Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe.
Upo umuhimu wa kuhubiri injili mahali popote na katika mazingira yoyote kwasababu ni agizo la Bwana mwenyewe. Wapo wanaoamini kuwa injili ya mitaani na masokoni hazina faida yoyote kwasababu watu wanakuwa hawapo katika utulivu. Na pia wapo wanaoamini kuwa injili za kwenye mikutano au makanisani ndizo zilizo bora.
Lakini nataka nikuambie: Injili zote zina umuhimu. Za watu walio katika utulivu na utayari wa kusikiliza, na hata za wale ambao hawako tayari kabisa.
“Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku.”
(Matendo 17:17)
“Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu…”
(Luka 8:1)
Kikawaida ni ngumu kumsimamisha mtu barabarani na kumwambia asikilize. Lakini unapohubiri bila hata ridhaa yake, Neno linaweza kuingia ndani yake hata kama hataki. Lile Neno linaweza kuwa mbegu njema itakayochipuka kwa wakati wake.
Kwahiyo ni heri asikie moja kuliko kutokusikia kabisa. Wengine hawaendi kanisani, wengine ni wa imani tofauti, wengine wamejitosheleza – lakini kwa kuhubiri, unawafikia.
“Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana”
(Ezekieli 2:7)
Hata kama ni mara ya mia, huenda Neno moja tu likamgusa. Au wewe ndiye umeanza safari ya wokovu ndani yake ambayo itakamilika baadaye.
Wapo wanaohitaji kusikia mara nyingi. Ndio maana Bwana alituma manabii kupiga kelele:
“Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta…”
(Isaya 58:1)
Kazi ya kuhubiri si nyepesi. Lakini matokeo yake ni makubwa sana:
“Kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”
(Luka 15:10)
Pengine umesikia injili mara nyingi lakini bado hutaki kubadilika. Injili ya kurudia rudia si tangazo, ni ushuhuda dhidi yako.
“Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”
(Mathayo 24:14)
“Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu”
(Warumi 2:16)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, basi wasiliana nasi:
📞 +255789001312
📞 +255693036618
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya hapa:
👉 https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mafundisho mengine:
Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?
INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?
About the author