Unaona sasa uwezo wa namna hiyo, wa kuweza kuendana nayo na kushinda mambo yote hayo pasipo kumwacha Mungu, sio kwa jitihada za mtu binafsi kupambana na hizo hali, hilo haliwezekani kwa mtu yeyote Yule, hiyo ni YESU KRISTO mwenyewe ndio anafanya ndani ya mtu ili kuhakikisha kwamba hakupotezi wewe kipenzi chake, haungamii, hivyo tatizo linapokuja, kabla ya kukufikia wewe, linawasili kwanza kwake, kisha analipatia utatuzi, ndipo litakaposhuka kwako, na litakaposhuka linakuja na dawa madhubuti ya kulishinda, Uwezo wa kipekee unatoka kwa Mungu, na nguvu ya kushinda majaribu na mitikisiko yote..