IJUE KANUNI YA KUREJESHA NGUVU ZA KIROHO.

IJUE KANUNI YA KUREJESHA NGUVU ZA KIROHO.

Je Imani yako imefifia?, je upendo wako umepoa?, je Amani yako imepungua?, na haki yako imepoa?.. Na hujui cha kufanya na ndani bado una haja sana ya kuwa na mambo hayo?.. Basi suluhisho lipo ndani ya biblia.

Ifuatayo ni kanuni moja nyepesi ya kurejesha joto la ROHO MTAKATIFU ndani yako. Kumbuka mtu aliyejaa Roho Mtakatifu ataonyesha matunda yafuatayo…

Wagalatia 5:22  “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23  upole, kiasi;…”.

Ikiwa mambo haya yalikuwa ndani yako lakini sasa huyaoni tena, au ikiwa hauna kabisa, basi tumia kanuni ifuatayo kuyarejesha/kuyajenga ndani yako.

KAA KARIBU NA WATU WATU WANAOMWITA BWANA.

Watu wanaomwita Bwana, kwa lugha nyingine ni watu waliookoka kikweli kweli,…Utauliza kwa namna gani?…Tusome maandiko yafuatayo..

2Timotheo 2:22  “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, PAMOJA NA WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI”.

Hapo mwisho anasema, ukatafute haki, Imani na upendo na amani “pamoja na wale wote wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Kumbe! Haki inapatikana kwa watu wanaomwita Bwana kwa dhamiri safi, kumbe tukikaa na watu waliomaanisha kumwita Bwana na kumtafuta basi Amani tutaipata, na upendo na Imani.

Kama maandiko yasemavyo kwamba “chuma hunoa chuma, Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake” (Mithali 27:17). Vivyo hivyo na sisi tunapokaa na watu wenye kumaanisha kumtafuta Mungu basi ule moto ulio ndani yao atahamia na kwetu pia.

Lakini tukijitenga na kubaki wenyewe, au tukijumuika na watu wengine wasio na nia ya dhati kumtafuta Bwana, ni ngumu kuuwasha ule moto wa Roho ndani yetu!, tutabaki kama tulivyo!.. Kanuni ni kukaa pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi!…Vile vile tunapojitenga na kuamua kukaa peke yetu kwa muda mrefu ni pia ni hatari!!.. Imani, amani, upendo na haki yako vinaweza kuathirika pakubwa.

Sasa tunawapatia wapi watu wamwitao Bwana kwa moyo safi?.

1.Katika kanisa lililo hai.

Hii ni sehemu pekee ambayo utawapata watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, jiunge na kanisa la kiroho lililo karibu nawe, au hata lililo mbali ikiwa lililo karibu nawe halina utakatifu. Jumuika na watu hao, katika utii na unyenyekevu, na katika ibada zote, na hapo Roho Mtakatifu atakujenga ndani yako na kukujaza nguvu zake, utaona Imani yako inapata nguvu, upendo wako uliopoa unawaka tena, haki yako iliyopotea inarudi na Amani yako pia inahuika upya, na ifanye hiyo iwe desturi yako daima.

Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine;..”.

Na utajuaje kanisa hilo, ni la kiroho?.

Kigezo cha kwanza ni mwonekano wa nje wa waabuduo wa mahali hapo!, ukiona mwonekano na mazungumzo ya waabuduo si ya kiMungu, kwamba wanazungumza kidunia na wanavaa kidunia, kiasi kwamba hauoni tofauti na mtu anayeenda disko na anayeshiriki mahali hapo, basi tuchukua tahadhari hapo si sehemu salama!.

Vile vile mafundisho yanayofundishwa mahali pale kama hayalengi TOBA, na UJIO wa PILI wa BWANA YESU, na UTAKATIFU wa MWILINI na ROHONI, pia hapo si sehemu salama, lakini kama kanisa lina vigezo hivyo vya Utakatifu wa kimafundisho na kimwonekano, basi ndani yake watakuwepo watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, kaa hapo na utaona mabadiliko makubwa ya kiroho ndani yako.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments