Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha

Jinsi ya kuandaa mahubiri ya kufundisha kanisani au kwenye semina.

Jinsi ya kuandaa mahubiri ya kufundisha kanisani au katika ibada. Zifuatazo ni dondoo chache zitakazoweza kukusaidia katika kuandaa Somo ambalo litakuwa na uvuvio wa Roho Mtakatifu.

1. Tafuta sehemu ya utulivu.

Hii ni hatua ya kwanza kabisa: Tafuta eneo lisilo na kelele, wala usumbufu, hakikisha husumbuliwi na mtu au simu. Hiyo inaweza kuwa katika chumba cha utulivu au mahali ambao hauwezi kusumbuliwa, Huo ni mlango wa kwanza unaouvuta uwepo wa Mungu karibu nawe, kwasababu maandiko yanasema Mungu wetu si Mungu wa machafuko (1Wakorintho 14:33) na pia ni Mungu anayezungumza katika mazingira tulivu.

1Wafalme 19:12 “na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu”.

Hivyo kabla ya kuanza kufikiri kuandaa somo au hubiri, jitenge na mazingira yote yatakayokuondolea utulivu, kwasababu ukikaa katika hayo mazingira hutamsikia Mungu, Hivyo zima simu kwa muda na pia kaa peke yako kwenye utulivu.

2. Kuwa na Kalamu na Karatasi.

Hii ni hatua ya pili: Andaa kalamu na karatasi kwasababu kabla ya kwenda kuwafundisha wengine, Roho Mtakatifu atakufundisha wewe kwanza.

Warumi 2:21  “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe”

Kwahiyo wewe ni mwanafunzi wa kwanza wa Roho Mtakatifu kabla ya kwenda kuwafundisha wengine, na Mwanafunzi bora ni sharti awe na kalamu na karatasi kwa lengo la kuyarekodi yale anayojifunza. 

Usipokuwa na sehemu ya kurekodi yale utakayoenda kujifunza itakuwa ni ngumu hata kuyashika..

3. Fungua kwa Maombi.

Omba utakaso kwaajili ya nafsi yako, Omba uwepo wa Mungu ushuke mahali hapo, omba utakaso wa eneo ulilopo, omba roho ya ufunuo ishuke juu yako, kemea nguvu za giza na  zinazoshindana na azimio lako hilo (Tumia muda kidogo kuomba kwa kumaanisha).

4. Anza kusoma biblia na kutafakari

Baada ya maombi, anza kusoma biblia huku ukiruhusu akili yako itafakari. Wengi wakifika hii hatua wanafungua tu biblia na kutafuta mistari wanayoifahamu au watakayokutana nayo kwanza, pasipo kuruhusu tafakari katika fahamu zao.

Siri moja ya Roho Mtakatifu ni kwamba anazungumza na sisi pale tunapotafakari na si pale tunapoziba tafakari zetu. Unapokuwa katika kutafakari ndipo Roho Mtakatifu naye anaungana na tafakari zako pasipo kujua na ghafla unajikuta unafunguka akili na kujikuta unapokea vitu vipya, ambavyo ulikuwa huvijui, vitu hivyo vipya ambavyo ulikuwa huvijui vinavyokubaliana na Neno la Mungu ndio sauti ya Roho Mtakatifu, hivyo andiko hivyo ulivyovipokea kwasababu ndio vitakuwa sehemu ya somo lako ambalo Roho Mtakatifu anataka ujifunze wewe kwanza kisha ukawafundishe na wengine.

5. Omba tena

Hii ni hatua ya mwisho, baada ya kusoma na kutafakari kwa muda mrefu, na kupokea Funuo nyingi. Omba maombi ya mwisho ya kushukuru, kisha funga daftari lako.

Darasa lijalo tutajifunza jinsi ya kusimama na kufundisha kile ulichofundishwa na Roho Mtakatifu. Kwani ni muhimu pia kujua jinsi ya kufundisha ili usije ukajikuta unamzimisha Roho. (Kanuni ya kufundisha kwa matokeo yaliyokusudiwa ni rahisi sana, usikose darasa lijalo).

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

Wanikolai ni watu gani? Katika biblia?

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments