Kuzimu ni mahali, ambapo roho za watu waliokufa zinakwenda..Ni sehemu ya rohoni ambayo haionekani kwa macho ya kibinadamu..
JE! WANAOENDA KUZIMU NI WATU GANI?
Wanaoenda kuzimu ni watu ambao wameasi Neema ya Yesu Kristo, wale wote ambao waliikataa Neema ya Msalaba iliyoletwa na Mwana wa Mungu Yesu Kristo, watahesabika kuwa na hatia ya kuingia kuzimu…Kwasababu biblia inasema tunahesabiwa haki kwa Neema, ambayo hiyo inatokana na Imani ya kumwamini Yesu Kristo.
Kwahiyo mtu anapokufa, katika dhambi (Yaani nje ya Neema ya Yesu Kristo) anashuka moja kwa moja kuzimu, ambako huko kuna mateso makali, na roho yake inakuwa imefungwa. Atakaa huko mpaka wakati wa mwisho wa KITI CHEUPE CHA HUKUMU, Ambapo biblia inasema wafu wote watafufuliwa na kisha kuhukumiwa kulingana na matendo yao, hivyo mtu aliyekufa katika dhambi atasimama siku ile mbele ya kiti kile cheupe cha Hukumu na kisha kuhukumiwa sawasawa na matendo yake. Na baada ya kuhukumiwa atahamishwa kutoka kuzimu alipokuwepo na kuhamishiwa katika ZIWA LA MOTO, Ambako kuna matezo mengi zaidi..
Kinyume chake wanaokufa katika haki sasa, wanakwenda mahali panapoitwa Paradiso, mahali pa raha, wakingojea ufufuo wa Unyakuo ambapo watafufuliwa na kuvaa miili ya Utukufu na kisha kwenda Mbinguni kwa Bwana.
Je Umempa Bwana Yesu maisha yako? Upo ndani ya Neema ya Yesu Kristo, au unasubiria ufe na kwenda kuzimu? Kumbuka hakuna nafasi ya Pili ya kutubu baada ya kushuka kuzimu..Kila atakayeingia kuzimu atasubiria adhabu ya ziwa la moto.
Bwana akubariki!
Mada Nyinginezo:
KUMWAMBIA MTU MWENYE DHAMBI KUWA ATAKWENDA KUZIMU ASIPOTUBU JE! NI KUHUKUMU?
NITAAMINI VIPI KAMA KUNA MBINGU AU KUZIMU?
JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.
UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.
About the author