UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.

UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.

Jina la Mwokozi YESU, Ngome Imara libarikiwe (Mithali 18:10).

Hatujaitwa kujipenda tu wenyewe, au kuwapenda wale wenye imani moja na sisi au watu wa familia zetu tu!, bali tumeitwa kuwapenda hata watu walio mbali na imani zetu, tamaduni zetu, na hata itikadi zetu (hao ndio Biblia imewatafsiri kama majirani zetu).

Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Katika Agano la kale ilizoeleka kufahamika kuwa Jirani wa mtu ni Yule wa jamii moja naye, itikadi moja naye, na hata Taifa moja naye, jambo lililowafanya wana wa Israeli wasiwe na ushirika na mtu mwingine yoyote kutoka katika Taifa lingine, na wala wasiwe na upendo na mtu wa Taifa lingine lolote na kuwaona wote maadui (Na kwa wakati huo hawakufanya kosa kwasababu hawakuujua ukweli wote wa Upendo wa Mungu).

Lakini alipokuja Bwana YESU, (mjumbe wa Agano jipya sawasawa na Waebrania 12:24) yeye alitukamilishia kweli yote..na kuwafundisha kuwa majirani zao si tu watu wa Taifa lao, au wanaowajua…

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Jambo hili Bwana Yesu aliliweka vizuri tena, wakati alipojiwa na yule mwanasheria ambaye alitaka kujionyesha yeye ni mwenye haki (kwamba anawapenda majirani zake) pasipo kujua jirani yake ni nani,

Huyu alipokuja alimwuliza Bwana je! Jirani yangu ni nani?.. kuna jibu Bwana alilompa, tusome..

Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.

29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?

30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.

36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni YUPI ALIYEKUWA JIRANI YAKE yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?

37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.

Kufuatana na mfano huu.. ni wazi kuwa huyu Mwanasheria alijiona kuwa yeye hana upendo kabisa!… Kwasababu hapo Bwana alikuwa anaonyesha kuwa Kuhani na Mlawi ambao walikuwa ni wayahudi, walishindwa kumsaidia myahudi mwenzao, aliyeangukia katika mikono ya wanyang’anyi, na badala yake anakuja kusaidiwa na Msamaria (mtu asiye wa imani yao wala Taifa lao).

Maana yake Yule Msamaria kafanya Ujirani mwema kwa myahudi aliyeangukia kwenye mikono ya wanyang’anyi zaidi hata ya wayahudi wenyewe… Hiyo Ikifunua kuwa ujirani sio tu kwa mtu wa imani moja na wewe, au wa Taifa moja na wewe, au rangi moja na wewe.. hata mtu mwenye itikadi tofauti kabisa na zetu, huyo tumeamriwa tumpende na hata kumfadhili pale inapobidi.

Na ndicho Bwana YESU alichokuwa anajaribu kukipanda kwa wayahudi kwamba kama vile Mungu aliyemtakatifu anavyowanyeshea mvua yake wenye haki na wasio haki, na sisi pia hatuna budi kunyesha mvua zetu za upendo na Baraka kwa wanaofanana nasi na wasiofanana nasi, kama vile Mungu anavyowaangazia Jua lake waovu na wema, na sisi hatuna budi kuangaza fadhili zetu kwa watu wote (wenye haki na wasio haki), huo ndio ujirani mwema.

Lakini tukijifunga kwa imani zetu, jamii zetu, itikadi zetu na kuwadharau wengine wote na hata kutoonyesha upendo, basi tufahamu kuwa tumejifungia wenyewe fadhili za MUNGU.

Bwana Yesu atasaidie sana, kwasababu kwa nguvu zetu hatutaweza.. pale tunapoambiwa “tumpende adui”.. ni jambo zito sana… Lakini kwasababu yupo Roho Mtakatifu aliyewekwa kutusaidia udhaifu wetu, basi tutaweza na kushinda na zaidi ya kushinda..

Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Maran atha!a

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

About the author

Nuru ya Upendo administrator

2 comments so far

Kaylin MayoPosted on12:12 pm - Oct 4, 2025

I’m often to blogging and i really appreciate your content. The article has actually peaks my interest. I’m going to bookmark your web site and maintain checking for brand spanking new information.

Leave a Reply