Je! Ni Kristo au Kristu? Lipi ni neno sahihi?

Je! Ni Kristo au Kristu? Lipi ni neno sahihi?

JIBU: Neno Kristo limetoka katika lugha ya kigiriki (Khristos) ambalo likitafsiriwa katika Kiswahili linatamkika kama KRISTO.

Lakini Neno hili hili, kwa lugha ya kilatini  (Christus), likitafsiriwa katika Kiswahili linatamkika kama  KRISTU.

Swali ni Je! Ipi ni tafsiri sahihi?

Tufahamu kuwa biblia yetu  (husasani sehemu kubwa ya agano jipya) haikuandikwa katika lugha ya kilatini, au kiingereza, au kichina, au kifaransa.. Hapana bali iliandikwa katika lugha ya Kigiriki ya kale. Hivyo tafsiri ya biblia yetu ya Kiswahili tunaitolea moja kwa moja kutoka katika lugha hiyo ya kigiriki, na sio kiingereza au kilatino.

 Hivyo ni vizuri tukitumia lahaja ya lugha ya asili, iliyotumika kwenye biblia(Kigiriki) kuliko nyingine.

Japo wapo wanaotumia lahaja ya kilatino (Kristu), pia hawafanyi makosa, maadamu ni Kristo Yule Yule analengwa na sio mwingine. Ni sawa na anayesema ‘Sulemani’ au ‘Solomoni’. Ni Yule Yule mlengwa isipokuwa katika lahaja mbili tofauti.

Maana ya Kristo ni “Mtiwa-Mafuta” Ambapo kwa lugha ya kiyahudi anaitwa “MASIHI”. Hivyo tunaposema Yesu Kristo, tunamaanisha Yesu mtiwa mafuta.  Yaani Yesu aliyeteuliwa na Mungu mahususi kwa kazi ya kuwakomboa wanadamu. Ni yeye tu ndiye mwokozi wa ulimwengu wala hapana mwingine.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

Nini maana ya ELOHIMU?

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

Mharabu ni nani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments