MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Baraka ni karama ya Mungu, na kila mmoja wetu aliyekombolewa na Yesu, ahadi hiyo ni yake. Baraka zimegawanyika mara mbili, zipo baraka za mwilini, na baraka za rohoni. Lakini kubwa zaidi ni zile za rohoni. Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyoeleza Baraka za Mungu. Lakini pia ikiwa utapenda kupata vifungu mbalimbali, pamoja na mafundisho mazuri ya Neno la Mungu, bofya link hii uweze kujiunga na kundi letu la Whatsapp>>> WHATSAPP GROUP

Wafilipi 4:19  “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu”

Yakobo 1:17  “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”.

Hesabu 6: 24 “Bwana akubarikie, na kukulinda;  25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;  26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani”

3Yohana 1:2  “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”

2Wakorintho 9:8  “Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;”

Kumbukumbu 28:2 “na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.  3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.  4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.  5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.  6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo”.

Waefeso 1:3 ” Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;”

Mathayo 6:30 ” Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? 31  Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32  Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33  Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34  Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”

Malaki  3:10 “Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Zaburi 20:4 “Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote”.

Mathayo 5:6  “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa”.

Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”

Yeremia 17:7 “Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake”

Pia Kwa wokovu/ maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU KIFO.

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Smaili Kiza magambi
Smaili Kiza magambi
2 months ago

Amen

Kambale lajoie
Kambale lajoie
1 year ago

MUNGU ATUPATIYE BARAKA ZAKE, NASEMA ASANTE KWAKUTUJALI MPAKA SASA.

Alex
Alex
1 year ago

Nashum kuru mungu ya maneno mzuri sana katika kanisa na biblia moja dunia leo ni furaha mimi mtoto ya mungu thank you God of time Amen of people