Bwana alimaanisha nini kusema “Yeye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo”? (Mathayo 23:20)

Bwana alimaanisha nini kusema “Yeye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo”? (Mathayo 23:20)

Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri, turejee mistari hiyo (kuanzia ule mstari wa 16 -22).

Mathayo 23:16  “Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.

17  Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu?

18  Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga.

19  Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka?

20  Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.

21  Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake.

22  Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake”.

Shabaha kubwa ya Bwana YESU hapo si kuhalalisha VIAPO, Kwamba ni halali Mtu kuapa kwa Hekalu au kwa maadhahabu!.. La! Hiyo haikuwa shabaha yake kwani tayari alishaonya kuhusu viapo katika Mathayo 5:33-37.

Mathayo 5:33 “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;

34  lakini mimi nawaambia, USIAPE KABISA; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;

35  wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.

36  Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37  Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu”.

Na Pia Mtume Yakobo akaliandika jambo hilo hilo katika Yakobo 5:12.

Kwahiyo lengo la Bwana YESU halikuwa kuhalalisha viapo, bali ni kuonyesha UOVU na UNAFIKI wa viongozi hao wa kiyahudi (Mafarisayo na Masadukayo na waandishi) kupitia viapo vyao!. Kwamba wanavipa nguvu viapo vya sadaka Zaidi ya viapo vya Hekalu ambalo ndani yake lina Mungu na sadaka pia…Lakini wenyewe wanatazama sadaka tu!.

Maana yake ni kwamba kama Mtu ameapa kutoa sadaka (dhahabu au kitu kingine chochote) basi amejifunga (maana yake ni lazima atimize kiapo chake hicho, na asipotimiza ni dhambi kubwa)..lakini kama ameapa tu kwa kwa hekalu (labda kuabudu siku hiyo hekaluni, na asiabudu), basi sio kosa kubwa sana!!..

Ila kwa upande wa dhahabu (sadaka), ni kosa kubwa! Pasipo kuona kuwa Hekalu/Madhabahu ni kuu kuliko sadaka! Kwamba aliyeapa kwa Hekalu kaapa jambo kubwa sana kuliko yule aliyeapa kwa sadaka (dhahabu) peke yake itolewayo Hekaluni… kwasababu ndani ya Hekalu ndiko kwenye taratibu zote za matoleo, na si ndani ya matoleo ndio kwenye Hekalu…Ila Mafarisayo walikuwa hawalioni hilo, na ndio maana Bwana YESU anawaita vipofu.

Na kwanini walikuwa wamevipa hadhi kubwa viapo vya sadaka kuliko vya Hekalu??… Hakuna sababu nyingine Zaidi ya kwamba walikuwa wanapenda fedha!!!, walijua ya kwamba wakiwabana watu katika matoleo basi watanufaika Zaidi, hivyo walijali matoleo kuliko Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu yake..

Na jambo hilo hilo utaona Bwana YESU alilirudia juu ya “vile vipasavyo kuwasaidia wazazi”..ambapo Mafarisayo walisema endapo mtu akipata chochote na kile anaweza kukifanya chote wakfu (yaani Korbani) na wala asiwape chochote wazazi, na isiwe dhambi!… jambo ambalo ni baya sana! (soma Marko 7:11).. na kwa maelezo marefu juu ya habari hiyo ya Korbani fungua hapa >>>>Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

Mfano kamili wa baadhi ya viongozi wa kiimani wa leo??…. Utaona wanathamini Matoleo Zaidi ya Hekalu la Mungu na taratibu zake. Utaona mtu akiahidi kuja kanisani na asije, haiwi shida….lakini hebu mtu aahidi kutoa halafu asitoe!, inakuwa ni vita vikali na ni laana kubwa!…pasipo kujua kuwa nyumba ya Mungu ni kuu kuliko sadaka, kwasababu ndani ya nyumba ya Mungu kuna matoleo!.. (Na mtu akiiheshimu nyumba ya Mungu ataheshimu pia matoleo).

Bwana atusaidie sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ipi tofauti kati ya matoleo na sadaka?

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

UJIO WA BWANA YESU.

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments