USIVAE HERENI

USIVAE HERENI

Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa PETE MASIKIONI MWAKE, na kwa vito asema Bwana”.

Kabla ya kuvaa kitu, au kuiga mtindo fulani, hebu tenga muda kwanza kufuatilia asili ya kitu hiko kibiblia, kwasababu kuna vitu vingine asili yake ni mbaya, na isiyo na baraka kwa Mungu.

Hebu jiulize swali hili.. Mungu akuumbe na masikio yaliyo kamili, halafu akwambie au akuruhusu ukayatoboe masikio hayo, eti ili tu upendeze?..hivi jambo hilo ni kweli Mungu kaliagiza au kaliruhusu??.. au ni ujanja tu wa akili za watu! (walionyanyuliwa na ibilisi, Waefeso 4:14).

Sasa sikuhukumu wewe uliyetobolewa masikio, huenda si wewe kwa hiari ulifanya hivyo, bali walikutoboa tu ukiwa mchanga..na pia waliokutoboa huenda nao pia walipokea tu kwa waliotangulia, hivyo huenda kosa si lako wala la wazazi, bali la yule wa kwanza kuanzisha makosa hayo..

Lakini sasa baada ya kuelewa, si sawa kuendeleza hayo makosa kwa vizazi vyako, vile vile si sawa kuweka chuma au dhahabu katika matundu ya masikio yaliyotobolewa, kwani kwa kufanya hivyo bado utakuwa unaendeleza desturi hiyo.

Hebu tusome tena…

Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa pete masikioni mwake, na kwa vito asema Bwana”.

Asili ya kujipamba kwa pete za masikioni (yaani kuweka hereni) ilikuwa NI KUJIWEKA TAYARI KWA KUVUKIZA UVUMBA KWA MABAALI… na baali si mwingine zaidi ya shetani mwenyewe/kusifa katika kinyago chake kingine.

Kwahiyo zamani mtu akijipamba kwa kutoboa masikio na kuweka hereni alikuwa aidha ametoka kuvukiza uvumba kwa baali au ndio anaenda kuvukiza uvumba kwa baali, na hereni zamani hazikuwa zinavaliwa tu na wanawake, bali hata na wanaume, na lengo lilikuwa ni hilo hilo kumvukizia uvumba baali.

Labda utauliza ni wapi tena pengine panapoonyesha hereni, zinahusishwa na ibada za miungu..

Mwanzo 35:2 “Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, ONDOENI MIUNGU MIGENI ILIYOKO KWENU, mjisafishe mkabadili nguo zenu. .

4 NAO WAKAMPA YAKOBO MIUNGU MIGENI YOTE ILIYOKUWA MIKONONI MWAO, NA PETE ZILIZOKUWA MASIKIONI MWAO, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu”.

Sasa shetani ni yule yule, na ibada zake ni zile zile, hazijabadilika……kama bado yupo kwenye makafara ya mang’ombe mpaka leo, na mambuzi, na bado waganga wake ni wale wale, na mavazi yao ni yale yale, na uchawi wake ni ule ule, unadhani uchawi wake katika HERENI (pete za masikioni) utakuwa umebadilika??.. Jibu ni la! Utakuwa ni ule ule tu.

Tafakari, tafakari mama, tafakari dada, tafakari kaka unayevaa hereni, kuambiwa usivae hereni sio kwamba unawekwa chini ya sheria, hapana!.. bali kinyume chake ndio UNAKUWA HURU… Lakini kuvaa hereni ndio sheria, kwani itakulazimu kila siku kuivaa kabla ya kutoka nje, na kubadilisha aina ya hereni leo hii kesho ile, sasa huoni kama hiyo ndio SHERIA???, na kutokuvaa hereni ndio uhuru??.

Ni kweli ukiacha kuzivaa utaonekana si mrembo kwa baadhi ya watu, lakini utakuwa umejiepusha na ibada za sanamu, ambazo zitakuzalia madhara mengine makubwa kiroho.

Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, sawasawa na 1Wakorintho 3:16, na 1Wakorintho 6:19.

Kwa jinsi tunavyozidi kuiweka kuwa mitakatifu, ndivyo Roho Mtakatifu anavyokaa ndani yetu, na ndivyo tunavyomfaidi Roho Mtakatifu kwa matunda yake yaliyotajwa katika Wagalatia 5:22.

Bwana akubariki sana.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

                          Rudi Nyumbani.

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments