Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?

Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?

SWALI: Tumeambiwa sisi (Watakatifu) tutahukumu, Je! baada ya kuhukumu tutaweza kuwaamurisha malaika wawachukue wale tuliowahukumu na kuwatupa kwenye ziwa la moto?


JIBU: Ubarikiwe kwa swali zuri, lakini kuna jambo la kujifunza zaidi hapo, siku ile tutakapoketi na Bwana kuhukumu, sisi ndio tutafanana na yeye lakini hukumu ya mwisho atatoa yeye peke yake YESU KRISTO. Sisi tutakuwa kama mawakili. Kwa mfano siku ile atasimamishwa mtu aliyekuwa anafanya uasherati, na huku anasema ameokoka, na Bwana atamwuliza kwanini ulikuwa unafanya vile, labda atasema kwasababu kizazi chetu kilikuwa na simu zenye internet hivyo ilikuwa ni ngumu kujizuia, sasa utaitwa wewe Michael ambaye saa hiyo utakuwa pembezoni mwa Bwana, na Bwana atakuuliza ilikuwaje wewe uliushinda uasherati katika kizazi cha internet, utatoa sababu pale, sasa zile sababu zako utakazozitoa wewe mtakatifu ndizo zitakazo muhukumu yule mkosaji Unakumbuka yale maneno Bwana Yesu aliyoyasema katika..

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.

42 Malkia wa kusini atasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, naye atawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu yeye alikuja kutoka pande za mwisho za dunia ili asikie hekima ya Sulemani, na hapa yupo aliye mkuu kuliko Sulemani”.

Kwa namna hiyo ya malkia wa sheba atakavyokihukumu kizazi kile, ndivyo na sisi tutakavyokihukumu kizazi hichi.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

JE NI KWELI TUTAWAHUKUMU MALAIKA? SAWASAWA NA 1WAKORINTHO 6:2

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

JE! BAADA YA ULIMWENGU HUU KUISHA MALAIKA WATAKUWA NA KAZI GANI TENA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments