Wakatoliki wanaabudu sanamu?

Wakatoliki wanaabudu sanamu?

Kulingana na Biblia, Wakatoliki ni kweli wanaabudu sanamu…

Biblia inasema, katika

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao”,

Sasa tatizo sio kutengeneza sanamu, wala kuning’iniza picha manyumbani mwetu za watakatifu au za wanafamilia wetu, bali tatizo ni “kuzisujudia” na “kuzitumikia”…Hivyo vitu viwili ndio tatizo.

Sasa Kanisa katoliki linafundisha watu kusujudia sanamu pamoja na kutumikia sanamu. Na kumbuka sanamu haimaanishi tu lisanamu likubwa kama lile la Nebkadneza, bali sanamu  hata ndogo tu kama punje ya harage pia ni sanamu…mbele za Mungu zote ni sawa!

Sasa Waumini wa kanisa katoliki wanafundishwa kuzipa hizi sanamu heshima fulani kana kwamba zimebeba kitu cha kiungu ndani yake..Kitendo tu cha kuzipa heshima fulani, kama kwamba ni kitu cha Kiungu hiyo tayari ni Ibada ndani ya moyo wa Mtu, na ndio kitu kinachomchukiza Mungu..

Kadhalika, kutumikia maana yake ni kukiwekea hicho kitu utaratibu fulani ambao ni kama sheria fulani inayokufanya wewe kuwa mtumwa wa hicho kitu…Kwamfano kusali rozari kila siku asubuhi, mchana na jioni na kuogopa hata kuikanyaga kwa bahati mbaya  hiyo ni kuitumikia rozari….ambapo kwako inakufanya kuwa mtumwa..Jambo hilo ni machukizo mbele za Mungu.

Sasa si wakatoliki wote wanajua hilo, na si wakatoliki wote wana nia mbaya katika kwenda kuabudu katika kanisa hilo, wengi wana nia ya kweli ya kwenda kumtafuta Mungu, isipokuwa Mfumo wa Udini umewafunga hata hawawezi kuiona kweli tena!..Lakini wale Bwana aliowachagua wakati ukifika wanapokutana na Ukweli wanafunguka macho na kurekebisha njia zao, kwa kutoka katika mifumo ya kanisa hilo na kugeukia kumwabudu Mungu katika roho na Kweli.


Mada Nyinginezo:

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
3 years ago

Samahani mtumishi,
Kwani MUNGU alivo mwambia Musa ajichongee sanamu ya nyoka wa shaba alafu wamisiri wakiangalia waishi je unaweza kunifafanulia hapo? Maana ndo MUNGU huyo huyo aliye kuwa amekataza kuchonga sanamu yoyote si mfano mbinguni au duniani