FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.

FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.

(Masomo maalumu yahusuyo Sadaka na Matoleo)

Angalizo: Masomo haya hayana lengo ya kuhimiza matoleo, (Au kuwaweka watu katika mitego ya kutoa) bali yana lengo la kutoa elimu sahihi ya kiMungu juu ya faida za kumtolea Mungu kwa njia yeyote ile.

Na wajibu wa kumtolea Mungu si wa waumini (au washirika tu peke yao) bali wa kila mtu ikiwemo wainjilisti, wachungaji, maaskofu, wazee wa kanisa, mitume, waimba kwaya na wengine wote. Hivyo ni muhimu pia kujifunza mambo haya, ili tupate faida (Isaya 48:17)

2Wakorintho 9:11 “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, UMPATIAO MUNGU SHUKRANI KWA KAZI YETU.

12 Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali HUZIDI SANA KUWA NA FAIDA KWA SHUKRANI NYINGI APEWAZO MUNGU;”

Nataka uone hilo neno.. “HUZIDI SANA KUWA NA FAIDA”… Maana yake ni kwamba pamoja na faida hiyo iliyotajwa hapo ya “kuwatimizia watakatifu riziki zao”..lakini pia Faida iliyo kubwa kupita yote ni hiyo kwamba “MUNGU ATAPEWA SHUKRANI NYINGI”.

Unawasaidia mayatima, wale mayatima watamshukuru MUNGU SANA KWA KILE WALICHOKIPOKEA… Na ndicho Mungu anachokihitaji sana.. SHUKRANI… shukrani.

Unaweza kuona kama shukrani ni jambo dogo!.. lakini kwa MUNGU ni jambo kubwa…

Mungu anapendezwa na shukrani kuliko maombi mengi tuyapelekayo mbele zake… Unaweza kutumia lisaa limoja kumshukuru tu MUNGU kwa mema yake na ukapata faida kubwa kuliko kupeleka mahitaji orodha ya mahitaji kwa muda huo.. (Shukrani ni darasa pana sana na lenye faida kubwa sana kiroho).

Na hapa Neno la Mungu linasema kuwa “shukrani atakazopewa MUNGU kutoka kwa wale waliopokea, basi hizo ni faida kubwa”.

Mtu akimshukuru Mungu kwaajili ya kile ulichotoa, hiyo ni faida kubwa kwako, Maskini akimshukuru Mungu kwaajili ya kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako, Mtumishi wa Mungu akimshukuru Mungu kwaajili kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako, Yatima akimshukuru Mungu kwaajili kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako, Mnyonge akimshukuru Mungu kwaajili ya kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako.

2Wakorintho 9:11 “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, UMPATIAO MUNGU SHUKRANI KWA KAZI YETU.

12  Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Shukrani ni nini kibiblia?

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

HUNA SHIRIKA NAMI.

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments