TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.

TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.

Shalom, nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima pamoja.

Muda mfupi kabla ya Bwana Yesu kwenda kutukuzwa na maelfu ya watu kule Yerusalemu lipo agizo ambalo aliwapa wanafunzi wake wawili, na agizo lenyewe lilikuwa ni kwenda kumletea mwana punda aliyekuwa amefungwa mahali Fulani. Wengi wetu tunaweza kuona lile lilikuwa ni agizo jepesi, lakini kiuhalisia halikuwa jepesi kama tunavyodhani, kwani walipotumwa walioambiwa sio wakaombe wapewe, hapana bali wakachukue, kana kwamba  hao punda walikuwa ni wa kwao.

Embu tusome kidogo;

Luka 19:29 “Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi,

30 akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa.

31 Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji.

32 Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia.

33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda?

34 Wakasema, Bwana ana haja naye”.

Utajiuliza ni kwanini, Bwana atumie kauli hiyo, mfungue na sio waombeni mniletee? Unadhani hakujua kanuni za kuchukua mali za watu wengine? Alijua sana, lakini si kila wakati aliruhusu hilo, pengine wale wanafunzi walisema kwanini Bwana asituambie tukaanze na kuomba kwanza, si tutapewa tu, kuliko kwenda na kufungua wanyama ambao si wetu, si tutaitwa wezi?

Ni sawa na leo hii mtu akuambie, nenda pale mlimani city, utakuta gari limepakiwa, ingia kisha piga ufunguo, endesha uniletee, bila shaka utasema huyu mtu hanitakii mema bali mabaya.. anataka nikachomwe moto kama mwizi.

Lakini Kristo alikuwa na sababu kufanya vile, alijua mwisho wake utakuwaje..Vilevile alijua madhara ya kutanguliza kuomba omba vibali kwenye kazi yake, alijua milolongo ambayo wangekutana nayo, alijua vikwazo ambavyo shetani angevizusha mahali pale..pengine nyie ni wakina nani, mmesajiliwa wapi, shughuli yenu ni nini, hatuwatambui hapa mtaani, msimgolee yule punda, elimu yenu ni ipi, leta uthibitisho kwanza wa barua kutoka kwa huyo Bwana wenu, n.k. vinginevyo tutawashitaki..

Lakini wao hawakuongea chochote walipofika, badala yake walianza kufanya kama Yesu alivyowaagiza, kufungua punda na pengine katika hatua ya mwisho kabisa pale walipoanza kuondoka, ndipo wahusika walipowaona, na kuwauliza nyie mnafanya nini hapo? Mnawapeleka wapi hao punda?..Wakasema Bwana anawahitaji..

Sasa wale kuona tayari punda wao wameshafunguliwa na gharama imeshaingiwa, kuwarudisha itakuwa ni hatua ndefu sana wakaona ni bora wawache tu, pengine wawape masharti Fulani madogo ya kuwatumia, au walipie gharama Fulani kidogo tu. Hilo halijalishi maadamu punda wameshapatikana.

Vivyo hivyo na hata sasa, usitegemee kwanza ruhusu za watu kufanya jambo lolote la ki-Mungu, ni ngumu sana kusikilizwa au kusapotiwa, fanya kwanza kisha baadaye wakikuuliza kwanini ulifanya waambie ni kwababu Yesu aliniagiza..hata wakikasirika lakini tayari ulishafanya, lile agizo la Yesu litakulinda.

Vikwazo vya shetani ni vingi sana, unaweza ukajikuta haumfanyii Mungu lolote kisa, visheria Fulani vidogo vidogo, au viutaratibu Fulani vinakubana. Wewe fanya tu agizo lake litakulinda mbele ya safari. Unaweza hata usifanya huduma kisa hujakamilisha taratibu hii au ile, hayo tumeyaona sana sehemu nyingi, usingojee kukamilisha taratibu za wanadamu kwanza, endelea na taratibu za Mungu, kisha hizo za wanadamu zitafuata baadaye watakapokuuliza..kwasababu ukisema uanzie kwao, utavunjika moyo mapema mpendwa. Vikwanzo ni vingi kila kukicha.

Bwana Yesu alishatoa agizo, enendeni ulimwenguni kote, mkuhubiri injili kwa kila kiumbe. Hilo agizo halisemi, mkaombe kwanza kuhubiri, hapana, wewe kahubiri kwa jinsi Mungu alivyokujalia kisha wakikufuata, waeleze hilo ni agizo la Yesu. Kwa kufanya hivyo Yesu mwenyewe atafungua njia ya kukusaidia, atakuwekea wepesi, au kupewa kibali cha kuendelea na kazi ya Bwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

EPUKA KUUNDA MATARAJIO YAKO, KWENYE AHADI ZA MUNGU.

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

Baghala ni nini katika maandiko?(2Wafalme 5:16).

Mafundisho

Fitina maana yake nini kwenye biblia?

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments