IMANI NI NINI?

IMANI NI NINI?

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. Pamoja na maswali mengi ya biblia yaliyojibiwa..kwa link hii >>>> https://chat.whatsapp.com/F1fZHcuNCB69aZsaGFpe3E

Imani ni nini? ..Je tunaweza kufikia imani ya kuhamisha milima?..Nini maaha ya mstari huu?..Warumi 10:17 “Basi imani chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.

Biblia imesema wazi nini maana ya Imani katika kitabu cha Waebrania..

Waebrania 11:1 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana”.

Unakuwa na uhakika kwamba jambo fulani litatokea ambalo halipo sasa..Hiyo ni Imani. Na imani sio tumaini wala ujasiri..Unaweza ukawa na matumaini ya kutokea jambo fulani lakini bado usiwe na uhakika. Imani maana yake ni kuwa na uhakika…Kwamba asilimia 100 unaamini jambo fulani litatokea…Na kwamba jambo hilo ni lazima litokee..

Na Imani mtu hujiamulii kuamini tu!..Bali lazima kiwepo kitu cha kuishikilia hiyo Imani.

Kwamfano mwanafunzi ambaye amesoma kwa bidii na ameshafanya mazoezi ya kutosha huko nyuma na kuufahamu uwezo wake hivyo ujapo mtihani wa mwisho mbele yake anaamini kwamba ni lazima afaulu!..Kwanini anaamini hivyo?..Ni kwasababu ameshajiandaa vya kutosha. Hawezi tu kusema nitafaulu mtihani huu wakati hata kushika kalamu hajawahi kuiona. (Sasa huo ni mfano tu).

Tukirudi katika Ukristo ni hivyo hivyo..Mtu ili awe na Imani..Ni sharti kiwepo kitu cha kuisupport au kuishikilia hiyo Imani yake..Vinginevyo hiyo haitakuwa Imani bali tumaini.

Kadhalika katika Ukristo Mtu ili awe na Imani labda ya kuponywa ugonjwa wake na Yesu Kristo, Ni lazima awe ameshawahi kusoma au kusikia mahali kwamba Yesu anaponya..au ameshawahi kushuhudia mtu mwingine akiponywa na Yesu..au ameshawahi kuthibitisha uponyaji wa Yesu kwa kusikia ushuhuda mahali fulani….Nguvu ya Ushuhuda ule ndio unaoelezea Nguvu ya Imani mtu aliyonayo…Haiwezekani mtu ambaye hajawahi kusikia kabisa habari za Yesu kwamba ni mponyaji akawa na Imani ya kuponywa..Hiyo haiwezekani ni lazima awe amesikia kwanza..

Ndio maana Biblia inasema..

Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.

Ndio maana ili kuikuza imani..Mtu anatakiwa alijue sana Neno la Mungu..Na Kulijua Neno la Mungu sio kukariri mistari ya Biblia…hapana bali kumwelewa Yesu Kristo kwa mapana na marefu na kuzifahamu shuhuda zake.

Unaposoma Neno na kukutana na Mstari ambao Yesu Kristo alimponya kipofu Batimayo katika Marko

Marko 10:46 “Wakafika Yeriko; hata alipokuwa akishika njia kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano mkubwa, mwana wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa ameketi kando ya njia.

47 Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu.

48 Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.

49 Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita.

50 Akatupa vazi lake, akaruka, akamwendea Yesu.

51 Yesu akamjibu, akamwambia, Wataka nikufanyie nini? Yule kipofu akamwambia, Mwalimu wangu, nataka nipate kuona.

52 Yesu akamwambia, Enenda zako, imani yako imekuponya. Mara akapata kuona; akamfuata njiani”.

Imani ni nini? Unaposoma habari hiyo na kulihifadhi tukio hilo moyoni mwako badala ya kuikariri mistari hiyo..Hapo tayari Neno la Mungu umeliweka moyoni…hata kama hujaikariri mistari hiyo…Sasa tukio hilo tayari ni Neno la Mungu na tayari ni chanzo cha Imani…Sasa unapopitia wakati wa majaribu labda umeugua kifua…Ukamwomba na ukawa hatiani kufa..Ukalikumbuka hilo tukio…na kusema moyoni kama Bwana alimponya kipofu Batimayo hata mimi nitapona tu!..Hiyo tayari ni Imani yenye chanzo sahihi cha Neno la Mungu..Hivyo italeta majibu tu! haijalishi itachukua muda gani.

Na wakati ukifika kifua hicho kikapona kulingana na Imani hiyo…Imani yako kwa Mungu itakuwa zaidi.. Hivyo hata Lijapo jaribu lingine kubwa kuliko hilo..Unatumia ushuhuda wa Bartimayo na ushuhuda wa kwako kupona kifua unazijumlisha shuhuda hizo kuangusha tatizo hilo kubwa lililokuja mbele zako hata kufikia imani ya kuhamisha milima….Lakini huwezi kuangusha tatizo lolote kubwa mbele yako au huwezi kuamini jambo kubwa kama litatoke kama huna ushuhuda wowote au Neno la Mungu kukushikilia nyuma.

Unaweza kujiuliza Daudi alitolea wapi Imani kubwa kama ile ya kumwangusha Goliathi…Hakikuwa ni kitu cha kuamka tu na kupata ujasiri! hapana..Ile Imani ilitengenezwa tangu siku nyingi…Ukisoma Biblia utaona Mungu alikuwa anamwokoa Daudi na makucha ya simba na dubu wakati anachunga…sasa mkusanyiko wa shuhuda zile ziliipandisha Imani yake na hata kufikia kusema kama Bwana ameniokoa mikononi mwa simba basi hakuna mwanadamu yoyote ambaye Bwana hawezi kuniokoa mikononi mwake. Na alipokutana na Goliathi alimwona ni mdogo kuliko simba na dubu aliokoka nao.

1Samweli 17:33 “Sauli akamwambia Daudi, Huwezi wewe kumwendea Mfilisti huyu upigane naye; maana wewe u kijana tu; na huyu ni mtu wa vita tangu ujana wake.

34 Daudi akamwambia Sauli, Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na alipokuwa akija simba, au dubu, akamkamata mwana-kondoo wa lile kundi,

35 mimi hutoka nikamfuata, nikampiga, nikampokonya kinywani mwake; na akinirukia, humshika ndevu zake, nikampiga, nikamwua.

36 Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai.

37 Daudi akasema, Bwana aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na Bwana atakuwa pamoja nawe”.

Lakini Huwezi kuwa na imani hii kabla ya kuliamini Neno la Mungu..Usipoamini kwamba Bwana Yesu ni kweli alimponya Bartimayo huwezi kuwa na Imani ya kuponywa…Usipoamini kwamba ni kweli Yesu Kristo alikuja duniani miaka 2000 iliyopita na alikuja kufa kwaajili ya dhambi zetu, na alifufuka huwezi kuwa na Imani ya kitu chochote.

Hivyo inatangulia kwanza imani ya kumwamini Yesu Kristo na maneno yake..Ukimwamini huyo ndipo Imani kwa vitu vingine itafuata na utaona mambo makubwa na ya ajabu katika maisha yako ambayo yanaonekana kama hayawezekaniki..lakini yatawezekanika kwa kumwamini Yesu Kristo.

Hivyo kama hujamwamini Yesu Kristo ni wakati wako leo… Tambua kwamba yupo, na hapo ulipo anakutazama na anakutamani uwe wake na anakuita hivyo usishupaze shingo yako..Mkubali kwa kutubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kutozifanya tena…kama ulikuwa mwasherati unaacha uasherati wako kuanzia sasahivi..kama ulikuwa ni mshabiki wa mambo ya ulimwengu huu kama miziki leo hii unaiacha yote na kama ipo kwenye simu yako ya mkononi..ifute sasahivi yote usiache hata mmoja..kama ulikuwa ni mlevi acha leo, na kama unazo pombe kwenye friji yako kazimwage sasahivi..na mkubali huyu Yesu aingie moyoni mwako.

Na ukishamwamini kwa vitendo namna hiyo..tafuta mahali ambapo unaweza kujifunze Neno la Mungu kwa ufasaha zaidi..Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako atakuongoza katika kweli yote..Pia hakikisha unabatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38. Na kwa kufuata hatua hizo utakuwa umeokoka kwa kuzaliwa mara ya pili.. Hivyo usitende dhambi tena, na Roho Mtakatifu atakupa uwezo wa ajabu wa kushinda dhambi…Na hapo utakavyozidi kudumu katika kuyasoma maneno ya Yesu Kristo Imani yako itakuwa mpaka kufikia Imani ya kuhamisha milima.

Hivyo kwa hitimisho Imani ni nini?..Ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo..na chanzo chake ni kuyaamiini maneno ya Yesu Kristo. Na maneno ya Yesu Kristo ni Yesu mwenyewe (Yohana 1:1). Ukimpokea Yesu umeyaamini maneno yake, hivyo tayari una Imani.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali share na wengine.

+255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments