Swali: Kughofiri ni kufanya nini kama tunavyosoma katika Zaburi 79:9?.
Jibu: Turejee..
Zaburi 79:9 “Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. Utuokoe, UTUGHOFIRI dhambi zetu, Kwa ajili ya jina lako”.
Maana ya “Kughofiri” ni “kuondoa”.
Neno hilo limeonekana mara moj tu kwenye Biblia…na maana yake ni ile ile na ya kusamehe..
Lakini Biblia inazidi kutufundisha kuwa Bwana anatuokoa na kutusamehe pia makosa yetu kwaajili ya jina lake.
Maana yake pia kwa utukufu wa jina lake, anapotusamehe makosa basi pia jina lake linatukuzwa zaidi, hivyo ni fahari ya Mungu pia kutusamehe sisi.
Isaya 43:25 “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako”
Sasa swali kama Mungu anafurahia kutusamehe makosa yetu kwanini tusitumie hiyo fursa kuungama?.
Je umempokea YESU?.. Umetubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha?kama bado je unasubiri nini?…
Tubu leo upate msamaha wa dhambi, na upate ondoleo la dhambi pia.
Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; 47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.
Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NGUVU YA MSAMAHA
UMUHIMU WA KUOMBA MSAMAHA.
KAMA NISIPOKUTAWADHA, HUNA SHIRIKA NAMI
NINI MAANA YA UKOMBOZI?
ZIFAHAMU ALAMA KUU NNE ZA KRISTO NDANI YAKO.
Print this post
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ