Title February 2026

KUMBUKA NI AMRI MPYA!

Yohana 13:34

[34]Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. 

Hapo mwanzo nilipokuwa nautafakari huu mstari, nilijiuliza maswali Yesu anaposema “AMRI MPYA..

Ni amri ipi hiyo mpya?

Maana ukitafakari anasema “mpendane” kwani kupendana ni amri mpya?

Mbona ilikuwepo tangu zamani? Na ilijulikana

Mambo ya Walawi 19:18

[18]Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA. 

Kupendana kulifundishwa tangu zamani za torati…lakini mpaka Kristo anasema amri mpya maana yake kupendana anakokusema yeye ni tofauti na kule kulivyodhaniwa…

“Ndio maana akasema…Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.”

Yaani mpendane kwa mfano wa upendo wangu, sio mfano wa upendo mwingine.

Je upendo wa Yesu ulikuwa upi?

Upendo wa upeo.

Yohana 13:1

[1]Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo. 

Upeo ni ukomo wa mwisho kabisa…Yesu hakutupenda kwa wakati fulani tu…bali alitupenda (sisi tuliomwamini) mpaka mwisho, kabisa kutoka moyoni..

Ikiwa na maana alipiga gharama ikitokea huyu amenisaliti, Amenikana, amenizunguka…je nitakoma kumpenda?…hivyo akaamua kukubaliana na yote…liwalo na liwe nimempenda, na nitampenda mpaka mwisho..

Ndio maana ijapokuwa alijua Yuda atamsaliti, na Petro atamkana, hakuacha kuwapenda…sasa huo ndio upendo wa Kristo mpya..upendo wa upeo

Leo ni rahisi kupenda mtu kwa mema, au mazuri anayoyadhihirisha sasa…lakini ikitokea baadaye yule uliyemsaidia anakusaliti, uliyemhudumia anakudharau, uliyemsomesha hatimaye amekuwa na cheo kikubwa kuliko wewe sasa anakucheka,..hapo hapo unaanza kuumizwa, hata kumchukia, na kumlalamikia…sasa huo sio upendo wa upeo….ni upendo wa nyakati…lakini ikiwa anakutendea mambo yote hayo halafu hujali hapo ndio upendo ule mpya wa Kristo anapodhihirika.

Bwana anataka tupige gharama ya kuanzia mwanzo hadi mwisho…ukiamua kumpenda mtu..basi mpende daima. Bila sharti.

Upendo mpya.. ni ule wa kupenda wanaokuchukia, ule wa zamani ulikuwa mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.(Mathayo 5:43-44).. kilele cha upendo huu mpya ni kuwa tayari kugharimika lolote kwa ajili ya wengine..(Yohana 15:13)

Je amri hii mpya tunayo?

2 Yohana 1:5

Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane. 

Bwana awe nawe.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

Print this post

LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.

1 Samweli 30:6

[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake. 

Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.

Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe, 

Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe, 

Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..

Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.

Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.  

Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu. 

Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.

Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.

Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

KATIKA UOVU MGEUZWE WATOTO WACHANGA

1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika UOVU MGEUZWE WATOTO WACHANGA, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”.

Biblia inatufundisha kuwa “Watu wazima” katika Akili, lakini tuwe watoto wachanga katika uovu, sasa ni nini maana ya kuwa watoto wachanga katika uovu?

Tukiwatazama watoto wachanga tunajifunza mengi, lakini jambo kuu tunaloweza kujifunza ni “Ukamilifu” watoto wadogo wanyonyao wanakuwa hawana hatia, sio waongo, si waasi, si walevi, si wazinzi, si wauaji, si wadhalimu, si wahuni, si waasi na mambo mengine maovu hayapo kwao, Na ndio maana Bwana YESU alisema kuwa ni lazima na sisi tugeuzwe kitabia na kuwa kama watoto wachanga..

Mathayo 18:3 “akasema, Amin, nawaambia, MSIPOONGOKA NA KUWA KAMA VITOTO, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni”.

Lakini haishii tu kusema tuwe “watoto katika uovu” bali pia tuwe “watu wazima katika akili”.. Mtu mzima katika akili ni Yule aliyeyabatilisha mambo mabaya, ya kale… mtoto anayechezea matope na kupenda kula peremende kila siku anapokuwa mtu mzima, ndipo anapoyabatilisha mambo ya kitoto na kuwa mtu mzima (hapo tunasema ameimarika kiakili).

Vile vile mtu ambaye alikuwa katika machafu ya dunia (ambayo ndio mfano wa uchafu wote wa utotoni), anapompokea YESU basi ya kale yanakuwa yamepita na sasa amekuwa kiumbe kipya.

2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Lakini mtu aliye nje ya imani, na kuendelea na machafu yote ya dunia, kibiblia anakuwa hana akili, na anafananishwa na mnyama.

Zaburi 49:20 “Mwanadamu mwenye heshima, IWAPO HANA AKILI, Amefanana na wanyama wapoteao”.

Ndio kwani biblia imesema mtu aziniye hana akili kabisa (soma Mithali 6:32, Mithali 7:7), na mtu anayemdharau mwenzake pia hana akili (Mithali 11:12).

Kwahiyo ni lazima tuache mambo ya kale, na kumgeukia Kristo, ili tupate akili, na mwenye uwezo wa kutubadilisha ni YESU tu peke yake, lakini wanadamu wengine wote hawawezi kutusaidia kitu, je umempokea huyu YESU?.. Je unauhakika Kristo akija leo unakwenda naye?.

Kama bado haujampokea YESU unangoja nini?.. maisha ya dhambi na anasa yamekusaidia nini?.. je ukifa leo utaenda wapi?

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Print this post