JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

Wimbo Ulio Bora 3:1-4

[1]Usiku kitandani nalimtafuta mpendwa wa nafsi yangu, Nalimtafuta, nisimpate.

[2]Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini,  Katika njia zake na viwanjani,

Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu. Nikamtafuta, nisimpate.

[3]Walinzi wazungukao mjini waliniona; Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?

[4]Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena,  Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu,  Chumbani mwake aliyenizaa.

Kitabu cha wimbo ulio-bora, ni kitabu ambacho huchukiliwa kimwili na watu wengi kana kwamba kiliandikwa mahususi kwa wana-ndoa.. Jambo ambalo sio kweli, Ikumbukwe kuwa dhumuni kuu la biblia ni kutueleza WAZO la Mungu, juu yetu ambalo hilo alilikamilisha kifasaha kupitia Yesu Kristo. Hivyo popote pale unapopasoma kwa namna moja au nyingine inaeleza kusudi la Mungu kwetu, katika kuyatimiza mapenzi yake..

Na ni kawaida yake tangu zamani  kutumia mifano halisi ya namna mbalimbali ili kudhihirisha kusudi lake kamilifu kwetu.

Kwamfano ameweka familia, tujue sifa za wazazi ili tunapomwita Mungu Baba, tujue tabia za ubaba hasaa zipoje…Ameweka mabwana na watumwa ili tunapomwita yeye Bwana tujue sisi tunapaswa tuweje kwake kama watumwa..

Vivyo hivyo ameweka ndoa, na akajifunua kwetu kama mume, na sisi kanisa ni mke wake…Hivyo anataka tujue kama vile upendo wa mke na mume ulivyo ndivyo alivyo yeye kwetu sisi.

Sasa Katika habari hii, tunaona sifa ya upendo ambao Mungu anataka sisi tuuonyeshe kwake, Upendo usio ule wa upande mmoja, bali na upande wa pili, yaani sio  tu yeye kututafuta sisi wakati wote hapana bali Na sisi tumtafute yeye..

Anaeleza kwa mfano wa igizo picha ya  mwanamke ambaye yupo sikuzote na mpenzi Wake kitandani, lakini ikatokea siku moja alipoamka usiku hakumwona kitandani Mwake…

Hivyo hakuweza kuendelea kulala angali mumewe hayupo, ikambidi atoke aanze Kumtafuta usiku ule ule, sio kwa siri Bali hadharani tena sehemu zenye hatari ambazo walinzi tu usiku hupita kufanya doria..Na alipokutana Nao akawauliza juu ya mpenzi wake kama wamemwona, lakini Baadaye kidogo alimwona..akamkumbatia na kurudi naye mpaka mahali pao maalumu.

Ufunuo wake ni upi.

Yapo majira wewe kama mwana wa Mungu utapitia pengine hali fulani ya kushuka viwango kiroho, (ukame wa kiroho)

Lakini ukiwa na upendo wa kweli kwa Mungu wako, ni wazi kuwa hutakaa tu na kusema Mungu nisaidie…Hapana Utachukua tu hatua kama za huyu mwanamke ya kuamka na kuanza kutafuta namna ya kumtafuta mpenzi wako (Kristo) yaani kurejesha viwango vyako vya mwanzoni, hata kwa kugharimika raha, au vitu n.k..

Ndio hapo mtu hutenga muda mwingi wa maombi, mikesha, mifungo n.k.

Na kama vile yule Mwanamke alipowafuata walinzi usiku, kuwauliza habari za mumewe…Ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye kiu na pendo na Mungu hataridhika kutembea yeye kama yeye tu, ataulizia msaada mpaka kwa viongozi wake wa kiroho apate mwongozo..(ambayo hufunua wale walinzi). Na hatimaye kufikia kilele cha mahusiano na Mungu wake tena.

Ndugu, kumbuka kuwa furaha, na amani, uzuri wa Kristo sio tu wa kuletewa sikuzote, bali pia wa kutafuta…Ni kweli siku za kwanza za wokovu uliona Kristo akijifunua Kwako kwa namna za ajabu, hata kama hukufanya lolote lakini sasahivi ni kama huoni moto ule ule uliokuwa nao…jua tu si kwamba umetenda dhambi au umemkosea Mungu…hapana ni kwamba Mungu anataka amke sasa mtafuta mpenzi wako..kudhihirisha upendo wa kweli..

Ndicho Yesu alichowaambia wale waandishi na mafarisayo juu ya wanafunzi wake..

Marko 2:18 Nao wanafunzi wake Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
19 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.
20 Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku ile

Ongeza mikesha, mifungo, kusoma Neno sana…Na hatimaye utavipata na furaha yako itazidi ile ya kwanza…

Kwasababu upendo wa kweli hutafuta…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Naomba kujua maana ya haya maneno katika biblia..“Siti Msharifu”, “Mitalawanda” na “kulalama”

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments