Kijana ni nani kibiblia?

Kijana ni nani kibiblia?

Biblia haitoi umri fulani maalumu kwamba mtu akiufikia huo basi ndio huitwa kijana.. Japokuwa ni mtu ambaye yupo umri wa hapo katikati yaani utoto na utu uzima, lakini hutambulika kwa kuangalia vitu kama hatua za ukuaji wake, uwajibikaji wake na uzoefu wake wa kimaisha.

Kwamfano katika biblia watu hawa walitajwa kama vijana.

  • Ishmaeli (mwanzo 21:14-20)
  • Isaka (Mwanzo 22:5)
  • Yusufu mwanzo 42:22. (Akiwa na miaka 17)
  • Mfalme Sauli (1Samweli 9:2)
  • Timotheo (1Timotheo 4:12)

Na wengine kadha wa kadha..

Yafuatayo ni Mambo ambayo kijana yeyote anatarajiwa awe nayo kibiblia.

1) Awe anamtafuta Mungu Na kulitii Neno la Mungu.

Mhubiri 12:1

[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

Zaburi 119:9

[9]Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako. 

2) Awe na hekima na tabia ya uongozi, (yaani wakati wote ajifunze kuwa kielelezo.)

1 Timotheo 4:12

[12]Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.

3) Awe na nguvu za rohoni, za kumshinda shetani.

Mithali 20:29

[29]Fahari ya vijana ni nguvu zao,..

1 Yohana 2:14

[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Lakini pia kijana anakabiliwa na tamaa za ujanani kama vile uzinzi, anasa,starehe..hivyo Anatarajiwa azikimbie wakati wote.

2 Timotheo 2:22

[22]Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.

Kutokana na vigezo hivyo tunaweza Kuona ujana pengine huanzia umri wa kubalehe, mpaka wakati mtu anapungua Nguvu zake mwilini.. labda Miaka 12-45…japo yaweza kupungua au kuzidi..

Zingatia:

Ikiwa wewe ni kijana, hakikisha maonyo hayo unayatendea kazi mapema…

Lakini ikiwa wewe ni mzazi na una mtoto, fahamu kuwa siku moja atakuwa kijana,hivyo kabla adui hajamtumia, anza kumjengea misingi mizuri ya kutembea katika Imani ya wokovu, naye hataicha njia hiyo mpaka atakapokuwa mtu mzima

Mithali 22:6

[6]Mlee mtoto katika njia impasayo,

Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIJANA NA MAHUSIANO.

Je Bwana YESU alikuwa na amri ya kumwingiza mtu katika ufalme wa MUNGU au hakuwa nayo?

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments