Baraka ni nini na kuna aina ngapi za baraka?.

Baraka ni nini na kuna aina ngapi za baraka?.

Jibu: Baraka ni thawabu ya kipekee itokayo kwa Mungu na kumfikia mtu akiwa hapa duniani.


Baraka yaweza kutokana na matendo mtu aliyoyatenda au maombi aliyoyaomba.

Kwamfano utamwona mtu anayeitwa Yabesi alimwomba Mungu ambariki na Mungu akasikia na kumbariki.

1Nyakati 4:10 “Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia hozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba”

Baraka za MUNGU zimegawanyika katika makundi makuu mawili;

  1. BARAKA ZA ROHONI.

Hizi ni baraka zinazoinufaisha roho ya mtu na ndizo zenye umuhimu sana kuliko zile nyingine.

Baraka ya kwanza ya rohoni ni “WOKOVU”. Mtu aliyepata Neema ya kumwamini YESU na kuoshwa dhambi zake huyo amebarikiwa, kwasababu anao uzima wa milele.

Waefeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa BARAKA ZOTE ZA ROHONI, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo”.

Baraka ya rohoni inazaa Furaha, amani, utulivu na utakatifu kwa ujumla.

Watu waliobarikiwa rohoni hata wakose vyote vya mwilini bado wanaishi maisha ya raha, kwasababu roho zao zimebarikiwa kuwa ndani ya YESU ambaye kila kitu.

  2. BARAKA ZA MWILINI.

Baraka za mwilini ni vyote ambavyo mtu anavipokea kutoka kwa MUNGU vyenye manufaa ya mwili, ikiwemo afya, cheo, uzao au mali.

Mfano wa watu waliobarikiwa kwa baraka za mwilini ni Sulemani, alipewa utajiri mkubwa hata baada yake hakukuwa na mtu kama yeye,

Na wengine kwenye Biblia agano la kale ni Abramu na Ayubu hawa walibarikiwa vingi na MUNGU.

Lea naye alibarikiwa kuwa na watoto wengi, Samsoni alibariwa nguvu za mwilini n.k

Katika Agano jipya walikuwepo akina Yusufu wa Arimathaya, (Mathayo 27:57), na wanawake si haba, akina Yoana, Suzana na wengine wengi (Luka 8:3).

Na waliobarikiwa kwa vyeo, waliomwamini Bwana YESU walikuwa wengi sana wanaume na wanawake (soma Matendo 17:12-14).

Na kubarikiwa mwilini kunaweza kuwa ishara ya kubarikiwa pia rohoni, lakini sio ishara pekee kwasababu wapo matajiri wasiomwamini YESU na walikuwepo matajiri kabla ya Bwana YESU,

Na watakuwepo matajiri wengi katika ziwa la moto (Soma Luka 16:20-34).

Na tena Bwana Yesu alisema itamfaidia nini mtu apate kila kitu halafu apate hasara ya nafsi yake (Marko 8:34).

Na pia wapo maskini ambao hawajabarikiwa baraka za mwilini lakini wamebarikiwa mambo ya rohoni..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”.

Kwahiyo tukiwa wote ndani ya Kristo, hatupaswi kudharauliana kwa hali zetu, bali tunapaswa tuhudumiane kwa viwango vya baraka tulivyobarikiwa..

kwasababu yule unayemwona ni maskini wa vya mwilini huenda ni tajiri wa vya rohoni sana, ndivyo Neno la Mungu linavyosema..

Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri)…”

Na yule unayemwona hana vya rohoni kama ulivyo navyo wewe basi amebarikiwa vya mwilini, ambavyo kupitia hivyo vinahitajika kwaajili ya injili, ili mambo yote yakae katika uwiano na wote tuheshimiane.

Na pia inawezekeana mtu akabarikiwa kwa vyote vya rohoni na mwilini, kwa mapenzi ya MUNGU, lakini haiwezekani mtu aliyemwamini YESU akakosa vyote..

Ikitokea dalili ya kukosa vyote basi kuna kasoro katika imani, hivyo mtu huyo anapaswa aangalie jinsi alivyosikia na anavyoenenda.

Je umempokea YESU?..huo uchungu na hofu na wasiwasi ni ishara ya kupungukiwa baraka za rohoni.

Leo hii mpokee YESU ili uanze kula matunda ya baraka za rohoni.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAOMBI YA YABESI.

Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;

KILA MTU NA AMCHE BABA YAKE NA MAMA YAKE.

MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments