Sera za Faragha (Privacy policy)

Sera za Faragha (Privacy policy)

Ifuatayao ni Sera ya Faragha ya Tovuti/App ya Nuru ya Upendo (wingulamashahidi.org)

Tarehe ya Mwisho wa Marekebisho: [21/05/2025]

Tunapenda kukushukuru kwa kuchagua kutumia kituo cha Wingulamashahidi, jukwaa la injili ya YESU KRISTO, mafundisho ya Biblia, maombi, na jumbe za wokovu kupitia tovuti yetu na app yetu rasmi. Tunathamini faragha yako na tunajitahidi kuhakikisha taarifa zako zinalindwa kikamilifu.


1. Taarifa Tunazokusanya

Lengo la kukusanya taarifa zako ni kukuletea huduma ya kiroho iliyo bora zaidi. Na taarifa tuzikusanyazo ni:

  • Taarifa  Binafsi (kama utazijaza): ambazo ni Jina lako, barua pepe, namba yako ya simu.

  • Taarifa za Kiufundi: Aina ya kifaa unachotumia, anwani ya IP, aina ya kivinjari, lugha, na mfumo wa uendeshaji.

  • Taarifa za Matumizi: Maudhui unayoyasoma, au kupakua, au kushiriki. Hii inatusaidia kujua aina gani ya masomo yanayopendelewa zaidi na watu.


2. Jinsi Tunavyozitumia Taarifa hizo

Taarifa hizi zinahitajika kwa:

  • Kukurushia masomo mapya kwenye barua pepe yako.

  • Kuboresha muundo na mwonekano wa tovuti pamoja na app

  • Kujibu maswali yako, maombi ya maombi, au mawasiliano mengine ya kiroho..


3. Ulinzi na usalama wa Taarifa Zako

Hatua za kiusalama tunazizingatia  (kama SSL, uthibitisho wa watumiaji, na encryption) kuhakikisha taarifa zako hazidukuliwi na yoyote, wala kupotea, wala kutumiwa bila idhini ya mhusika. Pia tunazingatia kanuni za kimaadili kulingana na ukristo.


4. Ushirikishaji wa Taarifa

Hatutashiriki wala kuziuza, kusambaza, au kugawa taarifa zako binafsi kwa mtu mwingine yoyote bila idhini yako isipokuwa:

  • Kwa mujibu wa sheria au maelekezo ya mamlaka husika.

  • Kwa watoa huduma wanaotusaidia kutoa huduma hizi (mfano: huduma ya kutuma barua pepe), kwa masharti ya usiri.

  • Ikiwa kama utachagua kushiriki jumbe kwenye mitandao ya kijamii.


5. Watoto

Hatukusanyi taarifa za watoto walio chini ya miaka 12 bila idhini ya wazazi au walezi. Ikiwa mzazi ataona kuwa kuwa mtoto wake ametoa taarifa binafsi bila idhini yao, basi tunaomba awasiliane nasi ili tuchukue hatua za kuondoa taarifa hizo mara moja.


6. Haki Zako

Unayo haki ya:

  • Kufahamu ni taarifa gani tulizonazo kuhusu wewe.

  • Kuomba taarifa zako zifutwe au kurekebishwa inapohitajika.

  • Kujiondoa kwenye orodha ya wanaopokea pokea mafundisho kwa njia ya barua pepe au yoyote ile.

  • Kuhoji matumizi ya taarifa zako kwa ajili ya tafiti, chunguzi au matangazo (kama yatakuwepo).


7. Vidakuzi (Cookies)

Tovuti yetu hutumia cookies ili kuboresha matumizi yako. Unaweza kuchagua kuzima kama haitakuwa ni mapendekezo yako, lakini hii yaweza kuathiri usomaji wako wa tovuti.


8. Mabadiliko ya Sera ya Faragha

Patakapotokea mabadiliko ya Sera hizi, tutakujuza mabadiliko hayo kupitia tovuti z. Mabadiliko huanza kutumika mara moja baada ya kuchapishwa.


9. Mawasiliano

Kwa maswali kuhusiana na sera hizi za faragha, tafadhali wasiliana nasi kupitia:

Barua pepe: wingulamashahidi@gmail.com
Tovuti: https://wingulamashahidi.org


Mungu akubariki sana kwa kuwa sehemu ya huduma hii. Tunakuombea baraka za Bwana YESU ziende nawe

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Shalom

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments