FUNDISHA KILE UNACHOKITENDA NA KUKIISHI

FUNDISHA KILE UNACHOKITENDA NA KUKIISHI

Kamwe usifundishe kitu ambacho wewe mwenyewe hukitendi.. Usiwafundishe wengine kumcha MUNGU ilihali wewe mwenyewe uko mbali na MUNGU!.. Usiwafundishe wengine umuhimu wa kuomba ilihali wewe mwenyewe hufanyi hivyo..

Kuna madhara makubwa ya kuwafundisha watu kitu ambacho wewe mwenyewe hukifanyi au hukiwezi.. Katika Biblia walikuwepo Mafarisayo ambao walikuwa wanawatwika watu mizigo ambao wao wenyewe hawakuiweza..

Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa;

3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi.

4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao”.

Na tena kitabu cha Warumi kinazidi kuliweka hilo vizuri zaidi…

Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?

22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?

23 Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati?

24 Kwa maana jina la Mungu latukanwa katika Mataifa kwa ajili yenu, kama ilivyoandikwa”.

Mitume wa Agano jipya pamoja na Manabii wa agano la kale, hawakuwahubiria watu vitu wasivyoviishi wao, bali waliwafundisha watu yale wanayoyaishi ili wawe vielelezo..

Ezra 7:10 “Kwa maana huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake KUITAFUTA sheria ya Bwana, na KUITENDA, na KUFUNDISHA maagizo na hukumu katika Israeli”.

Hapa Ezra kwanza alianza kwa KUITAFUTA sheria ya Bwana, na AKAITENDA na ndipo AKAWAFUNDISHA wengine..  Ni lazima na sisi tupitie hizi hatua tatu; KUTAFUTA, KUTENDA na KUFUNDISHA.

Tukiiruka ile ya kwanza na ya pili na kuifanya hiyo ya Tatu ya kufundisha, hatutakuwa mashahidi wazuri, na wala ushuhuda wetu hautakuwa na nguvu, tutakuwa ni mashabiki wa injili na si wahubiri wa Injili.. Injili inahubiriwa kwanza katika matendo ndipo mafundisho, hatuwezi kufundisha tusichokitenda!, hapo tutakuwa waongo, au watu wa kutafuta faida zetu.

Bwana YESU atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.

TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.

MATENDO YETU YANAPIMWA KATIKA MIZANI.

Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?

Utakuwa Kichwa na si Mkia maana yake nini? (Kumbukumbu 28:13).

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments