YATOE MAISHA YAKO KWA YESU.

YATOE MAISHA YAKO KWA YESU.

Kuna tofauti ya kutoa uhai, kutoa mali, na kutoa maisha…Unapotoa uhai wako kwa Yesu maana yake unakuwa tayari kufa kwa ajili ya Kristo, unapotoa mali maana yake unatoa sehemu ya vile unavyomiliki kwa Kristo, na hivyo vinaweza kuwa fedha, hazina au milki yako yoyote ile….Lakini kuna kitu kingine cha muhimu ambacho ndicho tutakachokizungumzia leo…Na hicho ni kutoa maisha kwa Yesu.

Kuyatoa maisha yako kwa Yesu maana yake kuanzia huo wakati maisha yako sio milki yako wewe bali yake yeye…Hii ni sadaka kuu na ya kwanza na ya muhimu kuliko zote. Na maisha sio kipindi cha siku kadhaa, au wiki kadhaa bali ni kipindi chote chako cha kuishi ambacho kinaweza kikafika hata miaka 90. Ni kipindi cha kuweka chini mipango yako, na kuichukua mipango yake…ni kipindi si cha kuishi tena kama utakavyo wewe, bali atakavyo yeye..ni wakati wa kuvua nira zako ulizojivisha, na zile shetani alizokuvisha na kuzivaa nira za Yesu…ni wakati wa kutua mizigo yako binafsi uliyojitwisha na ile uliyotwishwa na shetani na kuibeba mizigo ya Yesu Kristo.

Unatoka kuwa mtumwa wa wanadamu na shetani na kuwa mtumwa wa YESU. Kitu kimoja kisichofahamika na wengi ni kwamba Yesu anapotutoa katika utumwa wa shetani..huwa hatuachi tu huru bila kuwa na shughuli yoyote…badala yake anatutwika mzigo wake,…maana yake tunaifanya kazi yake..na anapotuvua nira ya adui, ni ili atuvike nira yake yeye…ingawa yake ni laini na si ngumu kama ile ya Yule adui..Ndivyo maandiko yanavyosema katika..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Umeona?..Bwana na yeye anao mzigo wake..na vile vile anayo NIRA. Hivyo tunapompa Yesu maisha maana yake tunajiuza chini ya utumishi wake mpaka siku tutakayoondoka hapa duniani. Ndio maana Mtume Paulo karibia kila mwanzo wa nyaraka zake alianza na maneno haya…

Filemoni 1:1 “Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo aliye ndugu yetu, kwa Filemoni mpendwa wetu, mtenda kazi pamoja nasi,…..9 lakini, kwa ajili ya upendo nakusihi, kwa kuwa ni kama nilivyo, Paulo mzee, na sasa mfungwa wa Kristo Yesu pia”…

Kasome pia Waefeso 3:1,4:1,Tito 1:1..

Mtume Paulo ni mfano wa watu walioyatoa maisha yao kwa Kristo…Na sisi hatuna budi tuwe vivyo hivyo…maana yake maisha yetu kuishi ni Kristo na kufa ni faida.

Lakini ukijiona unaishi lakini upo huru, kufanya dhambi…upo huru kuishi utakavyo basi jua bado hujawekwa huru na Kristo,kwasababu ukiwekwa huru na Kristo ni lazima akuvishe nira zake yeye na akutwishe mizigo yake…Sasa nira ya Yesu iko wapi Maishani mwako?..wewe ni mlevi ukiambiwa unasema Kristo kakuweka huru..bado hujawekwa huru…wewe ni mtumwa wa dhambi bado…maisha yako bado hujayatoa kwa Yesu.

Neno la Mungu leo linakufikia kwa njia hii, pengine ulishalisikia…Lakini sasa ni wakati wa kugeuka na kumpa Yesu maisha yako…Amua kuukataa utumwa wa shetani na kusudia kuuvaa utumwa wa Bwana Yesu, ambao amesema mzigo wake ni mwepesi na nira yake ni laini, tofauti na hiyo ya dhambi uliyoivaa..

Hivyo unachopaswa kufanya ni hapo ulipo ni kutenga muda mchache binafsi na kuomba rehema na kumwambia Bwana aingie maishani mwako, ayaongoze maisha yako na wewe uwe wake…usisome habari hizi kama hadithi tu ya kukusisimua, bali uchukue hatua…na baada ya kuomba kusudia kuacha yote uliyokuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu..na baada ya hapo, katafute ubatizo sahihi, kwaajili ya kukamilisha wokovu wako…kabla ya kukitumia kijiko ni lazima ukioshe, na wewe kabla Bwana hajaanza kukutumia ni lazima akuoshe kwenye maji mengi kwanza kitakate…hivyo na wewe nenda katafute ubatizo sahihi kwa gharama zozote kwani ni wa muhimu sana, na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38,8;16,10:48,19:5) na Roho Mtakatifu atashuka juu yako kukufanya mtumishi wake…

Nakukumbusha kuwa tunaishi katika siku za mwisho, na Kristo yupo mlangoni kurudi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAP

Mada Nyinginezo:

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

USIHUSISHE HISIA KATIKA KUMTOLEA MUNGU.

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

 

USIHUSISHE HISIA KATIKA KUMTOLEA MUNGU.

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments