Wagerasi ni nchi gani? (Luka 8:26-39)

Wagerasi ni nchi gani? (Luka 8:26-39)

Wagerasi ni watu waliokuwa wanaishi katika mji ulioitwa Gerasi ambao ulikuwa kusini mashariki mwa bahari ya Galilaya. (Tazama kwenye picha)

Ulikuwa ni moja ya miji ya Nchi ya Dekapoli. Nchi ya watu wa mataifa.

ndio kule ambako Yesu alivuka na kukatana na wale watu waliokuwa vichaa wakali, akawafungua.

Marko 5:1-3

[1]Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. 

[2]Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; 

[3]makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; 

Urefu wa habari hii fungua hapa >>ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Mathayo 8:28-34, na Luka 8:26-39.

Ni nini ambacho Bwana anataka tujifunze kwa hawa wagerasi? 

Ni watu ambao walithamini, hazina zao, mali zao, utajiri wao, zaidi ya kufunguliwa kwao, ndio maana mara tu walipoona nguruwe wao wamekufa wote, jambo hilo liliwafanya wawe na hofu, na hiyo ikawapelekea kumsihi Yesu aondoke katika nchi yao, asije akaleta hasara zaidi.

hawakuona wokovu ule mkuu uliowafikia, waliona hasara waliyopata. Hiyo ni mbaya sana,  kwa urefu ya jambo hilo pitia hili somo.

Kamwe usiwe mgerasi.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine: 

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments