Kutoka 33:17 “Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, NAMI NAKUJUA JINA LAKO
Jina la Mtu limebeba siri kubwa sana, lakini kabla ya kutazama jina la MUNGU.
Kitu pekee kilichomtambulisha na kinachomtambulisha MUNGU kwetu sasahivi ni JINA LAKE!.. Kamwe hajawahi kutuonyesha Sura yake, wala kuitangaza mahali popote pale!, bali jina lake.. bali jina lake amelitangaza na kulitukuza sana..
Sasa si kwamba anapenda kujificha kwetu!.. La bali ametuchagulia kilicho bora kwake tukijue!.. Kwahiyo kulicho bora kwake kwetu ni jina lake zaidi ya sura yake.
Na kilicho bora kwa MUNGU kwetu kukijua ni MAJINA YETU zaidi ya SURA ZETU… Utauliza kivipi?..
Kitu pekee kinachoko sasa mbinguni kinachotutambulisha sisi sio SURA ZETU bali ni MAJINA YETU.. Mbinguni hakuna picha zetu!, bali majina!..
Ufunuo 13:8 “Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye JINA LAKE HALIKUANDIKWA katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia”.
Soma pia Ufunuo 17:8, Ufunuo 3:5, Wafilipi 4:3 utaona hakuna sura kule za watu kule mbinguni… hivyo uzuri wako wa sura, weupe wako, weusi wako, urefu wako, ufupi wako, unene wako, ubounsa wako na wangu unaishia hapa!!!..
Hiyo pia ndio sababu ya Bwana YESU kuwaambia wanafunzi wake wasifurahia pepo wanavyowatii bali wafurahie majina yao yameandikwa mbinguni…
Luka 10:20 “Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni”.
Na unajua, Mungu anatujua kwa majina zaidi ya Sura na rangi?…ndivyo alivyomwambia hata nabii Musa.
Kutoka 33:17 “Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, NAMI NAKUJUA JINA LAKO”.
Umeona hapo?.. Mungu anamwambia Musa anamjua jina lake, sio sura yake…. Kwahiyo ni muhimu sana kuaangalia MAJINA YETU na kuyatengeneza…. Maandiko yanasema ni heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi..
Mithali 22:1 “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi…”
Sasa tunachaguaje majina??.. je tubadilishe majina tuliyonayo?.. jibu ni La!.. tutaendelea kuwa na majina yetu haya haya ikiwa kama yana maana njema.. Lakini majina yetu haya haya yanaweza kubadilika na kuwa BORA..
Kwa jinsi jina lako linavyozidi kuwa Bora mbele za Mungu, ndivyo nafasi yako mbinguni inavyozidi kuwa kubwa, na kwa kadiri linavyozidi kufifia mbele za Mungu ndivyo mbinguni linavyofutika kumbukumbu lako..
Sasa tunafanyaje majina yetu kuwa Bora?.. Si kwa kwenda kuyatolea sadaka ya ukombozi, au kuyaombea kwenye mkesha.. La!.. unaweza kutoa sadaka za aina zote duniani na jina lako lisiwe mbinguni, lakini bado likaendelea kuwa kubwa mbele za watu, na unaweza kuwa na jina la heshima kwa mbele za watu lakini mbele za Mungu ukawa huna jina.
Ifuatayo ni njia pekee ya kulitakasa jina lako, na hivyo heshima yako, na hadhi yako.. na njia hiyo si nyingine zaidi ya KUMCHA MUNGU, na KUJITENGA NA DHAMBI.. Utauliza kivipi, tusome maandiko yafuatayo?.
Kutoka 32:31 “Musa akarejea kwa Bwana akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.
32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao — na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.
33 Bwana akamwambia Musa, MTU YE YOTE ALIYENITENDA DHAMBI NDIYE NITAKAYEMFUTA KATIKA KITABU CHANGU”.
Umeona kitu kinachochafua jina la Mtu?… ni DHAMBI, Hiko ndicho kinachomwondoa mtu kwenye kumbukumbu za MUNGU, na si tu mbinguni na hata duniani pia..
Kumbukumbu 29:20 “Bwana hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya Bwana na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na BWANA ATALIFUTA JINA LAKE CHINI YA MBINGU”.
Huenda dhambi imechafua jina lako!.. suluhisho ni moja tu, kutubu na kuacha dhambi!.. jina lako hilo litasomeka kwenye kitabu cha mwanakondoo mbinguni.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.
KWANINI TUNAOMBA KWA JINA LA YESU?
HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.
FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.
About the author