JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

Shalom, nakusalimu katika jina la Yesu Kristo mwokozi wetu. Karibu tujifunze maneno ya uzima maadamu siku ile inakaribia.

Katika siku hizi za mwisho ni lazima uwe makini sana na mahali ulipo, kwasababu zama zimebadilika, si kila jambo la kuliamini, vilevile si kila jambo la kutoliamini. Unamuhitaji Roho Mtakatifu sana kukusaidia kuchagua kilicho sahihi.

Bwana anatufananisha sisi na kama kondoo, na yeye kama mchungaji. Na sikuzote, mchungaji mwema, huwa anawapeleka kondoo wake katika maji ya mito-salama. Na si kila mto ilimradi mto tu anawapeleka kondoo zake kunywea maji hapana, bali pale tu palipo na maji ya utulivu ndipo anapowapeleka kondoo zake.

Ndio maana katika Zaburi ya 23 Inasema;

Zaburi 23:1 ‘Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.  2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza’.

Ni kwanini maji ya utulivu, kwasababu maji yenye mvurugano, au yaliyotibuliwa yana hatari nyingi, huwenda ni makao ya viboko na mamba na hivyo kutembea kwao huko ndio kunafanya maji Yale yawe na mvuragano, kwahiyo kondoo akinywa maji pale yupo hatarini kuvutwa na mamba, akafanyika kitoweo.

Au huwenda maji hayo ni mkondo wa mafuriko, hivyo kitu chochote kitakachotelezea kule mtoni, si rahisi kupona kinyume chake ni kitasombwa na kupotelea mbali.

Hivyo maji yasiyotulia, si salama kwa mifugo. Na mchungaji apendaye kondoo huwa hawapeleki mifugo yake hapo.

Ndivyo ilivyo kwa Kristo, anapotuokoa, anatuongoza kwa Roho wake malipo na maji ya utulivu tukae hapo tunywe. Lakini tatizo linakuja ni sisi kuyakataa maji ya utulivu, tunayatafuta maji ya mivurugano.

Ndugu usiangalie ukubwa wa mto, au ukubwa wa Bwawa, haikuhitaji wewe kunywa mto mzima ndio ukate kiu yao. Naamanisha usiangalie wingi wa watu, au ukubwa wa jengo na madhabahu iliyopambwa, au utajiri wa kanisa ndio ufikiri kuwa hapo ni salama kwa roho yako. Bali tazama palipo na utulivu wa kiroho. Hapo ndipo utulize nafsi yako. Kwasababu unaweza kwenda mahali kwa lengo la kuikata kweli kiu yako kwa Bwana lakini kinyume chake ukakutana na mamba wakali wakakumaliza kabisa.

Palipo na maji salama ni wapi?

Kwanza ni pale Palipo na fundisho la Yesu: Yesu ndio maji yenyewe tulivu ya uzima, na sio nabii au mtume au askofu, au kanisa, au pesa, au umaarufu.. Hivyo angalia kiini cha fundisho unalofundishwa mahali ulipo, je yote yanalenga kukukuza kumjua Yesu au linakupeleka katika mambo mengine? Fikiri Tangu umekaa hapo, ni nini umeongeza katika kulijua Neno la Kristo katika kweli yote. Lakini Kama umejazwa maarifa ya ki-mwili tu zaidi yale ya Kristo, yaani  ya ki-ndoa, ki-uchumi, uchawi, biashara,pesa, hiyo ni injili nyingine, ni mafuriko ya adui, hakuna maji tulivu hapo, utazombwa na kuangamia kabisa.

Yohana 4:13  “Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; 14  walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele”

Palipo na Upendo: Hicho ni kigezo cha pili.

Yakobo 3:16  “Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya”.

Katika mkusanyiko wowote, fundisho la tendo la upendo wa ki-ndugu linapuuziwa, au halihimizwi, ndani  kuna vita visivyokoma kati ya washirika, pengine huwenda na viongozi kwa viongozi, hiyo ni ishara kuwa utulivu wa Roho haupo hapo, hivyo ni hatari pia kwa maisha yako ya kiroho.

Tujitahidi sana kuwa na vipimo hivi vya kiroho katika kuchagua mahali tukusanyakapo kupata maji ya uzima, vitakusaidia sana, kwasababu hizi ni siku za mwisho, na manabii wengi na makristo wa uongo na madhehebu na dini za uongo  zimezuka kila pembe ili kuwatoa watu kwenye mstari.

Yajali maisha yako ya kiroho. Mpende Kristo na Agizo lake.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

JE! UNAMPENDA BWANA?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments