Isaya 50:8 “Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye HASIMU yangu? Na anikaribie basi”.
“Hasimu” maana yake ni “mpinzani”…Kwahiyo andiko hilo kwa lugha nyingine laweza kusomeka hivi…
Isaya 50:8 “Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye MPINZANI WANGU? Na anikaribie basi”.
Andiko hili linaelezea nguvu wanayotembea nayo watu wa MUNGU, kwamba wanao ulinzi mkubwa zaidi ya wote na wanao utetezi mkubwa zaidi ya wenngine wote, kwasababu mbingu inawatetea daima.
Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?”.
Je na wewe umezungukwa na Mahasimu? Je mtetezi wako ni nani katikati ya hao?.
Ni heri Mtetezi wako akawa YESU leo, kwasababu wanadamu wala mashetani hayawezi kukutetea wakati wa matatizo bali yatakuwa Mahasimu wako tu siku zote.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Print this post
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ