Mstari mfupi kwenye biblia

Mstari mfupi kwenye biblia

Mstari mfupi zaidi kwenye biblia ni upi? na umebeba ujumbe gani?

Mistari inatofautiana urefu kulingana na lugha na lugha.. Mstari unaoonekana mfupi katika lugha ya moja unapotafsiriwa katika lugha nyingine unaweza kuwa mrefu kuliko mistari mingine.

Kwamfano katika lugha ya kiingereza, mstari ulio mfupi kuliko yote unapatikana katika kitabu cha Yohana 11:35 unaosema kwa kiingereza “Jesus wept” Lakini tukiurudisha kwenye lugha Kiswahili unasomeka kama “Yesu akalia machozi”, Hivyo kuufanya mstari huo kutokuwa mfupi kuliko mingine katika lugha yetu.

Sasa mstari mfupi kuliko yote kwenye lugha ya Kiswahili ni upi? (Katika agano jipya).

Ni mstari unaopatikana katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:20 unaosema “msitweze unabii”.

Huo ndio mstari mfupi kuliko yote, katika biblia ya Kiswahili, ( Agano jipya) Na ndio ujumbe mfupi kuliko yote aliouchagua Roho Mtakatifu kwa watu wanaozungumza lugha ya Kiswahili, kwamba “tusitweze unabii”, au kwa lugha rahisi “Tusidharau wala kupuuzia unabii”.

Na unabii unaozungumziwa hapo kwamba tusiudharau/ tusiutweze sio nabii zinazosikika sasahivi za wanaojiita manabii au wanaojulikana kama manabii, hapana! Bali Nabii zilizoandikwa kwenye biblia, mfano wa Nabii hizo ni zile Bwana Yesu alizozitaja katika Mathayo 24, zinazohusiana na kurudi kwake kwamba Nyakati kutatokea vita, njaa, manabii wa uongo, Tauni, matetemeko, upendo wa wengi kupoa n.k Hizo ndio nabii ambazo hatupaswi kuzipuuzia, kwa maana ni kweli zitatimia.

Kuzidi  kufahamu kwa kina Zaidi maana ya kutotweza unabii fungua hapa >>Msitweze unabii

Je umempokea Yesu?.. Je unajua kwamba kizazi tunachoishi ni kizazi ambacho kina uwezekano wa kushuhudia ujio wa pili wa Yesu dhahiri??

Maran atha!.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments