Baghairi ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 11:28?

Baghairi ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 11:28?

Baghairi ni neno la kiunganishi lenye maana ya… “Mbali na”. Kwamfano nikitaka kusema.. “Mbali na yote ninayoyapitia bado nitasimama imara katika Imani”..naweza kuisema sentensi hiyo kama ifuatavyo “Baghairi ya yote ninayoyapitia bado nitasimama imara katika Imani”

Sasa katika biblia hilo neno limeonekana mara moja tu!. Katika kile kitabu cha 1Wakorintho 11:28

1Wakorintho 11:27 “katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.

28 BAGHAIRI ya mambo ya nje, yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa yote.”

Jambo dogo tunaloweza kujifunza kupitia mstari huo, ni kwamba.. Mtume Paulo, pamoja na wakristo wa kwanza walipitia dhiki nyingi, kwaajili ya Injili na wala hawakuikana imani, Ndio maana ukianzia juu kidogo, mwa mstari huo, utaona hilo jambo…

Waebrani 13:23 “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana;

katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.

24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.

25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;

26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga

mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.

28 Baghairi ya mambo ya nje, yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa yote”.

Bwana atusaidie tuzidi kujikana na kujitoa kwaajili ya injili.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Neno Bildi linamaanisha nini kwenye biblia(Matendo 27:28) ?

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

LANGO LIMEBADILIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments