SWALI: Matendo ya mitume 2:1 ″Hata ilipotimia “SIKU YA PENTEKOSTE” walikuwako wote mahali pamoja.Ndugu zangu hiyo Siku ya Pentekoste ilikuwa ni siku gani? Pentekoste ilimaanisha nini ndugu.?
JIBU: Pentekoste ni neno la kigiriki lenye maana “YA HAMSINI” . Hivyo kwa wayahudi walikuwa wanasherekea siku ya hamsini baada ya sikukuu ya pasaka (waliagizwa na Bwana wafanye hivyo) lakini wenyewe walikuwa hawaiiti kwa jina hilo la pentekoste, walikuwa wanaiita hiyo sikukuu kama “SIKU KUU YA MAJUMA”.
Bwana Mungu aliwaambia wahesabu majuma 7 yaani sabato 7 baada ya pasaka, yaani siku 49, na siku ya hamsini ( ndiyo pentekoste) wafanye sikukuu…Soma (Kumbu. 16:9 na Walawi 23:15).
Kwahiyo sasa kwasababu mambo yaliyokuwa yanafanyika agano la kale
yalikuwa ni kivuli cha agano jipya, ilikuwa ni lazima sikukuu hizo ziwe
na uhusiano mkubwa na mambo ya agano jipya,. Kwahiyo wayahudi pasipo
kujua lolote walishangaa Roho Mtakatifu anashuka juu yao siku ile ile ya
Pentekoste ambayo walikuwa wanasheherekea hiyo siku kuu yao ya Majuma,
kama tu kusulibiwa kwa Bwana kulivyoangukia katika siku kuu yao ya
pasaka kadhalika kumwagwa kwa Roho kuliangukia katika siku kuu yao ya
majuma (yaani pentekoste). Na ilikuwa ni siku ya HAMSINI baada ya
sikukuu ya Pasaka.
Ubarikiwe sana.
Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312
Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP
Mada Nyinginezo:
SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?
HATA ILIPOTIMIA SIKU YA PENTEKOSTE.
NINI MAANA YA KIPAIMARA?.NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?
SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!
ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU
MAFUNUO YA ROHO.
Rudi Nyumbani:
Print this post