Nyakati za Mwisho na Tumaini la Utukufu kwa Mwamini Mpya

Nyakati za Mwisho na Tumaini la Utukufu kwa Mwamini Mpya

Kama mwamini ni lazima ujue kila kitakachotekea siku za mwisho, na kile Mungu alichokiahidi kuhusu maisha yajayo

Siku za mwisho zilianza wakati ule wa pentekoste Roho alipomiminwa duniani, kwa watu wote, na hizo zinaendelea hadi sasa mpaka wakati ambapo Kristo atatokea ulimwengu kwa mara ya pili kuleta hukumu na ufalme wake mpya.

Ni ukweli usiopingika kwamba tupo ukiongoni kabisa mwa siku za mwisho.Ingawa Biblia haitupi tarehe kamili (Mathayo 24:36), inatupa ishara na maagizo ya kuwa macho na wenye tumaini wa siku hiyo kuu.

1) Baadhi ya Matukio Muhimu ya Nyakati za Mwisho ni kama yafuatayo:

  •  Injili kufikishwa kwa mataifa yote. (Mathayo 24:14).
  • Dhiki kuu — mateso na majaribu makali (Mathayo 24:21; Ufunuo 13)
  • Kuongezeka kwa maovu na maasi (2 Wathesalonike 2:3)
  • Kuibuka kwa Mpinga Kristo (1 Yohana 2:18; 2 Wathesalonike 2:4)
  • Kurudi kwa Yesu katika utukufu (Mathayo 24:30)
  • Ufufuo wa wafu na hukumu ya mwisho (Yohana 5:28-29)

Hii inaonyesha kwamba historia inaelekea kwenye mwisho ulioamriwa na Mungu.

2. Kurudi kwa Yesu Kristo

Yesu aliahidi atarudi tena (Yohana 14:3). Kurudi kwake hakutakuwa kwa siri, bali kutakuwa kwa utukufu, nguvu na hukumu.

[11]Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
. — Matendo 1:11

Ukweli uhusuo Kurudi Kwake:

  • i) Utaonekana na wote (Ufunuo 1:7)
  • ii) Utakuwa ghafla (Mathayo 24:27)
  • iii) Utakuwa katika utukufu mkubwa (Mathayo 24:30)
  • iv) Yesu atarudi akiwa na malaika na watakatifu wake (1 Wathesalonike 3:13)

Katika siku hiyo:

  • Uovu wote utaangamizwa (2 Wathesalonike 1:7-10)
  • Shetani atahukumiwa (Ufunuo 20:10)
  • Ufalme wa Mungu utaonekana kikamilifu (Ufunuo 11:15)

 3. Tumaini la Utukufu

Hili si tumaini la kubahatisha — ni matumaini ya hakika yaliyowekwa juu ya ahadi za Mungu.

“Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.” — Wakolosai 1:27

Utukufu” Ni Nini?

Kimaandiko, utukufu humaanisha:

Uwepo wa Mungu unaoonekana (Kutoka 33:18-20)

Utakatifu wake ulio mkuu na mkamilifu (Isaya 6:3)

Hali ya mwisho ya waamini — kufanana na Kristo milele (Warumi 8:17; 2 Wakorintho 3:18)

 4. Nini Kinamngojea Mwamini?

  1. Mwili wa utukufu.

1 Wakorintho 15:52
[52]kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

Hakutakuwa na ugonjwa, uchovu, wala mauti tena. Tutakuwa na miili kama wa Yesu baada ya kufufuka kwake (Wafilipi 3:20-21).

ii) Makao ya Milele

Yesu amekwenda kutuandalia  makao (Yohana 14:2). Mbingu mpya na dunia mpya hazitakuwa na huzuni, machozi wala laana (Ufunuo 21:1-5).

iv) . Kumwona Mungu Uso kwa Uso

Hatutamtazama tena kwa imani bali tutamwona moja kwa moja (Ufunuo 22:4). Tutamtumikia na kumtukuza milele (Ufunuo 22:5).

 5. Kuishi kwa fikra za Milele

🔸Kuwa Macho

Kanisa la kwanza liliishi kwa umakini mkubwa. Wakijua kuwa Yesu anaweza kurudi wakati wowote (Tito 2:13).

→ Usicheleweshe toba wala kuwa mzembe kiroho.

🔸Ishi Maisha Matakatifu

“Kila mwenye tumaini hilo ndani yake hujitakasa, kama Yeye alivyo mtakatifu.” — 1 Yohana 3:3

Ufahamu wa kurudi kwa Kristo unapaswa kutuchochea kuishi maisha ya utakatifu na utii.

🔸 Kuwa na Tumaini

Tufahamu kuwa Majaribu haya ni ya muda. Tumaini letu ni nanga ya roho zetu (Waebrania 6:19).

🔸 Tembea na Ujumbe kwa wengine.

Milele ni halisi. Ndio maana tunahubiri Injili—kwa sababu maisha ya watu yana hatma ya milele.

 Tafakari ya Mwisho:

“Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo!” — Ufunuo 22:17

 “Amina. Njoo, Bwana Yesu.” — Ufunuo 22:20

Sauti ya kanisa si hofu, bali ni shauku. Nyakati za mwisho si mwisho wa matumaini, bali ni mwanzo wa utukufu wa milele kwa wote waliomo ndani ya Kristo.

Mafundisho ya ziada kuhusu Siku za Mwisho.

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.

SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.

Jehanamu ni nini?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>  https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments