Je umewaonea utungu watoto wako?

Je umewaonea utungu watoto wako?

Ulishawahi kuona mwanamke anajifungua mtoto bila kusikia utungu wowote? Hilo jambo bila shaka Litakuwa ni la ajabu… kwasababu haliendani kabisa na kanuni za asili …

hata maandiko yanasema hivyo..

Isaya 66:7-8

[7]Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume.

[8]Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara?..

Ni kanuni ya asili ili kiumbe kipya kizaliwe, mzaaji ni lazima apate utungu tu kama malipo ya kile akizaacho ..kila mwanadamu unayemwona chini ya jua, kuna mtu alipata maumivu kwa ajili yake..

Kanuni hii ipo rohoni pia…Kila mtakatifu unayemwona (aliyesimama), haikuwa bure bure…au kirahisi rahisi tu kama unavyodhani, kuna Waliopitia utungu juu yao…

Utauliza hili lipo wapi Kwenye maandiko?.

Paulo kwa Wagalatia,aliandika maneno haya;

Wagalatia 4:19

[19]Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu;

Paulo anawalilia wagalatia, kwa jinsi walivyoiacha neema ya Kristo, na kurudia mafundisho ya kiyahudi..anasema nawaonea utungu tena….tafsiri yake ni kuwa hapo nyuma alishawahi kuwaonea utungu…akawazaa…lakini sasa ni kama vile wanahitaji kuzaliwa tena….

Hivyo watu wote waliozaliwa mara ya pili wapo Waliowanea utungu.

Siku za Utungu mwanamke hupitia mambo haya:

1). Hulia na kuugua: 

Maana yake hiki ni kipindi cha machozi na kuomba juu ya wale wote unaotamani wampokee Kristo..ndiyo tabia waliokuwa nayo mitume.

Matendo ya Mitume 20:31

[31]Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi.

Watu wengi wanatamani kuona geuko la dhati kwa jamii zao, rafiki zao, waume zao, watoto wao lakini hawana muda wa kuwaombea kwa kuzama sana kwa kipindi kirefu na wakati mwingine kufunga huku wakiwahubiria…wanaikwepa Kanuni hii ya kiumbe kipya kuzaliwa.

2) Mwanamke hupitia hatari mbalimbali zinazohatarisha maisha; 

Hichi kipindi wanawake wengi huchungulia kifo, kwa sababu ya maumivu, au shinikizo au kutokwa na damu nyingi sana.

Ndivyo ilivyo pale unapojaribu, Kumvuta mwenye dhambi aifikie toba ya kweli, adui huanza kuinua vita, dhidi yako wewe na huyo unayemzaa.. lile joka litataka kufanya vita na wewe.

Ufunuo wa Yohana 12:1-4

[1]Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.

[2]Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.

[3]Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

[4]Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.

Ukijikuta katika wakati huu fahamu ni kung’ang’ana kumfuatilia kondoo huyo bila kujali hali au vipingamizi…unaweza kuona visababu sababu visivyoeleweka, mara hataki tena kukusikiliza, mara anaumwa, mara ndugu zake wanampinga, mara anakuwa mzito.hapa hupaswi kukata tamaa..endelea kumfuatilia kwasababu hizo ni hila za adui kumzuia asikate shauri kwa Bwana Yesu..

Fahamu tu kazi yako si bure upo wakati ataamini na kugeuka kabisa kabisa kwasababu Nguvu uliyonayo na kuu kuliko ya ibilisi..na furaha yako itakuwa ni pamoja na malaika mbinguni. (Luka 15:10).

Pia Biblia inasema…

Yohana 16:21

[21]Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.

Upo wakati utayafurahia matunda yako. Siku utakapoona kupitia hao makumi, mamia, maelfu ya watu wanaokoka..na siku ile Bwana anakupa thawabu kwa tunda hilo ulilomzalia.

Swali ni je utungu wako upo wapi?.. ni wapi unaweza kusema yule ni mwana wangu nimemzaa mimi katika Kristo?..

Kwenda tu kusema Yesu anakupenda okoka, halafu ukamwongoza Sala ya toba na kumwacha…hili halimaanishi huyo ni mtoto wako. Ndio maana wapo watu wengi wanaosema leo wamemkiri Yesu, lakini ukiwaangalia sio viumbe vipya..kwasababu hawakuzaliwa, bali waliaminishwa tu.

Tukubali kuzaa kwa kuwafundisha, kuwaombea sana, na kuwafuatilia mpaka watakapokata shauri la kweli kumpokea Yesu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments