Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.

Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 25: 11 “Neno linenwalo wakati wa kufaa, Ni kama machungwa katika vyano vya fedha”.


JIBU: Vyano ni wingi wa neno “Chano”, lenye maana ya sinia. Hivyo hapo anaposema Neno linenwalo wakati wa kufaa, ni kama machungwa katika vyano vya fedha, anamaanisha kuwa ni kama machungwa katika masinia ya fedha.

Sasa kwanini afananishe Neno linalofaa na machungwa katika masinia ya fedha?. Si rahisi kuelewa kwa sisi watu ambao utamaduni wetu ni tofauti na ule wa watu wa mashariki. Kwasababu machungwa yanayozungumziwa hapo si kama ya jamii yetu hii tuliyonayo. Kule kuna aina ya machungwa, ambayo wanasema ni matamu kuliko jamii zote za machungwa duniani, juisi yake ina harufu nzuri sana, machungwa hayo huwezi kuyasafirisha nje ya nchi, kwasababu hayakai muda mrefu yanaharibika ni ya kule kule tu. Na kwa kawaida wanapoyachuma huwa wanayaweka kwenye vyombo vya masinia, na sio kwenye majaba au magunia.

Sasa machungwa haya yalikuwa ni mahususi, kwa ajili ya kupewa watu waliochoka, pale wanapokula, au wanapoinywa juisi yake, basi wanaburudika na kupunguza uchovu wao kwa sehemu kubwa sana. Ni sawa na leo hii labda mtu unapopewa soda ya baridi (Labda tuseme fanta orange) wakati jua kali na kiu. Itakuburudisha si ndio.. Na ndivyo ilivyokuwa kipindi hicho kwa watu wanaishi mashariki ya kati na baadhi ya sehemu za Asia.

Kufunua kuwa ni jinsi gani Neno zuri la kufajiri lilivyo na maana sana kwa mtu aliyekatika hali ya uchungu, au msiba, au Neno la kutia moyo lilivyo na thamani sana kwa aliyevunjika moyo, au Neno la kuhamasisha lilivyo na nguvu sana kwa walioishiwa nguvu, ni kama machungwa yaliyo kwenye masinia ya fedha, tayari kwa ajili ya waliochoka.

Na habari nzuri za kufajiri, za kujenga, za kuponya, za kuimarisha, hazitoki kwa mwingine zaidi ya Yesu Kristo pekee. Hivyo tunapowahubiria watu habari hizi njema za wokovu wa Yesu Kristo, zinaponya zaidi kuliko habari nyingine zozote tuzifahamuzo. Kwasababu yeye mwenyewe alisema alikuja kwa kazi hiyo..

Isaya 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.

2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;

3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe”.

Umeona, hivyo tuwahubiri watu habari za Kristo, hizo zinatosha kutibu makundi yote ya watu. Ukimsaidia mtu kumpata Kristo, umemsaidia kutatua matatizo yake yote. Kwasababu ndani yake sio tu atapata wokovu bali, na furaha ya kweli na amani ya kweli.  Na kwa kufanya hivyo rohoni na sisi Mungu anatuona  kama wahudumu wake wa machungwa katika vyombo vya fedha.

Bwana atupe na sisi macho ya kuyatendea hayo kazi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments