Swali: Neno Hiba linamaanisha nini kwenye Biblia kwa mujibu wa andiko hili, Wimbo 3:10.
Jibu: Turejee..
Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa urujuani, Gari lake limenakishiwa njumu, HIBA ya binti za Yerusalemu”.
“Hiba” kama ilivyotumika hapo inamaanisha “Mapenzi ya Kina (yale yaliyozama kabisa)”
Kwahiyo hapo kwa Kiswahili chepesi kabisa mstari huo unaweza kusomeka hivi.. “..Gari lake limenakishiwa njumu, MAPENZI YA DHATI ya binti za Yerusalemu”
Mstari huu unaelezea Machela ya Mfalme Sulemani (yaani kiti chake kinachotumika kumbebea, anaposafiri) jinsi kilivyopambwa vizuri, na jinsi kilivyo na ufahari, lakini hayo yote si kitu zaidi ya Upendo wa dhati.
Hivyo Upendo wa dhati unaotoka kwa hadhira ya binti za Yerusalemu ni bora kuliko fedha na dhahabu, na huo unaeleza zaidi uthamani wa kitu kuliko mapambo mengine yote.
Je umempa YESU maisha yako?
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?
UWEZO WA KIPEKEE.
TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU.
FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.
NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.
Print this post
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ