Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

Jibu: Turejee maandiko machache..

“Uhai” ni hali ya kuwa “HAI” (yaani kuishi) ili kiumbe kiwe kinaishi ni lazima kipumue, kile, kikue na hata kijongee. Hizo ndizo tabia chache za viumbe HAI,  Wanadamu, wanyama na mimea vyote vina uhai kwasababu vinapumua, vinaongezeka na pia kujongea.

Lakini “UZIMA” Umeenda mbali zaidi kuelezea UHAI wa kiroho ambao unapatikana kwa mtu kuwa na mahusiano na MUNGU.

Uhai unaelezea mwili lakini Uzima unaelezea roho. Mimea haina UZIMA bali ina UHAI.. wanyama hawana UZIMA bali wana UHAI maandiko yanaonyesha hivyo…

Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri UHAI WA MNYAMA WAKE; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.

Na UZIMA unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO,

Yohana 10:10 “Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, kisha wawe nao tele”.

ikiwa na maana kuwa wanadamu yoyote aliye nje ya YESU KRISTO anao “Uhai” tu kama wanyama lakini hawana “Uzima”… anapumua, anakula, anatembea lakini akisha kufa hana UZIMA tena.. Lakini aliye ndani ya KRISTO, hata akiwa amekufa ataendelea kwasababu anao  UZIMA wa MILELE alioupokea kutoka kwa YESU.

Je unao uzima wa milele ndani yako?…Je YESU ni sehemu ya maisha yako?

Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape UZIMA WA MILELE.

3 Na UZIMA WA MILELE ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.

Uzao wa Ibrahimu unamilikije mlango wa adui? (Mwanzo 22:17)

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments