MISTARI YA KUOMBEA AMANI YA FAMILIA.

MISTARI YA KUOMBEA AMANI YA FAMILIA.

UTANGULIZI: Neno la MUNGU ni DAWA, iponyayo Nafsi, Mwili na Roho.. Maombi yanayosimamiwa na Neno la MUNGU yanakuwa na nguvu kuliko yasiyo na msingi wa NENO, Hivyo wakati wa kuomba au kuombea jambo fulani, ni vyema Mwamini akawa na maandiko machache ya kusimamia wakati wa Maombi.

MAOMBI YASIYO NA NENO LA KUSIMAMIA ni kama BENDERA ISIYO NA MLINGOTI!!….Hivyo ni vyema kulijua Neno la kulitumia wakati wa Maombi.

        AMANI:

Ikiwa Amani imepungua au imepotea kabisa katika nyumba, ambapo inafikia hatua Baba haelewani na Mama, au wazazi hawaelewani na watoto, au watoto kwa watoto hawaelewani, vurugu imekuwa nyingi jambo ambalo hapo mwanzo haikuwa hivyo…. Na wewe kama Baba, au Mama, au Mtoto uliye na Kristo unaliona hilo na unatamani msaada kutoka kwa Baba wa mbinguni, kurejesha mambo yote yawe sawa.

Basi mistari ifuatayo inaweza kukufaa wakati wa maombi baada ya kuitafakari kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

Zaburi 4:8 “KATIKA AMANI nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama”.

Zaburi 29:11 “Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana ATAWABARIKI WATU WAKE KWA AMANI”.

Zaburi 122: 7 “AMANI NA IKAE NDANI YA KUTA ZAKO, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.

8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, AMANI IKAE NAWE”

Zaburi 147: 14 “Ndiye afanyaye AMANI mipakani mwako, Akushibishaye kwa unono wa ngano”

Ayubu 25:2 “Enzi na hofu zi pamoja naye; HUFANYA AMANI katika mahali pake palipoinuka”

Zaburi 35:27 “Washangilie na kufurahi, Wapendezwao na haki yangu. Naam, waseme daima, Atukuzwe Bwana, Apendezwaye na AMANI YA MTUMISHI WAKE”.

Zaburi 37: 37 “Umwangalie sana mtu mkamilifu, Umtazame mtu mnyofu, MAANA MWISHO WAKE MTU HUYO NI AMANI”.

Zaburi 72:7 “Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi, NA WINGI WA AMANI hata mwezi utakapokoma”

Zaburi 85:8 “Na nisikie atakavyosema Mungu Bwana, MAANA ATAWAAMBIA WATU WAKE AMANI, Naam, na watauwa wake pia, Bali wasiurudie upumbavu tena”.

Zaburi 85: 10 “Fadhili na kweli zimekutana, Haki na amani zimehusiana”

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa Amani”.

Ikiwa utaomba maombi hayo kwa Imani, na kwa ufunuo, na ukiwa umejihakika kwamba njia zako zimetakasika mbele zake basi tegemea majibu yake, kwamaana Neno la MUNGU halijawahi kupita kamwe!, wala kushindwa.

Bwana akubariki.

Usikose sehemu inayofuata juu ya Mistari ya kusimamia katika MAOMBI YA UPENDO WA FAMILIA.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.

TUNA WAJIBU WA KUOMBEA MAHALI TULIPO.

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments