Njumu ni nini? (Wimbo 3:10)

Njumu ni nini? (Wimbo 3:10)

Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa urujuani, GARI LAKE LIMENAKISHIWA NJUMU, Hiba ya binti za Yerusalemu”.

Neno hili pia tunalisoma katika 1Nyakati 29:2..

1Nyakati 29:2 “Basi kwa uwezo wangu wote nimeiwekea akiba nyumba ya Mungu wangu, dhahabu kwa vitu vya dhahabu, na fedha kwa vitu vya fedha, na shaba kwa vitu vya shaba, na chuma kwa vitu vya chuma, na miti kwa vitu vya miti; vito vya shohamu, na vya kujazia, VITO VYA NJUMU, na vya rangi mbalimbali, na mawe ya thamani ya kila namna, na marimari tele.

“Njumu” ni malighafi za “kung’ara ng’ara/ kuwaka-waka” Tazama picha juu, mfano wa vazi lililonakshiwa na Njumu..

Na gari la Mfalme Sulemani kulingana na maandiko hayo ya Wimbo 3:10, lilikuwa limenakshiwa na malighafi hizo za kung’ara ng’ara, hivyo lilikuwa linavutia sana, lakini pamoja na kunakshiwa kwa vito hivo vyote vya thamani lakini bado sifa za binti Yerusalemu zilikuwa bora zaidi.

Kufahamu kwa kina Gari/Machela ya Sulemani jinsi ilivyokuwa na rangi ya Urujuani ilikuwaje fungua masomo chini ya somo hili, Bwana akubariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)

Urujuani ni nini? (Wimbo 3:10)?

Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Print this post

About the author

Nuru ya Upendo administrator

Leave a Reply