Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Kuna mambo unaweza ukayafanya ukadhani ni sawa machoni pako. Lakini kumbe hujui kama unaleta huzuni kubwa kwa Kristo.
Mtume Paulo ambaye hapo mwanzo aliitwa Sauli, alikuwa akishindana na mawazo, na jamii ya watu waliomwabudu Mungu akidhani anashindana na ubaya kumbe anashindana na Kristo mwenyewe.
mpaka alipokutana na Kristo mwenyewe njiani alipokuwa anakwenda Dameski..akaambiwa maneno haya..Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Matendo 9:4-5
[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? [5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
[5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
Hilo Neno waniudhi, kwenye tafsiri ya asili linamaanisha hasaa “wanitesa”? Biblia ya kiingereza inaeleza vizuri zaidi inatumia neno “persecutest”…yaani kutesa..
Paulo alikuwa mfano wa wapagani waliomtesa Kristo, pale alipokuwa anawaburuta watakatifu, anawafunga, anawapinga, na kuwatukana…hakujua kuwa anamtesa Kristo mwenyewe..Leo hii makundi ya watu wanaowapinga watakatifu, wanaoyapinga makanisa ya kweli, wanaowatukana watumishi wa Mungu, wanaowapiga na kuwaua wafahamu kuwa wanamtesa Kristo.
Ikiwa wewe ni mmojawapo kuwa makini, uache mara moja, ni heri utubu leo umpe Yesu maisha yako. Akuokoe.
Lakini kundi la pili ni wale waamini- waliorudi nyuma. Mtu ambaye ameshaokoka, Halafu anaiacha Njia kwa makusudi anayafanya yale machafu aliyoyaacha nyuma huyo anamtesa Kristo, tena yale mateso ya msalabani kabisa.
Waebrania 6:4-8
[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, [5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, [6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri. [7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; [8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
[5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
[6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
[7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;
[8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
Acha tabia ya kuzoelea dhambi, ukishaokoka ukitenda dhambi, haihesabiki kama kosa kama la wapagani bali uasi.
Kama Ulimpokea Kristo ili umtese, kuokoka kwako kuna maana gani? Ulishawahi ona mtoto anampiga Baba yake? Hiyo si laana?
Ndivyo ilivyo kwako unapozini na huku umeokoka, unapokunywa pombe na kufanya anasa.. Tubu haraka sana umrudie Kristo
Penda utakatifu, Ishi maisha matakatifu..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
Kwanini Yeremia ailaani siku yake ya kuzaliwa? (Yeremia 20:14)
Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;
Print this post
Asante sana kwa mafundisho niungeni kwa Groupe watshap
Atukuzwe Bwana, tutafute kwa namba hizi tukuunge kwenye group la masomo la whatsapp +255789001312
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ