MIMI NIKO AMBAYE NIKO

MIMI NIKO AMBAYE NIKO

Musa alipomwuliza Mungu kuhusu jina lake, alitarajia kuwa atapewa jina Fulani maalumu kama vile jina la miungu mingine yoyote ijulikanayo mfano wa Baali, au arishtoreth, n.k.

Lakini tunaona Mungu alimjibu kwa ujumla na kumwambia, wakikuuliza jina langu waambie kuwa MIMI NIKO AMBAYE NIKO

Kutoka 3:14 Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli;MIMI NIKO amenituma kwenu.

Sasa kama ukitazama biblia yako kwa chini utaona imeeleza kwa tafsiri nzuri zaidi hiyo sentensi. Akiwa na maana kuwa NITAKUWA KAMA NITAKAVYOKUWA.

Yaani mimi sina jina moja maalumu, lenye sifa Fulani. Bali nitatambulika pindi niwapo katika hilo tukio, au tatizo au haja hiyo jina langu. Na kweli ndivyo ilivyokuwa baada ya pale. Tunaona Farao alipogoma tu, kuwaruhusu wana Israeli kutoka Misri tena kwa adhabu ya kuwaongezea kazi, ndipo hapo Mungu akaanza kujifunua kwa majina yake. Akamwambia Musa, kwa jina langu Yehova nilikuwa sijajifunua, sasa nitakwenda kujifunua, kwa jina hilo,

Kutoka 6:1 Bwana akamwambia Musa, Sasa utaona nitakavyomtenda Farao; maana kwa mkono hodari atawapa ruhusa kwenda zao, na kwa mkono hodari atawafukuza katika nchi yake. 

2 Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 

3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao. 

4 Tena nimelithibitisha agano langu nao, la kuwapa nchi ya Kanaani; nchi ya kukaa kwao hali ya ugeni. 

5 Na zaidi ya hayo, nimesikia kuugua kwao wana wa Israeli, ambao Wamisri wanawatumikisha, nami nimelikumbuka agano langu. 

6 Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa; 

7 nami nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ni YEHOVA, Mungu wenu, niwatoaye mtoke chini ya mizigo ya Wamisri. 

8 Nami nitawaleta hata nchi ile ambayo naliinua mkono wangu, niwape Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; nitawapa iwe urithi wenu; Mimi ni YEHOVA

Umeona? Jina la Mungu lililowatoa wana wa Israeli Misri ni jina la Yehova. Na baada ya hapo tunaona sehemu mbalimbali akijifunua kwa majina mengine mengi, kama Yehova yire, Yehova Nisi, Yehova shama, Yehova shalom, Ebenezeri, n.k. nyakati za vita, za mahitaji, za huzuni n.k. Kulingana na jinsi alivyowasaidia watu wake, walipomlilia.

Na mwisho kabisa akajifunua kwa jina kuu la UKOMBOZI, ambalo ni YESU, lenye maana ya Yehova-mwokozi.  

Hii ni kufunua nini?

Yatupasa tumwelewe Mungu wetu sikuzote kama “NITAKUWA KAMA NITAKAVYOKUWA”. Hana mipaka ya kujifunua kwake kwetu, nyakati za mahitaji atajifunua, nyakati za raha atajifunua, nyakati za magumu atajifunua, mabondeni atajifunua tu kwako, milimani ataonekana tu, yeye ni vyote katika yote. Uwapo visiwani, uwapo jangwani, uendapo mbinguni, ushukapo mahali pa wafu utamwona tu Mungu wako. Hakuna mahali hatajidhihirisha kwako. Pindi tu umwaminipo. Huhitaji kuwa na hofu na wasiwasi na kumwekea mipaka kwamba kwenye jambo hili au hili hataweza kuwepo au kujidhihirisha.

Swali ni je! Umemwamini Mungu aliyejifunua kwako kama mwokozi? Yaani Kristo? Kumbuka, kabla hujasaidiwa kwingine kote na yeye , unahitaji kwanza uokolewe, kwasababu umepotea katika dhambi, na mshahara wa dhambi ni mauti. Leo hii ukimwamini Yesu atakupa ondoleo la dhambi zako, utakuwa na uzima wa milele. Na utaufurahia wokovu kwasababu utakuwa tayari umevukishwa kutoka mautini kwenda  uzimani. Kumbuka hizi ni siku za mwisho. Itakufaidia nini uachwe katika UNYAKUO, angali nafasi unayo leo.Geuka umfuate Kristo.

Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako, basi wasiliana na namba zetu chini kwa msaada bure wa kuokoka.

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

JE! MUNGU NI NANI?

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments