ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU

ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU

Tukijua kuwa Mungu ni zaidi ya sisi tunavyofikiri, Na kwamba hukumu zake hazichunguzi (kama inavyosema Warumi 11:33), Siku hiyo tukifahamu mambo hayo kwa undani tutaishi maisha ya kumwogopa na ya kujichunga kila siku, Siku tukijua kuwa mambo yote mtu atendayo aidha yawe maovu au mema hayaji kwa nguvu zake mwenyewe bali ni kutoka kwa Mungu, ndipo tutakapomwopoga sana Mungu na kujua kuwa yeye si mwanadamu na kwamba mawazo yake si mawazo yetu.

Biblia inasema:

Mhubiri 7:13 “Tafakari vema kazi yake Mungu; kwa sababu ni nani awezaye kukinyosha kitu kile alichokipotosha yeye?”.

Watu wengi hawapendi kusikia maneno hayo kwamba Mungu anao uwezo wa kumletea mtu nguvu ya upotevu ili apotee,. Ni kweli Mungu hawezi kumletea mtu nguvu ya upotevu kwa yeye ambaye hajaijua neema bado lakini kwake yeye aliyeisikia na kuipuuzia na kuikataa, nguvu hiyo ya upotevu inaachiliwa juu yake, na nguvu hiyo haitoki kwa shetani bali inatoka kwa Mungu mwenyewe.

Soma >>

1Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11 KWA HIYO MUNGU AWALETEA NGUVU YA UPOTEVU, WAUAMINI UONGO;

12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.”

Kama tu vile mtu anayempokea Kristo kwa mara ya kwanza Mungu huwa anamshushia uwezo /nguvu ya kushinda dhambi na kufanyika kuwa mtoto wa Mungu (Yohana 1:12), kadhalika na wale ambao wanaikataa neema ya msalaba au wanaoipuuzia sasa, utafika wakati hii nguvu ya upotevu itokayo kwa Mungu inaachiliwa wao nao juu yao. Hivyo watu wa namna hiyo inafika wakati hata wahubiriweje injili, hata wauone ukweli kiasi gani, hawawezi tena kuamini. Hali yao ya rohoni inazidi kuwa mbaya kuliko hata waliyokuwa nayo mwanzoni, kule kuchomwa rohoni pale mtu anapotenda jambo baya kunakufa, dhamira yake inakuwa imekufa, mtu kama huyo dhambi inakuwa ni kitu cha kawaida sana kwake, hata akibaka mnyama, hata akiua, hata akifanya ushoga, hata akikufuru mbele za Mungu kwake ni kama jambo la kawaida tu,.

Ni kwasababu gani?, Ni kwasababu ile nguvu ya upotevu itokayo kwa Mungu imeachiliwa juu yake ili auamini uongo siku ile akahukumiwe ili ashuke moja kwa moja katika ziwa la moto, kwasababu hakuipenda kweli apate kuokolewa bali alijifurahisha katika udhalimu.. Na Watu wa namna hiyo kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndio mwisho wa siku wanaishia kuipinga biblia, wanaishia kusema hakuna Mungu, biblia ni kitabu kilichotungwa na watu, wanakuwa wanaishi tu kama wanyama duniani wasioweza kujizuia. Watu wa namna hiyo wanawaona hata wale wengine wanaotafuta wokovu kama ni watu wasioelimika, watu waliokata tamaa ya maisha, watu wajinga wasio na mwelekeo.

Biblia imetumia lugha hii kuwazungumzia jinsi walivyo watu wa namna hiyo..

Yuda 1:11-16 “ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;

13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.

14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,

15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake.

16 Watu hawa ni wenye kunung’unika, wenye kulalamika, waendao kwa tamaa zao, na vinywa vyao vyanena maneno makuu mno ya kiburi, wakipendelea watu wenye cheo kwa ajili ya faida.”

Sasa watu wa dizaini hii hata uwahubirieje injili hawawezi kubadilika wala hawatakaa wabadilike kwasababu ni Mungu wenyewe ndiye aliyewakusudia mabaya, na ndio maana biblia inasema:

Mhubiri 7:13 “Tafakari vema kazi yake Mungu; kwa sababu ni nani awezaye kukinyosha kitu kile alichokipotosha yeye?”.

Ndugu, Njia za Mungu huwa ZINATISHA, na ndio maana tumeambiwa TUZITAFAKARI VEMA KAZI ZAKE, sio tu kuzichukulia juu juu, Tukidhani kuwa hukumu za Mungu zinachunguzika kwamba nitaokoka tu siku moja! Au Tunasema Mungu ataokoa tu!, Mungu tu ataokoa tu! Na huku tunadumu katika dhambi tukidhani kuwa neema ni kitu cha kukifanyia mzaha. Kumbuka hilo neno lenyewe NEEMA ni kitu kinachoonyesha kuwa ni jambo AMBALO HUKUSTAHILI KULIPATA NI KWA HURUMA TU UMEPEWA, lakini unaendelea kulifanyia mzaha kana kwamba ulistahili kuipata ni haki yako?.

Unadhani NGUVU HIYO YA UPOTEVU itakapokujia juu yako ikiwa hautubu leo, na kusimama imara katika Kristo siku ile ya hukumu utasema Mungu ni MDHALIMU alikuletea mabaya kwa makusudi?. Ndugu Itafakari vema kazi ya Mungu ili ujue leo hii unasimamia wapi?.

Mungu alishamaliza mambo yote kabla hata ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, majina ya watakaookolewa Mungu alishayaandika katika kitabu cha uzima kabla ya misingi ya ulimwengu kuwekwa biblia inasema hivyo

Ufunuo 17.8 “Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. NA HAO WAKAAO JUU YA NCHI, WASIOANDIKWA MAJINA YAO KATIKA KITABU CHA UZIMA TANGU KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako”.

Embu tafakari kwa makini habari hii utajifunza jambo.

Warumi 9:11 “(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye),

12 aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo.

13 Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.

14 Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!

15 Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.

16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.

17 Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.

18 Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.

19 Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake?

20 La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?

21 Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?

22 Ni nini basi, ikiwa Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi, alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa uharibifu;

23 tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu;”

Je! Wewe ni chombo cha ghadhabu kilichowekwa tayari kwa uharibifu, au ni kile chombo cha rehema?. Jua tu ikiwa unaukwepa msalaba, ikiwa unaukwepa wokovu, ikiwa unaikwepa toba, ile nguvu ya upotevu mfano wa ile iliyokuwa juu farao ambayo HATA AONE MIUJIZA MIKUBWA KIASI GANI HAWEZI KUTUBU, NDIYO ITAKAYOKUJA JUU YAKO KAMA UTAENDELEA KUUPINGA WOKOVU NDANI YA MOYO WAKO.

TAFAKARI VEMA KAZI YAKE MUNGU. Ili ujiokoe nafsi yako, Epuka Injili ya maneno ya faraja kila siku unaambiwa kwamba Mungu ni Mungu wa rehema. Lakini upande wa pili wa Mungu hagusiwi ambao unasema BWANA NI MWINGI WA HASIRA, ni nani awezaye kusimama mbele ya hasira yake, ni nani awezaye kukaa katika ukali wa hasira yake? (Nahumu 1 )

Kwa kulijua hilo, utafahamu kuwa Mungu hadhihakiwi na hapo ulipo hupaswi kuendelea kudumu katika dhambi. Na ndio maana biblia inasema “(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”

Kwa nini usiwe mmojawapo wa kondoo wa Kristo?. Ikiwa upo tayari sasa kuwa mmojawapo unachopaswa kufanya ni kukusudia wewe mwenyewe kutoka moyoni mwako Kutubu na kuacha dhambi kabisa..Kumbuka kutubu ni KUGEUKA( au KUACHA) na sio sala ya toba tu.

Hivyo ukiwa umedhamiria kufanya hivyo wewe moyoni mwako kwa dhati kabisa na kutaka kumwishia Kristo kuanzia sasa na kuendelea. Unachopaswa kufanya ni kwenda kutafuta mahali ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kimaandiko, yaani ubatizo wa kuzamishwa, katika maji mengi na jina linalotumika liwe ni JINA LA YESU KRISTO na si linginelo. Ili upate ondoleo la dhambi zako, Kulingana na matendo 2:38,na Bwana mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu kuanzia huo wakati na kuendelea kukusaidia kuukulia wokovu na kuishinda dhambi.

Mungu akubariki sana.

“Share” Ujumbe huu kwa ndugu zako, Na Mungu atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UNAFANYA NINI HAPO?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

WAKATI WA JIONI KUTAKUWAKO NA NURU.

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments