Sasa wayahudi ambao leo hii utawaona wanalia usiku na mchana pale kwenye ule Ukuta wa maombolezo (wailing wall). wakimwomba Mungu wa Ibrahimu baba yao aje kuwaokoa na maadui zao na kuleta utawala wa masihi duniani, ipo siku hayo maombolezo yatakoma, na ndipo Mungu atawarudia kwa kuwafumbua macho na kumwona YESU, Kumbuka Mungu aliwapofusha kwa makusudi kabisa wasimwamini Kristo ili sisi mataifa tuipate neema vinginevyo huyu Yesu wa thamani ambaye leo hii tunaifurahia neema yake, tungemsikilizia tu kwa wayahudi, sisi tungeendelea kuwa waabudu miti,vinyago, na wachawi. Na hata hivyo dunia ungekuta imeshakwisha siku nyingi, wakati ule ule tu Yesu aliokuwa ndio ungepaswa uwe ni wakati wa wao kurejeshewa ufalme wa dunia na Yesu.