Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”

Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”

Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”.

Kutundua ni kujali mtu kupita kiasi, au kuonyesha wema uliopitiliza.

Hivyo hapo anaposema amtunduiaye mtumwa wake tangu utotoni, mwisho wake atakuwa ni mwanawe. Anamaanisha amjalie mtumwa wake, kupita kiasi, yaani kuishi naye kama sio mtumwa kwake, (kumdekeza), na kama mfano ikiendelea hivyo kwa kipindi kirefu, mwisho wake utakuwa ni kumfanya mwanawe, yaani mrithi.

Zamani enzi za biblia, watu walikuwa aidha wananunua watumwa, au wanawazalisha majumbani kwao, ikiwa na maana kama mtu huyo alikuwa na mtumwa, kisha mtumwa Yule akazaa, sasa wale watoto wanakuwa pia ni watumwa wa Yule bwana.

Na kulikuwa na sheria kwamba kila baada ya miaka 7, mbiu ilipigwa ya kuwafanya watumwa wote huru, hivyo waliotaka kuondoka waliondoka, lakini waliotaka kuendelea, basi waliendelea kwa mkataba mwingine wa miaka saba. Na hivyo mtumwa huyo aliwajibika kutumika ipasavyo muda wote huo wa mkataba wake (Kumbukumbu 15:1-18).

Sasa hapa, biblia inaeleza tabia ya bwana ambaye moyo wake ni wa kitofauti. Bwana ambaye, anatabia ya kumjali sana mtumwa wake kuliko uhalisia, huwenda anamuhurumia, kumwona anafanya kazi nyingi, hivyo anampa kidogo tu, au anapokwenda kwenye sherehe hamwachi nyumbani anakwenda naye pia, hata akiwa nyumbani majukumu anapewa machache sana, anakaa naye mezani pamoja wanacheka n.k… Sasa katika hali kama hiyo, ikiwa mtumwa huyo, atadumu kubaki kwa bwana wake, kwa kipindi kirefu, Yule bwana, atamfanya tu kuwa kama mmojawapo wa mwanawe, maana yake siku atakapotoa urithi, na huyu lazima apewe, kwasababu ameishi kama mtoto wake kwa kipindi kirefu.

Na hii ni kweli, hata katika kipindi hichi, labda mfanyakazi kaajiriwa kwenye nyumba fulani, kisha mwenye nyumba akampenda, akawa naye kwa kipindi cha miaka mingi, mwishowe, atamfanya tu kama mwanafamilia, na hatimaye atapata kitu kama mmojawapo wa watoto wake.

Ni kufunua nini rohoni?

Hii ni Tabia aliyokuwa nayo Mungu kwetu sisi watu wa mataifa.

Tulipokwenda kwake, hatukuwa wana wake, au warithi, bali warithi walikuwa ni wayahudi tu, lakini kwa ukarimu wake, akatutoa katika utumwa na kutufanya WANA, jambo ambalo si kawaida kwa bwana yoyote, kutenda kwa kijakazi aliyezaliwa kusikojulikana. Ndicho alichokuja kukifanya Yesu;

Yohana 15:15  Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.

Yohana 8:35  “Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36  Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.

Hivyo mimi na wewe tunafanyika, WANA na WARITHI, wa Mungu kwa njia ya Bwana Yesu. Haleluya. Utukufu na heshima ni kwa Bwana wetu Yesu!! milele na milele.

Lakini ni nini tunapaswa kukifanya?

Ni kukubali tu kudumu katika nyumba yake. Kama vile mtumwa Yule ambaye aliamua kudumu tangu UTOTONI. Hivyo na wewe umepewa neema, dumu katika neema, dumu katika wokovu, acha kutanga tanga huku na kule. Mungu akaghahiri mema kwako. Ulimwengu hauwezi kukupa unafuu wowote, ni kwa Kristo tu ndio utapata raha nafsini, Hakuna mateso kwa Kristo, Utumwa wake ni mwepesi sana alisema hivyo. Soma (Mathayo 11:28-30).

Ikiwa hujaokoka unasubiri nini sasa? Embu fanya uamuzi wa haraka sana umgeukie Kristo akuokoe. Hizi ni siku za mwisho, anakaribia kurudi kuwanyakua wateule wake. Kama upo tayari kutubu leo dhambi zako, basi fungua hapa kwa  ajili ya mwongozo wa sala ya toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;

Nini maana ya kukunguwazwa (Marko 14:27)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments