Unaona? Hili ni agizo la pili la Bwana kwa kanisa, kwamba kazi ya kufundisha, mfano uchungaji, ualimu, uaskofu na ushemasi, haupaswi ufanywe na mwanamke. Na Mungu alishatoa sababu ya kufanya hivyo hapo juu, Hivyo ikiwa mwanamke ataona kama hapewi haki yake na kutaka kwenda kuwa mchungaji au mwalimu ni sawasawa na ameingia katika mbio ambazo sio za jinsia yake, Hivyo matokeo yake mtu kama huyo, ataonyesha kweli nguvu nyingi na jitihada nyingi, lakini hatapokea tuzo yoyote katika siku ile,..Siku ile atasema Bwana mimi nilikuwa mchungaji wa kimataifa kanisani, nilifanya hivi nilifanya vile, lakini Bwana siku ile atamwambia hukupiga mbio mahali panapokupasa. Unaona hapo angepaswa akawe mchungaji, au mwalimu kwa wanawake wenzake, akawe muhubiri kwa wanawake wenzake, lakini sio kanisani penye mchanganyiko wa wanaume na wanawake.