinywa chako, kwa mamlaka uliyopewa na Kristo kukemea haraka sana, kila pepo, au kimelea chochote cha uovu kinachozaliwa na adui.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, mashetani hawafi, lakini kazi zao zinakufa.. Hatuwaui hao, bali tunaziua kazi zao. Usipoteze muda mwingi kumrushia shetani mabovu hawezi kufa, bali tuma nguvu zako nyingi kurushia mabovu mapanda yake, kwa kanuni hizo tulizojifunza. Utawashinda kabisa kabisa.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Print this post

LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.

Chemchemi kazi yake ni kutoa “maji ya kunywa” lakini pia ya maji ya “kustawisha mimea”.

Kama chemchemi ikitoa maji ya chumvi au ya magadi, ni wazi kuwa maji yake hayatafaa kwa matumizi yoyote yale, hivyo mahali hapo hapana uhai, watu hawawezi kuishi wala wanyama wala mimea..

Lakini kama chemchemi ikitoa maji safi yasiyo na magadi wala chumvi, na tena masafi, basi mahali pale kila kitu kitasitawi ikiwemo watu, wanyama na mimea, na hata shughuli zote nyingine za kiuchumi.

Mfano wa maji machungu na yasiyofaa ni yale wana wa Israeli waliyokutana nayo kule ‘Mara’

Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.

23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.

24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?

25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko”.

Sasa Biblia inafananisha “Mioyo yetu na chemchemi zinazotoa maji”… Maana yake yanayotoka mioyoni mwetu yanaweza kukuza, kustawisha au kudhoofisha afya zetu, wanyama wetu, mimea yetu…kwaufupi kila kitu kinachotuzunguka ikiwemo kazi zetu, elimu zetu, nafasi zetu, kibali chetu na mambo mengine yote yanategemea sana yanayotoka mioyoni mwetu.

Sasa najua utauliza haya maji machungu au matamu ni nini?.. Turejee maneno ya Bwana Yesu.

Mathayo 12:34 “Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.

35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya”.

Tusome tena Mathayo 15:18-20…

Mathayo 15:18 “Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19 kwa maana MOYONI hutoka MAWAZO MABAYA, UUAJI, UZINZI, UASHERATI; WIVI, USHUHUDA WA UONGO, NA MATUKANO

20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi…….”.

Umeona hapo?.. kumbe moyoni ndiko kunakotoka matukano, uzinzi, wizi, uongo n.k mambo ambayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi, na bila shaka hayo ndiyo Maji machungu yatokayo moyoni kupita kinywani, ambayo hayafai kwa kustawisha chochote…

Wengi wamepoteza na kuharibu maisha yao kwasababu ya uzinzi, na wengine kwasababu ya wizi, na wengine kwasababu ya mauaji, wapo waliopoteza kibali kwa Mungu na kwa watu kwasababu ya wizi, au uzinzi, au mauaji..wapo walipoteza kazi zao za mikono na huduma zao zilizokuwa zenye utukufu kwasababu ya uzinzi, au wizi au matukano..

Wapo walioharibu ndoa zao zilizokuwa za heshima na mfano kwasababu ya uzinzi, uongo, na mauaji (utoaji mimba) Kwanini?.. kwasababu chemchemi zao zinatoa maji machungu yanayoua ndoa, kazi, huduma, kibali, heshima na nguvu.

Yakobo 3:8 “Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.

10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.

11 Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?

12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu”.

Lakini kama moyoni kukutoka mambo masafi, ambayo ni upendo, ukweli, utu wema, uvumilivu (kwa ujumla utakatifu)… hakika hiyo ni chemchemi bora inayostawisha kila kitu, maji yake yatastawisha wokovu, kazi ya Mungu, kazi ya mikono, elimu, heshima, ndoa, nafasi na mambo mengine yote mazuri.

Je wewe chemchemi ya moyo wako inatoa maji ya aina gani?.. machungu au matamu?.. Kama inatoa machungu ipo dawa leo?.. dawa hiyo ni Roho Mtakatifu… Mwamini YESU leo kisha ukabatizwe na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukutakasa moyo wako Bureeeee kabisa!

Baada ya hapo ndoa  yako iliyokufa itafufua upya, huduma yako, kazi yako, elimu yako au kitu kingine cha thamani ulichopewa na Bwana, kitafufuka kwani tayari maji yatokayo ndani yako ni masafi..

Lakini labda tayari chemchemi yako ni safi, nayo inatoa maji masafi.. bado kuna jambo lingine la ziada la kufanya nalo ni KUILINDA chemchemi yako..

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.

Utaulinda moyo wako kwa MAOMBI, kusoma NENO, kujihadhari na ulimwengu na kushiriki ibada pamoja na watu wenye imani moja na wewe kila mara.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu?

Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;

MOYO ULIOELEKEA KWA MUNGU.

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

JIHADHARI NA MANENO YASIYO NA  MAANA 

Print this post

Je! Ni sahihi kwa mkristo kufundishwa na AI mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.

SWALI: Je! Ni sahihi kwa mkristo kujifunza, au kufundishwa na AI (Artificial Inteligence), mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.


JIBU: Ili kujibu swali hili ni vema, kutambua mashine hizi za akili bandia (AI), zinafanya kazi gani.

Kwa ufupi ni kuwa AI, inafanya kazi ya kuchakata taarifa nyingi, kutoka katika vyanzo vingi vilivyopo mitandaoni, mfano vitabu, makala, sauti, machapisho n.k, na hivyo inazichanganya taarifa hizo zote kwa kuangalia muktadha unaofanana na kuzifupisha, na kukujibu.

Hivyo kimsingi, ni chombo ambacho kinatoa msaada mkubwa katika ulimwengu wa sasa, na ndio ukweli usiopingika..Kwasababu kinarahisisha utafutaji wa taarifa. Lakini pamoja na hayo haimaanishi kuwa kinatoa kwa ufasaha wote.

Sasa tukija kwenye eneo la kiroho. Je ni vema mkristo kwenda kuuliza AI, au kuandaa maombi au masomo kupitia hiyo, n.k.

Ukweli ni kwamba Imani, sio taarifa, ni zaidi ya taarifa.. Hizi AI, zinatoa tu taarifa lakini hazitoi mafunuo. Hazina pumzi ya Roho Mtakatifu ndani yake.

Ikiwa unataka kuongeza maarifa kwa sehemu fulani zinaweza kukusaidia, lakini sio kukujenga nafsi, kwani inahitaji pumzi ya Mungu na miongozo ya Mungu wewe kujengwa nafsi, na sio taarifa.

Kwamfano ikiwa wewe ni mchungaji halafu, kila inapokaribia jumapili unachowaza ni kwenda chatgpt, kuiambia ikuandalie somo la kufundisha jumapili,  ndugu hapo hesabu kuwa umepotea kama sio kukengeuka… Tumia hiyo kwenye biashara zako, masomo yako,  projekti zao lakini sio kwenye mambo ya kiroho. Hilo liepuke kabisa.

Kufundisha Neno inahitaji ‘Neno’ mwenyewe (Yesu) akae ndani yako, kwasababu ni UHAI sio taarifa (Waebrania 4:12) ndio hapo itakupasa kupiga magoti kwanza uombe, kwa muda mrefu, utafakari moyoni mwako, ukae kwenye utulivu wa kutosha, ndipo Mungu alipande somo lake moyoni mwako. Ambalo yeye mwenyewe anajua litakuwenda kuwagusa vipi watu wake, wenye changamoto mbalimbali, kwamfano, pengine mtu mmoja alikuwa anakaribia kwenda kujinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha na mateso fulani, na Mungu kamwona anataka amsaidie, kwa kuliweka somo linalohusiana na mapito ya Ayubu ili ainuliwe imani. Kinyume chake kwasababu ya uvivu wako wewe unakwenda kuiambia chatgpt (akili bandia), ikuandalie somo. Halafu jumapili utakwenda na taarifa zao sio mafunuo. Badala uokoe roho inayokwenda kujinyonga, unaiambia, “leo tunajifunza kanuni kumi za kudumisha ndoa na mahusiano kibiblia”. Hapo unafanya nini sasa?

Au Neno fulani Bwana anataka kukupa la wakati wako, sasa ikiwa unakimbilia AI ikusaidie, hutaki kuchukua muda wako binafsi kutafakari na kuomba ‘jiandae kukutana na ukame wa kiroho.

Visaidizi hivi, hatupaswi kuvifanya ndio sehemu ya imani yetu, kwamba kila kitu tutegemee kule, hivi ni tone dogo sana kati ya bahari kubwa. Roho Mtakatifu alishatuandalia njia zake, kuu za kujengwa na yeye.

Wekeza zaidi, kuomba msaada kwa wakufunzi wako, viongozi wako, ndugu zako katika Kristo, wekeza katika maombi, mifungo, tafakari, na kujisomea mwenyewe Neno.  kwa njia hizi hakika Bwana atasema nawe na kujengwa zaidi kuliko visaidizi. Lakini pia ikiwa pana umuhimu wa kujiongezea taarifa kwa vile unavyovijua, visaidizi hivi vitakufaa (Katika uangalizi maalumu), vinginevyo utajidumaza kiroho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>  https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Karismatiki ni nini?

Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.

Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.

Print this post

Akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake

Akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.

Waebrania 11:21

[21]Kwa imani Yakobo, alipokuwa katika kufa, akambariki kila mmoja wa wana wa Yusufu, akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.

Ulishawahi kujiuliza ni kitu gani Yakobo alikuwa anawaonyesha wana wake siku ile alipokuwa anakaribia kufa.. kitendo cha yeye kusujudu kwa kuegemea kichwa cha fimbo?

Kwanini biblia iseme akaegemea fimbo na sio ukuta, au kitanda au au kiti au isikae tu kimya, bila kueleza chochote?

Yakobo alikuwa na maana kubwa kufanya vile, kwasababu hata alipokuwa akiwabariki watoto wa Yusufu (Efraimu na Manase) alipishanisha mikono..wakidhani kuwa amekosea, akawaambia sijakosea naelewa ninachokifanya, leo ndio tunajua kumbe alikuwa anaunda msalaba, ambao kwa kupitia huo neema inawafikia mataifa kwanza.

Vivyo hivyo na alipokuwa anakufa alisujudu kwa kuegemea kichwa cha fimbo, na huwenda watoto wake walistaajabishwa na kusujudu kule, pengine walijaribu kumwondoa pale ili asujudu vema, lakini akawaambia niacheni naelewa…

Fimbo kibiblia inafunua mamlaka ya mfalme, mchungaji na safari.

Yakobo hakuishi bila tegemeo la mchungaji…udhihirisho Ulikuwa ndio ile fimbo..kwasababu sikuzote alijiona kama kondoo wa Mungu, hakutaka kuiacha fimbo ya mchungaji wake, popote alipokuwepo kwasababu ndio faraja yake.

Daudi alisema…Bwana ndiye mchungaji wangu…gongo lake, na fimbo yake vyanifariji..

Zaburi 23:1-4

[1]BWANA ndiye mchungaji wangu,  Sitapungukiwa na kitu.

[2]Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,  Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

[3]Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza  Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

[4]Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya;  Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. 

Kwa ufupi ni kuwa palipo na fimbo ya mchungaji hapo hapo utaona Na kondoo wamejilaza. Yakobo alitembea na Kristo, Mpaka dakika ya mwisho wa maisha yake.

Lakini pia Fimbo inamfunua msafiri…zamani wasafiri walikuwa wanasafiri na fimbo kuwasaidia kutembea..

Wana wa Israeli walipokuwa wanajiandaa na safari ya kutoka Misri, utakumbuka usiku ule walipewa maagizo kila mmoja kushika fimbo yake.

Kutoka 12:11

[11]Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya BWANA.

Kristo pia alipokuwa anawatuma wanafunzi wake katika ziara za injili aliwaagiza Kubeba fimbo zao..

Marko 6:8

[8]akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;

Hii ni kutufunulia kuwa Yakobo alikataa kuishi kama mwenyeji duniani.. bali msafiri..

Hivyo alitamani urithi wake ujue jumla ya mwenendo wa maisha yake hapa duniani ulikuwaje..

Hiyo ndio sababu kwanini historia za maisha ya watu kama hawa Mungu kazihifadhi tuzisome hadi leo.

Hata sasa, ujiulize je na Mimi je! fimbo ya mchungaji wangu(YESU KRISTO), ipo pamoja nami? ujiulize je mimi ni msafiri hapa duniani?

Fahamu tu Wazao wote wa Mungu huwakosi na fimbo ya Mungu, hiyo ndio alama yetu.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Print this post

Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)

Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote”

1 Petro 5:10

[10]Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.

Tafsiri ya Neema ni kukubaliwa kusikostahili.. au upendeleo usio na sababu. Kwamfano pale mtu anapomwajiri mtu asiye na ujuzi kisha akampa nafasi au mshahara mkubwa wa kiwango cha sawasawa na yule mwenye elimu nyingi na uzoefu..hiyo tunaiita neema.

Hivyo katika ukristo msingi mkuu wa wokovu wetu unategemea neema ambayo ililetwa na Bwana wetu Yesu Kristo(Yohana 1:17).

Yaani Tunakubaliwa na Mungu kuwa sisi tumestahili kuingia katika ufalme wa Mungu na kuwa watoto wake, kwa kumwamini tu Yesu Kristo bila kutegemea matendo yetu wenyewe kama kigezo cha sisi kufikia kiwango hicho.

Neema hiyo hujulikana kama neema ya wokovu. Ambayo ndio neema kuu, iliyomfanya Kristo aje duniani kufa kwa ajili yetu kama fidia ya dhambi ili sisi tuitwe waliostahili. (Waefeso 2:8-9)

Lakini pamoja na hayo Mungu hana mipaka kwamba anatoa neema ya aina moja tu yaani ya wokovu peke yake…hapana anazo Neema nyingi, ambazo zinaingia katika nyanja mbalimbali za maisha ya mwanadamu.

Sehemu nyingine katika biblia huitwa. Neema juu ya neema..

Yohana 1:16

[16]Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.

 

Zifuatazo ndio mfano wa neema Mbalimbali ambazo Mungu anatoa.

1) Neema ya kutumika na kibali.

Neema hii unamwezesha mtu, kuwa na matokeo katika Huduma na ustahimilivu wote. Ndiyo ambayo Paulo na Barnaba walipewa, iliyowafanya waweze kukichukua kijiti cha injili na kufanikiwa kukipeleka kwa mataifa.

Matendo ya Mitume 13:2

[2]Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.

Mbeleni utaona maandiko yanasema..

Matendo ya Mitume 14:26

[26]Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza.

Hivyo wewe kama mtakatifu ukitaka mafanikio katika huduma au karama yako. Kujifunza kuomba neema ya Mungu katika huduma ni liwe ni sehemu ya maisha yako. Kwasababu hiyo Ipo kukusaidia…Na utapata matokeo ambayo hayategemei zaidi nguvu zako. Ndicho walichokuwa wanakiomba sana mitume.

Matendo ya Mitume 15:40

[40]Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana. Neema ya kupokea vitu.

2 Wakorintho 9:8

[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Kumbukumbu la Torati 8:18

[18]Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Hata kupata vitu kiwepesi, hasaa hutegemea neema ya Mungu, kama mkristo ni lazima ujifunze kumwomba Mungu neema ya kufanikishwa, katika mambo yako yote ya kimaisha, isizitegemee tu nguvu zako au akili zako, hata kama jambo ni jepesi vipi, ikiwa ni kazi Omba Mungu akupe neema ya mafanikio, ikiwa ni biashara omba Akupe neema ya kupata Faida Zaidi, ikiwa ni elimu omba Mungu akuongezee akili zaidi.

2) Neema ya kuendelea Mbele (nguvu mpya).

Zaburi 68:9

[9]Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.

Ni sifa ya Mungu kauchilia neema yake kwa watu wake pale wanapochoka huwatia nguvu mpya, wao wenyewe wanashangaa wanainuka tena na kuendelea mbele.. Ndio maana tunasema Mtu anayedumu katika wokovu maisha yake yote, hata anapopitia katika tufani, Pepo na mawimbi, bado hatetereki.. Ni neema ya Kristo inakuwa imehusika hapo kumvusha, si nguvu Zake.

Jifunze kuiomba hii namna ya neema.

3) Neema ya madhirihisho ya karama za Roho.

Matendo ya Mitume 6:8

[8]Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.

Karama za Roho, mfano miujiza, uponyaji, lugha, unabii, utume, uchungaji, n.k, ni vipawa ambavyo hutolewa bure na Roho Mtakatifu, Hakuna jitihada Yoyote ambayo mtu atafanya aweze kukunua nguvu za kumfufua mfu, au kuona mambo ya mbeleni Ayatolee unabii, au kuundoa Ukimwi kwenye damu Ya mtu, isipokuwa kwa neema za Mungu, kutembea na yeye.

Ni neema ambayo tunapaswa tuiombe, ambayo inamfanya Mungu aachilie mafuta mengi ndani yako ya kutembea katika vipawa hivyo, ili kulijenga kanisa.

1 Petro 4:10

[10]kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.

4) Neema ya Kutembea katika utakatifu.

2 Wakorintho 1:12

[12]Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.

Inategemea nguvu ya Mungu (neema), kutembea katika hali ya kutimiza mapenzi yote ya Mungu katika utakatifu… maana yake ni kuwa mwanadamu Akijifunza kumpa Nafasi Roho Mtakatifu ndani yake. Atajaliwa kuishi Maisha yote yampendezayo Mungu, sawasawa na Wagalatia 5:16

5) Neema ya kutoa.

2 Wakorintho 8:1-3

[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;

[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.

[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;

Hii ni uwezo wa kutoa vitu/ maisha/ chochote kwa wengine bila kujali nafsi yako mwenyewe.

Jifunze kumwomba Mungu neema ya utoaji. inafaida kubwa sana kwa wengine, kwa binafsi lakini pia katika kukua kwa ufalme wa Mungu.

2 Wakorintho 8:9

[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

6) Neema ya ulimwengu ujao.

1 Petro 1:13

[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.

Yapo mambo Mengi mema tusiyoyajua, ambayo tutapewa tukifika kule ng’ambo Kristo atakaporudi.. ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, biblia imehitimisha kwa kuyaita “neema”

Je Umepokea neema zote? Lakini zaidi ya yote neema ya wokovu?. Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo Yesu akusamehe dhambi zako, basi tawasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili upate msaada huo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

 

Print this post

Chakula kigumu mfano wake ni upi kama tunavyosoma katika Waebrania 5:12?

SWALI: Biblia inasema maziwa ni kwa watoto wachanga, lakini chakula kigumu ni cha watu wazima. Mfano wa chakula hichi kigumu ni kipi?

Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya

JIBU:

Kabla ya kufahamu hicho chakula kigumu, ni vema kujua kwanza maziwa ni yapi.

Hivyo ukiendelea kusoma  vifungu vinavyofuata anasema..

Waebrania 6:1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.

Sasa hayo mafundisho ya kwanza ya Kristo ndio maziwa. Yaani Mafundisho ya toba, imani kwa Mungu, ubatizo, kuwekewa mikono, kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele ni mafundisho ya watoto wachanga..kiroho hujulikana kama maziwa..

Kimsingi mtoto akiendelea kunywa maziwa tu peke yake daima, kitakachotokea baadaye ni kudumaa kama sio kufa kabisa, hivyo itafika wakati tu atahitaji chakula kingine ili aendelee kuishi. Vivyo hivyo na sisi, vipo vyakula ambavyo tunapaswa tule, kwa jinsi tunavyoendelea kukua kiroho.

Vifuavyo ndio vyakula vigumu vya kiroho vya watu wazima:

1) Upendo kwa maadui

Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu jambo hilo linaenda kinyume na asili ya mwanadamu, linafunua asili ya ndani kabisa ya Kristo, ambayo si rahisi mtu aliyemchanga kiroho, kuielewa, au kulipokea nyakati za mwanzoni, yaani kumwombea  na kumpenda Yule ambaye anaiwinda roho yake au aliyemjeruhi, ..

2) Makusudi ya Mungu katika mateso

Wafilipi  1:29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;

Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu mwamini mchanga, mara nyingi atapenda kuambiwa maneno ya faraja, baraka, na mafanikio, awapo kwa Kristo,  lakini mkristo aliyekomaa, anayaona mapenzi ya Mungu pia hata katika majaribu na kuyashangalia.

1Wathesalonike 3:3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo

Soma pia 1Petro 1:6-8, 4:13, Wakolosai 1:24, Luka 6:22-23

3) Upambanuzi wa kiroho

Waebrania 5:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya

Mkristo aliyekomaa kiroho, anafundishwa na Mungu kutambua na kugawanya vema mambo yote, kujua vilivyo najisi na visivyo najisi, mafundisho ya kweli na yale ya uongo, anafundishwa, busara, ujuzi na hekima hata katika kuhubiri injili kwa makundi yote, bila kuanguka na kunajisika, kwasababu amepewa roho ya upambanuzi ambayo huja kwa kuzoeshwa na Mungu kwa kipindi Fulani cha muda kupitia  Neno lake.

1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.

21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.

Soma pia, 1Wakorintho 8:6-13, Yohana 2:1-12, Mathayo 11:19.

Kwanini ni chakula kigumu? Kwasababu mtu ambaye ni mchanga kiroho, akijihusisha katika viwango hivyo, hupotea na kunajisika kama sio kupotea kabisa. Ndicho kilichowatokea Adamu na Hawa kuuvamia mtu wa ujuzi wa mema na mabaya nje ya ratiba ya Mungu, matokeo yake wakayavuna mabaya, wala sio mema.

4) Kuikubali Fimbo ya Mungu.

Katika wokovu ipo fimbo ya Mungu; Mzazi yoyote huwa hatoi zawadi tu, sikuzote, hacheki na mwanawe siku zote, lakini pia kuna wakati fimbo hutumika, Vivyo hivyo Mungu ni Baba yetu, huadhibu, pale tunapokosea..

Waebrania 12:11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.

Kwanini ni kigumu? Kukubali marekebisho kwa kuadhibiwa kama sehemu ya kutengenezwa na Mungu, si jambo rahisi mtu kulikubali mkristo ambaye hajakomaa. Yeye atakachojua tu, kuwa Mungu ni upendo.

5) Kujikana na kuubeba msalaba.

Luka 9:23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

Kwanini ni chakula kigumu? Aliye mchanga kiroho kukubali kukataa mapenzi , kuingia gharama kuacha vyote na kuyakubali ya Mungu tu, si jambo rahisi kwa mwanafunzi wa ngazi ya chini.

6) Unyenyekevu na kujitoa kwa wengine.

Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.

5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba

Kwanini ni chakula kigumu?.

Mkristo mchanga kiroho, si rahisi kuangalia mambo ya wengine, mfano wa Kristo, si rahisi kujinyenyekeza na kukubali kutembea kama mtumwa ili kuwatumikia wengine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

USIGEUZE JIWE KUWA MKATE.

Je unaujua uhusiano wa JIWE na MKATE kibiblia?.. Hebu leo tujifunze…

Mathayo 7:8 “ kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, MWANAWE AKIMWOMBA MKATE, ATAMPA JIWE?”

Ni hakika, hakuna mzazi yoyote mwenye akili timamu, ambaye mtoto wake akimwomba MKATE atampa JIWE. Hayupo mzazi wa namna hiyo, wala wanyama hawawezi kufanya mambo ya mfano huo wa watoto wao.

Lakini tunaona wakati fulani shetani alijaribu kumchonganisha Bwana YESU na Baba yake wa mbinguni kwa kumwambia, AGEUZE JIWE LIWE MKATE, kana kwamba Baba wa mbinguni alikuwa amemwekea yale mawe kule jangwani kuwa chakula chake (uvunjifu mkubwa wa heshima)!

Luka 4:2 “akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.

3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, LIAMBIE JIWE HILI LIWE MKATE”.

Hili lilikuwa ni jaribu kubwa la shetani kwa Bwana YESU kutaka kumwingizia roho ya kumwona Baba wa mbinguni kama ni mkatili, ambaye anampa mwanae mawe badala ya mkate kupindi cha njaa, na hivyo adui sasa anamfundisha ayageuze yale mawe kuwa mkate.

Na adui alijua kuwa endapo KRISTO angefanya vile (kwaasababu huo uwezo wa kugeuza jiwe kuwa mkate alikuwa nao) angempokonya uhusiano wake mwema aliokuwa nao na Baba yake, na tangu ule wakati angejua Baba anatoa mawe kwa watoto wake badala ya mkate.

Lakini Kristo kwasababu alikuwa amejaa Roho Mtakatifu aliyajua mafumbo yote ya shetani, hivyo hakudanganyika,  na ndio maana hapo baadae katika Mathayo 7:9 akawaambia wanafunzi wake kuwa Baba mwema hawezi kumpa mtoto wake JIWE badala ya MKATE, sasa kwanini alisema vile?..kwasababu alishakutana na jaribu la namna hiyo hiyo jangwani.

Hali kadhalika unapopitia hali Fulani ya majaribu, usianze kutanga tanga na kuruhusu hofu, na kuona kama kila kitu kilichoko mbele yako hata kisicho na uhai ni fursa kutoka kwa MUNGU, sio kila kitu ni fursa kwako wakati wa majaribu!…vingi ni mitego ya ibilisi kwasababu anajua upo katika hali ya uhitaji wa hali ya juuu….hiyo ndiyo kawaida ya shetani.. alitaka pia kumwaminisha Bwana YESU kuwa yale mawe ni fursa ya kuondoa njaa yake.

Si kila kazi inayokuja mbele yako wakati wa vipindi vigumu ni fursa kutoka kwa MUNGU, kazi nyingine ni za Ibilisi (ni mawe). Mungu hawezi kukupa hayo kama riziki, ziache zipite!.. kazi za Bar ni mawe!, kazi ya Saloni za kiduni ni mawe!, kazi inayohusisha rushwa ni jiwe!, kazi inayohusisha kuuza utu wako ni jiwe!, kazi inayohusisha kuabudu miungu mingine ni jiwe!.. usizigeuze MAWE hayo kuwa MKATE!, hata kama una njaa ya kukaribia kufa!..ziache zipite, si majibu kutoka kwa MUNGU, bali ni majaribu kutoka kwa shetani, kwani huwezi kumwomba Baba wa mbinguni MKATE akakupa JIWE.

Huwezi kumwomba akupe kazi nzuri halafu akakuletea kazi ya kujiuza mwili wako!.. huyo sio MUNGU, bali ni ibilisi…Njaa yako, udhaifu wako, changamoto zako ambazo ni za muda tu!, zisikufanye ukaharibu mahusiano yako na MUNGU moja kwa moja.

Je tayari umeshampokea YESU?.. Kama bado fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho, na YESU amekaribia kurudi, na dunia inaenda kuisha, ni heri leo ukayasalimisha maisha yako kwake, ili usamehewe dhambi zako na jina lako liandikwe kwenye kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Je ni kweli Bwana YESU hajui siku ya kuja kwake? (Mathayo 24:36)

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

Print this post

Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’

SWALI: Nini maana ya Mithali 3:27 ?

[27]Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.


JIBU: Kuna mambo mawili yaliyogusiwa katika hicho kifungu..

  1. Usiwanyime watu mema yaliyo Haki yao.
  2. Lakini pia, ‘ikiwa katika uwezo wa mkono wako’.

1] Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao.

Hili ni agizo la Bwana kuwasaidia wengine. Lakini pia Bwana anataka tujue ni akina nani wenye haki hiyo ya kusaidiwa.

Kibiblia Makundi ambayo ni haki yao kusaidiwa.(wawapo na shida), ni matatu (3)

 i) Familia (yaani ndugu wa mwilini)

1 Timotheo 5:8

[8]Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Wazazi wako, wadogo zako, watoto wako. Ni haki yao kuwasaidia, kwasababu ni damu moja na wewe. Usipotimiza wajibu huo unahesabika sawa na mtu aliyeikana imani. Hakikisha jicho lako haliwapiti ndugu zako, ni sehemu ya wajibu.

ii) Ndugu wa rohoni:

Wagalatia 6:10

[10]Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

Kanisa la kwanza lilitambua jukumu hili la kusaidiana, vivyo hivyo na sisi ikiwa mpendwa mwenzako yupo katika hali na uhitaji mkubwa hupaswi kufumba macho, bali msaidie, watumishi wa Mungu wanaojibidiisha kuhubiri kweli ya Mungu wanastahili kusaidiwa mahitaji yao. (Warumi Romans 12:13, Hebrews 13:16).

1Yohana 3:17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.

Hapa inalenga pia na wajane pia walio ndani ya kanisa wale walio wajane kwelikweli. (1Timotheo 5:3–5, 9–10)

iii) Maskini.

Wapo maskini wengi ulimwenguni, ambao wanashindwa kufikiwa na mahitaji yao ya msingi, wengine wanakuwa mabarabarani walemavu, wagonjwa, majirani maskini, wote hawa pia wanastahili kusaidiwa.

Wagalatia 2:10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya.

Hayo ndio makundi yenye haki ya kusaidiwa. Lakini wengine wanaweza kusaidiwa lakini sio haki yao,ikiwa na maana hata wasiposaidiwa hakuna shitaka lolote juu yako kwa Mungu.

2]  Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda:

Lakini Ukiendelea kusoma anagusia tena jambo la pili ambalo ni; “Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda”.

Akiwa na maana gani?

Mtume Paulo kwa uweza wa  Roho aliandika maneno haya;

2 Wakorintho 8:12-13

[12]Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.  [13]Maana sisemi hayo, ili wengine wapate raha nanyi mpate dhiki;

Yaani kwa jinsi moyo wako unavyoguswa, tenda mema,  lakini pia kulingana na uwezo wako uliokirimiwa na Mungu,  ili upande mmoja usiuache na taabu au kupungukiwa kabisa. Kwamfano umepata rizki kipimo cha watoto wako tu, ukaenda kukichukua na kuwapa maskini huku familia yako ikabaki Kulala njaa.. hapo hujafanya busara kwasababu umehamisha Tatizo sehemu moja kupeleka kwingine, hujatatua tatizo.

Tenda mema, bila kusahau pia kipimo chako ulichopimiwa cha mema.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Masomo mengine:

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe?

Print this post

SADAKA INAONDOA MADHARA YA MAUTI

Sadaka inayotolewa kwa mwongozo wa Neno la MUNGU ina matokeo makubwa sana kwa anayeitoa. Yapo madhara yanayoondoka kwa maombi tu peke yake, lakini yapo mengine yanahitaji sadaka pamoja na maombi.

Hebu turejee Biblia kidogo tujifunze jambo..

Wakati ambapo Nabii Samweli anataka kwenda kumpaka mafuta Daudi ili awe mfalme mahali pa Sauli..biblia inatuambia kuwa alipofikiri kwenda tu hofu ilimwingia..

Na hofu hiyo ni kwamba alimwogopa Mfalme Sauli, kwani alijua kabisa endapo Sauli akisikia mtu mwingine anaenda kupakwa mafuta ya kifalme kuchukua sehemu yake, wivu utamwingia na atataka kumwua nabii Samweli na yule atakayeenda kupakwa mafuta.

Sasa ili zoezi la Daudi kupakwa mafuta likamilike bila kuleta madhara yoyote kwa Nabii Samweli na Daudi anayeenda kupakwa mafuta ya kifalme, SADAKA ILIHUSIKA!.

Utauliza ilihusika vipi?…turejee maandiko…

1 Samweli 16:1 “BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.

2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi BWANA akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea BWANA dhabihu.

3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako”

Je umeiona nafasi ya sadaka katika kuyaokoa maisha ya Samweli na Daudi?.

Hapo MUNGU hakushindwa kumwambia nabii Samweli aende hivyo hivyo na kwamba atamlinda!…La! Hakufanya bali alimwambia aende na dhabihu..

Jambo hilo Bwana MUNGU wetu aliliruhusu pia ili tuelewe umuhimu dhabihu/sadaka.

Unapomtoleo MUNGU kwa ufunuo wa Neno, bila kushurutishwa na mtu wala uchungu, kuna mambo mengi katika ulimwengu wa roho yanafanyika, kama ni nira za mauti zinalegea na kama kuna vifungo vya dhambi pia vinaondoka.

Na kumbuka sadaka kwa BWANA inapelekwa kwa BWANA, maana yake mahali ambapo BWANA anatumikiwa (mfano kanisani au mahali panapofanyika kazi ya MUNGU ikiwemo mikitano ya injili)..hapo ndipo penye neema.

Usipeleke sadaka yako maalumu mahali pengine kama kwa marafiki, au watu au maskini wa barabarani…ni vizuri kufanya hivyo na kuna baraka zake lakini vya Bwana vinapaswa vipelekwe kwa Bwana ndivyo maandiko yanavyofundisha..

Tenga kiasi chako kungine peleka kwa maskini na wenye uhitaji, lakini hakikisha una sadaka yako maalumu kwa BWANA utakayopeleka aidha kanisani au mahali popote kazi ya MUNGU inapofanyika kwa usahihi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Kibiblia, hekima, ni uwezo wa  kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.

Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)

Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,

Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.

Lakini inapatikanaje?

Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.

Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.

Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.

Yesu anapatikana wapi?

Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.

Anapazaje sauti?

Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.

Hivyo, hilo andiko linalosema,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.

Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post