JIBU: Tukiangalia mwanzo wa mstari huo, unasema..
Mithali 11:16 Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; Na watu wakali hushika mali siku zote.
Ukitazama tafsiri nyingine maana iliyonyooka zaidi ya mstari huo, unasema “mwanamke wa adabu huheshimwa daima, lakini watu wakali hushika tu mali”.
Yaani unalinganisha, sifa njema, na vitu vingi, akilinganisha mwanamke anayewekeza maisha yake katika tabia nzuri, matokeo yake heshima itakuwa kwake ambayo itadumu daima, lakini mtu mkali anayewekeza katika kujilimbikizia mali isivyo halali, akiwakandamiza wengine, akitumia ukali, akiwanyima mshahara wengine, ni kweli na yeye atapata matokeo yake ambayo ni mali nyingi tu. Lakini hana heshima yoyote nyuma yake. Haachi kitu chenye thamani kitakachoweza kuwa faida kwa wengine, hana la kuigwa, hana la kusifiwa isipokuwa, malalamiko, uchungu na machozi kwa wengine.
Hivyo andiko hilo linalinganisha sifa njema na mali. Ni heri ujijengee sifa njema ambayo hiyo itafuatwa na vizazi hata vya mbeleni, kama vile tuwaonavyo wanawake wacha Mungu kwenye maandiko, mfano wa Ana binti Fanueli, Mariamu, Sara, watu kama akina Ayubu, Danieli, Yusufu, ambao njia zao huigwa hata sasa, kuliko kuwa kama Nabali aliyetajirika lakini mpumbavu, hana chochote cha kuigwa na watu.
Ni heri maskini ahubiriye watu, na kuwaleta kwa Kristo, wanaacha dhambi, na kupokea Roho Mtakatifu, kuliko mtu yule ambaye kutwa nzima anachowaza ni kujiwekezea nafsi yake, kuiba, na kudhulumu, kutumia ukali kupata mali mambo ambayo yataishia hapa hapa tu duniani.
Mithali 22:1 Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’
Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,
Print this post
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ