1 Samweli 15: 20 “Sauli akamwambia Samweli, Hakika mimi nimeitii sauti ya Bwana, nami nimemleta Agagi, mfalme wa Waamaleki, tena nimewaangamiza Waamaleki kabisa.
21 Ila watu waliteka nyara, kondoo na ng’ombe walio wazuri, katika vitu vilivyowekwa wakfu, KUSUDI WAVITOE DHABIHU KWA BWANA, MUNGU WAKO, huko Gilgali.
22 Naye Samweli akasema, JE! BWANA HUZIPENDA SADAKA ZA KUTEKETEZWA NA DHABIHU SAWASAWA NA KUITII SAUTI YA BWANA? Angalia, KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU, NA KUSIKIA KULIKO MAFUTA YA BEBERU.
23 Kwani KUASI NI KAMA DHAMBI YA UCHAWI, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.