Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

SWALI: Paulo alimaanisha nini kusema…”Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia;?

1Wakorintho 14:14 “Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.

15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia”.


JIBU: Hapa mtume Paulo alikuwa anaondoa mkanganyiko uliokuwa unaendelea katika kanisa kuhusiana na karama za rohoni, hususani karama ya lugha. Na mkanganyiko huu unaendelea hata sasa katika kanisa la Mungu.

Lakini kabla ya  kufahamu mtume Paulo alikuwa anamaanisha nini hasaa hapo, ni vizuri tukajua jinsi hii karama inavyofanya kazi. Lugha zinazozungumziwa katika maandiko, ambazo Roho Mtakatifu anazishusha juu ya mtu kwa jinsi apendavyo yeye, zimegawanyika katika makundi mawili.

Kundi la kwanza: Ni lugha za kibinadamu. Mfano kichini, Kiswahili, kimasai n.k.

Kundi la Pili: Ni Lugha za malaika. Hizi hazijulikani na wanadamu,.

Sasa lengo kuu la hizi  lugha ni kama zifuatavyo:

  1. kulijenga kanisa la Mungu (waliookoka),
  2. kuwavuta watu wengine katika wokovu(ambao hawajaokoka).
  3. Na pia kuwasiliana na Mungu katika roho.

Mtu yeyote akimwomba Mungu ampe kunena kwa lugha, atapewa, (1Wakorintho 14:5)..  Lakini pia haiwezi kuwa wakati wote, au ikaja kwa wepesi kama vile mtu yule aliyejaliwa karama hii na Mungu. Mtu aliyepewa karama hii, inakuwa ni rahisi sana kwake kunena, hususani pale anapoanza tu kuomba, hatumii nguvu nyingi, anashangaa ulimi wenyewe unaanza kuzungumza lugha nyingine gheni. Sasa kwa mtu kama huyu anapaswa kujua hiyo ni sehemu ya karama yake, na hivyo anapaswa aelewe ni nini anatakiwa afanye baada ya pale ili karama hiyo iwe ina manufaa kwa ajili ya kanisa la Mungu.

Sasa, jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa hizi lugha zinaposhushwa ndani ya mtu, kwa kipindi cha mwanzoni, huwa haziji na tafsiri yoyote, zinakuwa ni kwa ajili ya yule mtu tu husika (mnenaji), na sio kwa kanisa, hapo ndipo utaona mtu anaweza kunena kwa lugha usiku kucha. Lakini kusiwe na kitu chochote unachokielewa yeye, au yule mwingine anayesikia.

Lakini baadaye kama ataichochea karama yake, kwa kumwomba Mungu, amjalie na tafsiri, ndio inapokuja na tafsiri ndani yake. Na hiyo inakuwa ni kwa faida ya kanisa la Kristo. Hivyo mtu ambaye karama yake inatenda kazi ni yule ambaye akinena katika kanisa, basi na Mungu anamfunulia tafsiri ya maneno yale aliyoyanena, kisha analiambia kanisa.. Na kanisa linajengwa, kwasababu hiyo.

Sasa tukirudi katika jambo ambalo Paulo alilisema.. kuhusiana na upungufu wa maarifa kuhusu karama hizi, ni kwamba watu walikuwa wananena kwa lugha mbele ya kanisa, lakini hakuna tafsiri yoyote ile. Ndipo hapo mtume Paulo akasema, Je! Yule anayesikia, ataelewaje?si atakuona wewe ni mwendawazimu? Akaongezea kusema, kama hutakuwa na tafsiri ya lugha hiyo, basi ni heri ukae kimya uombe kivyako vyako. Kuliko kusimama mbele ya kanisa na huku unatoa lugha ambazo hazieleweki kwa wasikiaji.

Ndipo hapo akasema..

Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia..

Yaani, nitaomba kwa lugha, halafu wakati huo huo ninaomba kwa akili zangu, na sio tena tafsiri ya ile lugha niliyoizungumza bali maneno yangu mengine ya sikuzote.. kwamfano, mtu aanze kuzungumza  kiharabu katikati ya mahubiri, bila kutolea tafsiri yoyote halafu anaendelea kuzungumza Kiswahili chake..wewe kama msikiaji utaelewa nini hapo?..

Ndicho kinachoendelea leo hii, mtu atasema ananena kwa lugha, anapohubiri, lakini hatoi tafsiri ya kile anachokisema, anaendelea na maneno yake ya Kiswahili. Katika mazingira kama hayo, wewe msikiaje unajengekaje?

Vilevile Roho Mtakatifu atakujalia kuimba hata wimbo katika lugha nyingine ya rohoni, halafu hutoi tafsiri yake, Je! Msikaji atajengekaje?

Naamini, kama na wewe ni mmojawapo mwenye karama hii, utafanya marekebisho katika hilo. Na kama umekuwa ukinena tu, huoni tafsiri, basi unawajibu wa kumwomba Mungu kwa bidi akupe na tafsiri, pindi uwapo mbele ya kanisa lake. Kwa msingi huu sasa, naomba upitie vifungu hivi hapa chini, ili uelewe Zaidi.

1Wakorintho 14:10 “Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana.

11 Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu.

12 Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa.

13 KWA SABABU HIYO YEYE ANENAYE KWA LUGHA NA AOMBE APEWE KUFASIRI.

14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.

15 Imekuwaje, basi? NITAOMBA KWA ROHO, TENA NITAOMBA KWA AKILI PIA; MTAIMBA KWA ROHO, TENA NITAIMBA KWA AKILI PIA.

16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo?

17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi.

18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote;

19 lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.

20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima.

21 Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana.

22 Basi, hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

USINIE MAKUU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments